Jumatano, 30 Oktoba 2013

DHIKI KUBWA



Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

Somo: Dhiki kubwa

Tunajifunza somo hili kwa kuligawa katika vipengele saba.

( i ). Dhiki tofauti na zote

( ii ). Muda wa dhiki kubwa

( iii ). Majina yanayotumika kuzungumzia dhiki kubwa

( iv ) Watakaohusika kuileta dhiki kubwa

( v ). Makusudi ya dhiki kubwa

( vi ) Hali itakavyokuwa wakati wa dhiki kubwa

( vii ). Jinsi ya kuikwepa dhiki kubwa

( I ). DHIKI TOFAUTI NA ZOTE

Wanadamu hapa duniani, wanapitishwa katika dhiki za namna namna. Wanapitishwa katika mateso ya namna namna. Wengine wanapitishwa katika hali nzito ya njaa nchi nzima hali inakuwa mbaya. Nchi ambazo zimewahi kushuhudia njaa kali kama Ethiopia na Somaria, watu watakondeana na kubaki mbavu kabisa.

BARAZA LA MAKANISA KENYA LAUNGA MKONO VIONGOZI WA MAKANISA KUKABIDHIWA BUNDUKI KUJILINDA


Katibu mkuu wa Baraza la makanisa nchini Kenya NCCK mchungaji Peter Karanja. ©Dailynation.
Watu mbalimbali nchini Kenya wakiwemo waumini wa dini ya Kikristo wamepinga wazo lililotolewa na viongozi wa dini hiyo kwamba wakabidhiwe bunduki aina ya AK47 ili kupambana na waumini bandia wa dini ya kiislam nchini humo ambao wamesababisha kifo cha mchungaji pamoja na kuchoma kanisa huko mkoani Mombasa nchini Kenya.

KWA TAARIFA YAKO : ALIYEIMBA "MFALME DAUDI" THE BIG NOVEMBER CRUSADE UNAJUA ALIKO?

Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu


KWA TAARIFA YAKO hii leo mdau wetu ni kuhusiana na mwimbaji aliyewahi kuwika jijini Dar es salaam kutokana na uimbaji na uhamasishaji wake katika kumtukuza Mungu, huyu si mwingine bali ni Allen Kinsalla Lopez mwimbaji huyu alipachikwa jina la "Mfalme Daudi" kutokana na ghani yake ama rap yake ya "Mfalme Daudi, mfalme Daudi alicheza x2 aliicheza nguo zote zikaanguka, tuchezetuchezze kwa BWANA YESU tucheze, turukee turuke kwa BWANA YESU turukee……"rap hii ilipata umaarufu sana wakati wa mikutano ya "The Big November Crusade" iliyokuwa ikifanyika viwanja vya Jangwani jijini Dar es salaam.

Mwimbaji huyu bwana Allen Kinsalla ambaye pia alikuwa ni mwimbaji wa kwaya ya Uinjilisti Sayuni Kinondoni Lutheran, yeye pamoja na kundi la kusifu na kuabudu ama stage band ilivyozoeleka katika mkutano huo walikuwa wakipenda sana kuimba pambio "Yale alotenda ndani yangu" na mapambio mengine ambayo yalikuwa yakiwakaribisha katika uwepo wa Mungu, mamia ya wakazi wa jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake ambao walikuwa wakifika katika mkutano huo.




Kwasasa mwimbaji huyo mwenye asili ya Congo Kinshasa anaishi nchini Marekani pamoja na familia yake kwa maana ya mkewe na watoto wawili. Mwimbaji huyu alikuwa kipenzi cha wanafunzi wa Ushirika wa kikristo wa wanafunzi Tanzania(UKWATA) mkoa wa Dar es salaam na Pwani wakati ambao kwaya ya Sayuni ilikuwa ikialikwa kila mwaka kwenye makambi ya pasaka, matamasha, joint mass pamoja na sherehe mbalimbali za wanafunzi hao wanapohitimu masomo yao(Graduation za UKWATA).

BAADA YA MUNGU KUJIDHIHIRISHA KILIMANJARO, UFUFUO WAPATA JENGO MAELFU WAHAMIA


Jengo linavyoonekana kwa nje.

Baada ya kumalizika kwa mkutano mkubwa wa injili viwanja vya mashujaa mjini Moshi mkoani Kilimanjaro, mmoja kati ya watu waliohudhuria katika mkutano huo ametoa jengo lake kubwa ili litumiwe na kanisa la Ufufuo na uzima kwaajili ya huduma mbalimbali zikiwemo ibada.

Jumatatu, 28 Oktoba 2013

unabii; TB JOSHUA ATOA TAHADHARI KWA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI,"KUNA RAIS ATATEKWA NA KUTAKUWA NA MILIPUKO YA MABOMU KWENYE CLUB HIZI"!!!

Yule Mchungaji Maarufu kutoka Nigeria Ambae hutabiri mambo mbalimbali na kweli yakatokea TB Joshua jumapili hii ametoa utabiri mpya ambao unahusisha Africa Mashariki ...ameonyeshwa rais mmoja Africa Mashariki atatekwa na ameonyeshwa watu wakiwa club wanacheza nakisha wanalipukiwa na nchi iyo ni jirani na Kenya,

Jumamosi, 26 Oktoba 2013

HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SIKU YA KUICHAMBUA BIBLIA

SOMO: HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI
L
eo, tunamaliza kutafakari SURA YA 14 ya Kitabu cha YOHANA katika Biblia zetu. Tunachukua muda wa Siku ya leo ya Kuichambua Biblia, kujifunza YOHANA 14:13-31. Katika mistari hii, pamoja na mambo mengine, tutajifunza kuhusu, “HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI“. Tutayagawa mafundisho yote tunayoyapta katika mistari hii, katika vipengele tisa:

(1) KUOMBA KWA JINA LA YESU (MST. 13-14);

(2) HAKIKA YA KUJIBIWA MAOMBI (MST. 13-14);

(3) ALAMA YA KUMPENDA YESU (MST. 15, 21, 23-24);

(4) MSAIDIZI MWINGINE (MST. 16-27, 25-26);

(5) SITAWAACHA NINYI YATIMA (MST. 18-20);

NATAKA NIPATE KUONA *sehemu ya pili*

CHANZO;GOSPLE KITAA.

Mtumishi Gasper Madumla.
Bwana Yesu asifiwe...
Nakusalimu mpendwa katika Jina kuu la uweza la Yesu Kristo,
Nikikuambia ;

Jina la BWANA lipewe sifa....

Dhima kubwa ya fundisho hili ni kupata kona kiroho.
Maana hakuna jambo lililo kubwa kama kuona kiroho. Yeye mwenye kuona kiroho ni mtu wapekee sana,maana hata maombi yake huwa ni yakipekee.

Leo tunajifunza kiundani kwa habari ya Bartimayo ambaye alifanikiwa kupata kuona. Nasi tunahitaji tupate kuona.

Nampenda sana huyu Bartmayo kipofu.
Yeye alijua jambo moja tu,;

KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI NA VITA YA HAR-MAGEDONI

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO: KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI NA VITA VYA HAR-MAGEDONI

Tuliangalia katika masomo yaliyopita kwamba, Dhiki kubwa au Dhiki kuu, itachukua kipindi cha miaka saba ( 7 ). Katika kipindi hiki pia, watakatifu walionyakuliwa wakati wa kunyakuliwa kwa kanisa, watakuwa katika kipindi cha kupewa taji na kufanyiwa karamu ya harusi ya MwanaKondoo. Ni makusudi ya somo letu la leo kujifunza tukio litakalofuata mwisho wa miaka hii saba, Kuja kwa Yesu Kristo mara ya pili duniani na Vita vya Har-Magedoni. Tutaligawa somo letu la leo katika vipengele vitano:-

( 1 ). KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI.

( 2 ). TOFAUTI YA KUJA KWA YESU WAKATI WA KUNYAKULIWA KWA KANISA NA KUJA KWA YESU MARA YA PILI DUNIANI

( 3 ). MAKUSUDI YA KUJA KWA YESU MARA YA PILI DUNIANI

( 4 ). TAIFA LA ISRAELI WAKATI WA KUJA KWA YESU MARA YA PILI DUNIANI.

( 5 ). VITA VYA HAR-MAGEDONI NA KUFUNGWA KWA SHETANI MIAKA ELFU MOJA.

( 1 ). KUJA KWA YESU MARA YA PILI DUNIANI.

Yesu Kristo, mara ya kwanza, alikuja hapa duniani katika udhaifu na unyonge kwa kuzaliwa na Mariamu na kulazwa katika Hori kulia ng’ombe. Kwa Waisraeli ambao hawakujua maandiko vema, hawakutambua kwamba Kristo Kristo ni Yesu kutokana na mazingira yake ya umaskini na unyonge ( LUKA 9:58; 2 WAKORINTHO 8:9 ). Walidhani wakati ule wa kwanza angekuja kama Mfalme na kushindwa kafahamu kwamba wakati wa kuja kama Mfalme, ilikuwa wakati wa kuja kwake MARA YA PILI duniani. Wakati wa kuja kwa Yesu mara ya pili, atakuja katika mazingira tofauti kabisa na pale mwanzoni. Atakuja na hali zifuatazo:-

MKUTANO MKUBWA WA INJILI UNAOENDELEA MJINI MOSHI. SOMO: LAANA ZA FAMILIA Na Mchungaji Kiongozi: Josephat Gwajima


Mch.Kiongozi Josephat Gwajima.
Kuna familia zinaandamwa na matatizo mbalimbali, mfano. matatizo ya kutokuolewa,umasikini au matatizo mengine yanayotokana na laana za familia. Mchungaji Kiongozi alihaidi kuvunja matatizo yote ya kifamilia yanayoletwa na familia,na kusema kuwa leo kuna mambo ambayo anataka kuusemea ukweli.
kuna familia ambazo zinakuwa zipo chini ya laana fulani na hata mtu akipenya anapenya kwa taabu sana.
Sasa tutaangalia siri iliyopo nyuma yake halafu utafunguliwa katika Jina la yesu.
Tukiangalia maandiko

Mwanzo 9:18-25..
18 Wana wa Nuhu waliotoka katika safina, ni Shemu, na Hamu, na Yafethi; na Hamu ndiye baba wa Kanaani.
19 Hawa watatu walikuwa wana wa Nuhu na kwa hao nchi yote ikaenea watu.
20 Nuhu akaanza kuwa mkulima, akapanda mizabibu;
21 akanywa divai, akalewa; akawa uchi katika hema yake.
22 Hamu, baba wa Kanaani, akauona uchi wa baba yake, akawaeleza ndugu zake wawili waliokuwa nje.
23 Shemu na Yafethi wakatwaa vazi, wakalitanda mabegani mwao wote wawili, wakaenda kinyumenyume, wakaufunika uchi wa baba yao; na nyuso zao zilielekea nyuma, wala hawakuuona uchi wa baba yao.
24 Nuhu akalevuka katika ulevi wake, akajua mwana wake mdogo alivyomtendea.
25 Akasema,Na alaaniwe Kaanani;Atakuwa mtumwa kabisa kwa ndugu zake.

SHUHUDA, MKUTANO WA INJILI MOSHI WALIOCHUKULIIWA MISUKULE WA RUDI,alikuwa makaburini Tanga,mwingine alikuwa Singida kwenyye mashamba ya mpunga.



Matendo makuu ya Mungu aliyoyafanya Arusha, imemfanya leo MIRRIUM mkazi wa Arusha kufika katika viwanja vya mashujaa mjini Moshi kushuhudia Mungu alivyo mponya.Mirium alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya moyo kuvimba, na uvimbe tumboni. Alishuhudia kuwa mara baada ya kuhudhuria mkutano huko Arusha uliokuwa katika viwanja vya relini, alipokea uponyaji wake papo hapo. Binti huyu hakuishia hapo aliamua kwenda katika hospitali ya MOI kuhakikisha muujiza Mungu aliomtendea. Huku akiwa na uso wa furaha, alishuhudia mbele ya madhabahu kuwa mara baada ya kwenda kufanya uchunguzi hospitalini madaktari walithibitisha muujiza wake maana amekuta moyo wake umepona na uko vizuri na uvimbe umetoweka kabisa.


Hakika sauti ya "njoo kwa jina la Yesu" inarudisha watu kutoka mateka,Isaya 42:22... Huyu anaitwa DORIS ana umri wa miaka 13, alichukuliwa mateka na kuwekwa uvunguni mwa kitanda. Leo binti huyu kaisikia sauti ya njoo kaifuatana nakujikuta yuko katika kundi la watu wengi.Yesu ni yuleyule jana na leo na hata milele.




Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima akihoji binti aliyepatwa na muujiza wake katika maombi, Yesu alisema Adui wa mtu ni wa nyumbani mwake, EUGENIA PHILIPO mkazi wa mjin moshi, mwenye umri wa miaka 22, alichukuliwa na mama yake mdogo na kuwekwa katika zizi la ng’ombe. Huko alikuwa akifanya kazi ya kulisha ng’ombe na kukamua maziwa, huku chakula chake kikiwa ni nyama za watu na kunywa damu.

kama vile haikutosha mama wa binti huyu pia alikuwa akimtumikisha kwa njia ya kichawi kwenda kukamua maziwa ya ng’ombe kwa watu. Aliendelea kushuhudia kuwa ng’ombe wa majirani walikuwa hawatoi maziwa kwa sababu ya kuibiwa kichawi na binti huyu. Yule mtenda miujiza ambaye alikirimiwa Jina lipitalo majina yote YESU KRISTO leo kamtoa katika utumwa wa shetani na kumuweka huru.

Alhamisi, 24 Oktoba 2013

UKOO WA MALKIA UINGEREZA WATAKIWA KUMLEA MTOTO AMJUE YESU, ANGALIA PICHA ZA UBATIZO


Askofu mkuu wa Canterbury kanisa Anglican duniani Justin Welby amewataka wazazi na wadhamini wa mtoto Prince George Alexander Louis kuhakikisha mtoto huyo anamjua Yesu ninani katika maisha yake. Askofu Welby ameyasema hayo wakati akimbatiza mtoto wa kwanza wa mjukuu wa malikia Elizabeth wa Uingereza, Prince William na mkewe Kate Middleton katika ibada fupi iliyohusisha familia pamoja na wageni wao 22 na kufanyika katika kanisa la kifalme ndani ya jengo la Mtakatifu James jijini London.

Wakati wa ibada hiyo baba mdogo wa mtoto huyo Prince Harry alisoma neno kutoka kitabu cha Yohana 15:1-5 ukizungumzia suala la mzabibu na matawi huku mama mdogo wa George, Pippa Middleton kwa upande wake alisoma neno kutoka kitabu cha Luka 18:15-17 ukizungumzia Yesu aliposema waacheni watoto wadogo waje kwangu. Katika ubatizo huo uliohudhuriwa na malkia pamoja na mumewe Prince Philip jumla ya wadhamini ama walezi wa mtoto wapatao saba walichaguliwa wakiwemo kutoka ukoo wa ufalme, marafiki wa karibu na Prince William pamoja na rafiki wa karibu sana na marehemu Princess Diana aitwaye Julia Samuel.

Askofu Welby alitumia maji ya mto Yordani katika kumbatiza prince George maji ambayo yamekuwepo katika kanisa hilo lenye historia ya ukoo wa kifalme toka mwaka 1894. Kwa mujibu wa Prince William amesema mwanae hajasumbua hata kidogo ikiwa ndio siku yake ya kwanza hadharani toka azaliwe, ambapo imeelezwa mtoto huyo kuonekana mwenye furaha na tabasamu toka awasili na kutoka kanisani hapo, huku muonekano wake ukiwa kama baba yake alivyokuwa katika umri kama huo.



Kate Middleton akiingia na mwanae.


Prince William akiwa mwenye furaha na mtoto wake Prince George mwenye miezi mitatu.


Wazazi wenye furaha na mtoto wao ambaye yupo katika mstari wa tatu katika urithi wa kiti cha ufalme Uingereza.

ONA NAMNA MALAIKA WALIVYOMUOKOA MWIMBAJI NYOTA KWENYE AJALI


Gari likiwa limepinduka bondeni.

Mwimbaji anayetamba na wimbo wa "Zawadi gani nitamtolea BWANA" ambaye pia ni mtume akichunga kanisa jijini Dar es Salaam John Komanya amepata ajali mbaya juzi mchana maeneo karibu na daraja la Mto Wami akiwa njiani kuelekea mkoani Arusha kukutana na viongozi wanaohudumu na mwalimu Christopher Mwakasege, kwa ajili ya mkutano wa injili ambao utakuwa na lengo la kuombea taifa kwa siku nne mwezi Disemba.

Kama una Mashaka na Huamini huduma ya mtumishi fulani…EPUKA KUWASEMA VIBAYA,TUMIA HEKIMA


KAMA UNA MASHAKA NA HUAMINI HUDUMA YA MTUMISHI FULANI, USIFUNGUE MDOMO KUMSEMA AU KUWASHAWISHI NA WENGINE WAWE NA CHUKI NAYE; KWA KUFANYA VILE, HATA KAMA UNACHOKISEMA NI SAHIHI, LAKINI TAYARI HAUJAKIFANYA KWA KANUNI ZA KIMUNGU, CHUKI YAKO NI SAWA NA UUAJI!
NJIA RAHISI YA KUSHUGHULIKA NA HUYO AMBAYE WEWE UNA MASHAKA NA HUDUMA YAKE AU HUAMINI KWAMBA NI MTUMISHI WA MUNGU, FANYA HAYA YAFUATAYO:

miujiza,WALIOKUWA VIWETE ZAIDI YA SABA WATEMBEA BAADA YA MAOMBEZI MKUTANO WA UFUFUO NA UZIMA - MOSHI NA Mch. Josephat Gwajima

WATU ZAIDI YA SABA AMBAO WALIKUWA NI WALEMAVU KABISA WA MIGUU, HATIMAYE WAWEZA KUTEMBEA BAADA YA KUOMBEWA NA MCH.KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA KATIKA MKUTANO MKUBWA WA INJILI UNAOENDELEA MJINI MOSHI, MATUKIO HAYA NI YA SIKU YA JUMATANO TAREHE 23.10.2013

Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima kutoka Kawe Jijini Dar es Salaam akiwaombea maelfu ya waamini katika uwanja wa Mashujaa mjini Moshi, maelfu ya wakazi wa mjini Moshi walikusanyika kwa ajili ya kusikiliza Neno la Mungu,Kuombewa na kuwekwa huru kutoka katika vifungo vya shetani.




Mchungaji kiongozi wa kanisa la Ufufuo na Uzima wa kwanza kushoto akiwa kwenye picha ya pamoja na walioponywa ulemavu wa miguu na kushoto kwake ni Petronila anafuatiwa na Mama Ruckless na wa

MOTO WA MILELE HAKUWEKEWA MWANADAMU



Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

Somo: Moto wa Milele Hakuwekewa Mwanadamu

Mpendwa msomaji, ninatanguliza shukrani zangu za dhati kwako, kwa jinsi ulivyoamua kuisoma “note” hii. Nasema tena, asante sana. Sasa basi ninakusihi uisome “note” hii hadi mwisho, ili uchote baraka zote za Mungu zilizokusudiwa kwako.

Mpendwa msomaji, najua kabisa ungependa kwenda mbinguni, mahali pema peponi, na kukaa na Mungu milele, mara tu baada ya kuiaga dunia hii. Nia yako ni njema sana. Kila mmoja wetu anapenda kwenda mbinguni, hakuna anayependa kwenda katika moto wa milele. Mimi pia, ninapenda kwenda mbinguni, sipendi kabisa kwenda motoni. Hata Mungu anapenda sisi sote twende mbinguni aliko. Kuonyesha jinsi Mungu anavyopenda twende mbinguni, muda mfupi kabla ya Yesu Kristo kupaa kwenda mbinguni, alisema katika YOHANA 14:1-3, “Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali. Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”. Mungu hapendi kabisa yeyote kati yetu aende motoni. Moto wa milele, haukutengenezwa kwa ajili yetu wanadamu, bali ni kwa ajili ya Ibilisi na malaika zake. Biblia inasema katika MATHAYO 25:41, “………..Moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake”.

Jumatano, 23 Oktoba 2013

NATAKA NIPATE KUONA *sehemu ya kwanza*


Mtumishi Gasper Madumla.
Bwana Yesu asifiwe...
Haleluya...
Karibu katika mfululizo huu wa fundisho zuri kupita maelezo.
Mfululizo huu ndio kwanza umeanza siku ya leo na una DHIMA KUU ya kukufundisha KUONA KIROHO kama vile Bwana atakavyo tuwe.

WHO IS BISHOP ZACHARY KAKOBE ( HISTORY)

Bishop Zachary Kakobe is the International Revivalist, and Founder of Bishop Zachary Kakobe International Ministries (BZKIM), a faith based non-profit organization, registered in the USA. He is also the Founder and the General Overseer of the Full Gospel Bible Fellowship Church, which is registered in Tanzania. He pastors a megachurch in Dar-Es-Salaam City, Tanzania; which is the mother Church; and from there, he oversees more than 400 branch churches (daughter churches), which he planted scatteredly across all the regions and districts of Tanzania mainland.

Bishop Zachary Kakobe is a Tanzanian national; born on Monday, June 6, 1955; in Kibondo, Tanzania. His spiritual journey began on Easter Sunday, April 6, 1980; when he was born again at a Miracle Healing Indoor Crusade, which was conducted by a renowned National Evangelist in Tanzania, Bishop Moses Kulola, at the Tanzania Assemblies of God Church, Ilala, Dar-Es-Salaam, pastored by Pastor Titus Mukama. In that evening, the Gospel message that was preached by Bishop Moses Kulola, made Zachary Kakobe to go forward to the pulpit, for salvation. He went forward to the pulpit, weeping bitterly in public, and repented his sins; with a real intention from the depths of his heart, to turn away from all sins, and deceitful pleasures; and accepted Jesus in his heart to be his personal Lord and Saviour. From that day on, his life was completely transformed. His wife and his friends who knew him before, testified that his life was changed. He was born again. He was a new creature, in Christ. Shortly after, he made Tanzania Assemblies of God church, Temeke, Dar-Es-Salaam; his local church home. For a number of years after his conversion, he was a faithful member of this church, and his Pastor was the late Callist Masalu, who was a renowned Servant of God in Tanzania, for more than four decades.

JOYOUS YATANGAZA TAREHE YA KUREKODI DVD MPYA, MASHABIKI WALUMBANA


Mwanadada Sphumelele Mbambo au mwite Ntokozo kwa jina lingine, akiwajibika jukwaani.
Hatimaye kundi mahiri la gospel barani Afrika la Joyous Celebration limetangaza rasmi tarehe na ukumbi ambao wanatarajia kurekodi album yao mpya ya 18 mwishoni mwa mwaka huu. Kupitia ukurasa wao wa Facebook kundi hilo limesema litarekodi album yao tarehe 21 December katika ukumbi wa ICC Durban na kuahidi kutoa taarifa zaidi juu ya tukio hilo.

ALIYEKUWA FREEMASON KWA MIAKA 14 AOKOKA MOSHI, AONYESHA KIDOLE ALICHOKATWA


Aliyekuwa Freemason kwa miaka 14 afunguliwa katika mkutano wa Ufufuo na Uzima unaoendelea Moshi; alikatwa kidole akiwa mdogo kama udhihirisho wa alama yao (devil horns)
alieleza mwenyewe mbele ya waliokuwepo mkutanoni maelfu ya watu wa mkoa wa Kilimanjaro na vitongoji vyake wanaohudhuria mkutano huo katika viwanja vya mashujaa unaoongozwa na mchungaji Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima lenye makao makuu yake Kawe jijini Dar es salaam.



Binti wa kiislamu ambaye aliwekwa ndani ya bahari kwa miaka mingi; alipokea ukombozi wake mara baada ya maombezi. Kule baharini alikuwa ameolewa na jini ambaye alimweka awe malkia wa baharini kwa miaka mingi... Mungu akamrudisha baada ya maombezi na kumpokea Yesu Kristo.
Baadhi ya picha jinsi maelfu ya wakazi wa mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro wanavyohudhuria mkutano huo toka ulipoanza tarehe 20 mwezi huu, unatarajiwa kumalizika siku ya jumapili tarehe 27.

JE,WAJUA; Si Mke mwema tu, hata mchumba bora hupatikana kwa Bwana!!?



Habari SG,
Jamani kuna shuhuda nyingine si tu zinasisimua/leta raha rohoni mara tu uzisikiapo lakini pia zinakua challenge/ somo kabisa la kutendea kazi na ku-share mara moja ili kusaidia/kubariki na wengine. Pia zinafanya hata mtu unashangaa na kupenda jinsi gani Wapendwa wanapoamua kutembea na Mungu na kumtumikia inavyopelekea Bwana naye kufurahi kua na mambo yao toka hatua za mwanzo kabisa.
Kila mmoja wetu anajua kua Bible inaongea sana jinsi ya kupata Mke kuliko Mume na maandiko maarufu ni kama-‘’Mithali18:22-‘’Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana’’ na Mithali.31:10-’’Mke mwema( Kiswahili imetumia neno moja tu .’’Mwema’’ lakini Kiingerea ktk Bible mbalimbali imetumia maneno mengi yenye nguvu ya ajabu na kushangaza kujua kumbe Mwanamke

Jumatatu, 21 Oktoba 2013

MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : http://www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO: MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

Kama vile kunavyokuwako na mwisho wa dakika, saa, siku, wiki, mwezi, mwaka, karne, milenia au “millennium”, ndivyo kutakavyokuwako pia na “mwisho wa dunia” na “siku za mwisho”. Chenye mwanzo, hakikosi kuwa na mwisho. Biblia inaeleza juu ya siku za mwisho (1 TIMOTHEO 4:1), mwisho wa dunia(MATHAYO 24:3), n.k. Sasa basi, maandiko matakatifu yanatuonyesha kwamba tunapaswa kujiangalia, ili siku ya mwisho isitujie ghafla; kama mtego unasavyo ( LUKA 21:34-35 ). Ndiyo maana leo, tunajifunza somo,”MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU”. Tutajifunza somo hili, kwa kulitafakari katika vipengele vine:-

( 1 ). MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

( 2 ). KUNYAKULIWA KWA WATAKATIFU

( 3 ). DHIKI KUBWA AMBAYO HAIJAWAHI KUTOKEA TANGU KUUMBWA KWA ULIMWENGU


( 4 ). JINSI YA KUFANYA ILI KUNYAKULIWA

( 1 ). MWAKA 2000 KATIKA KALENDA YA MUNGU

MCHAWI AJISALIMISHA KANISANI TAG MAGOMENI


Mchungaji Kanemba akiangalia vifaa vya kishirikina vya kijana huyo.
Haya ndio yaliyotokea Jumapili katika Kanisa la TAG Magomeni Mikumi kituoni jijini Dar es salaam. Katika mwendelezo wa ushuhudiaji wa shabaha ambapo kijana aliyekuwa akitumikishwa na shetani katika mambo ya kichawi kuamua kuokoka na kukabidhi sanduku lake lenye vifaa vya kichawi ili vichomwe moto.

Kijana huyu ambaye ni dereva wa bodaboda na ni mkazi wa Magomeni Mapipa aliamua kwa hiari yake kuokoka wakati wa ibada kuu ya jumapili kanisani hapo alipokwenda kuabudu ambapo baada ya ibada alikwenda kwa mazungumzo ofisini kwa Mchungaji Kanemba akiwa yeye na mama yake ambako aliomba alete vitu vyake vya kichawi ili vichomwe moto jambo ambalo lilitekelezwa.

Tukio hilo lilipelekea kilio kikuu kwa mama yake mzazi maana hakuwa akijua kuwa mwanaye huyo alikuwa anajishughulisha na mambo ya kichawi, kijana alieleza matumizi ya vifaa hivyo vya kichawi; ikiwemo na mvuto ki-biashara, mvuto wa ki-mapenzi na hata kuwadhulu wabaya wake jambo ambalo liliwaacha watu waliokuwa wakishuhudia tukio hilo kwa mshangao na wengine wakimtukuza Mungu.

MOYO WA NCHI ,UFAHAMU MOYO WA ULIMWENGU WA ROHO



Mchungaji(Resident Pastor) Adriano akifundisha mapema leo ibadani
Na Mch. Adriano Makazi

Yona 2:1-10
Ninawi ulikua ni mji ambao watu wake walikua wamemuacha Bwana, na Mungu alikua amemtuma Yona ninawi na alimpa ujumbe kwaajili ya watu wa Ninawi, lakini Yona akaghairi na kwenda Tarshishi ambako Bwana hakumtuma.

Na alipokua akielekea ambako hajatumwa na Bwana ikatokea dhoruba, kura ilipopigwa ikaangukia kwa Yona, walipomhoji wamtendee nini Yona akasema wamtupe baharini. Alipotupwa baharini Bwana akaandaa samaki ili ammeze.

Nivizuri kujua samaki huyu hakua samaki wa kawaida, kwasababu angekua samaki wa kawaida Yona asingekaa ndani ya tumbo la samaki kwa siku tatu.


Baada ya siku tatu Bwana akasema na samaki na samaki yule akamtapika pwani ya Ninawi ili kwenda kuifanya kazi aliyokuwa akiikimbia.

Mathayo 12:40 Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa muda wa siku tatu mchana na usiku, vivyo hivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku tatu, mchana na usiku

GLORIOUS YABARIKI WATU MWANZA, WAMTEMBELEA MJANE WA ASKOFU KULOLA


Baadhi ya waimbaji wa GWT wakiwa mbele ya kaburi la marehemu Askofu Dkt. Moses Kulola, E.A.G.T Bugando jijini Mwanza.
Kundi la Glorious Worship Team(GWT) lenye makao makuu yake jijini Dar es salaam limeendelea na ziara yao ya kihuduma jijini Mwanza wakiambatana na mlezi wao bwana Eric Shigongo mkurugenzi wa Global Publisher, ambapo hapo jana waliweza kuwabariki watu waliofika katika ibada ya kusifu na kuabuduiliyofanyika ukumbi wa JB Belmont hotel kwa jinsi walivyoweza kushusha uwepo wa Mungu katika sifa na kuabudu.

KWAYA ZA AIC SHINYANGA ZATIKISA UWANJA WA CCM KAMBARAGE MAADHIMISHO MIAKA 20 YA DAYOSISI YAO


Mercy Nyagwaswa kutoka AIC Dar es salaam Choir akishambulia jukwaa hapo jana.
Kwaya na waimbaji binafsi kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga wamependezesha maadhimisho ya miaka 20 tangu kuanzishwa kwa dayosisi ya mkoa huo kwa kanisa la African Inland (AIC)Tanzania mwaka 1993, tamasha hilo lililoanza siku ya ijumaa lilihitimika hapo jana katika uwanja wa CCM Kambarage mkoni humo.

Jumla ya kwaya 13 zimeshiriki toka siku ya ijumaa, ikiwemo kwaya ya AIC Shinyanga wana wa kung'ang'ania, AIC Kambarage kwaya wana wa Piga kelele, mwanadada Mercy Nyagwaswa kutoka AIC Dar es salaam kwaya ambaye amealikwa kama mwimbaji binafsi, AIC Mwadui na kwaya nyinginezo.

Maadhimisho hayo yanatarajiwa kuendelea wiki nzima hii kwa mkutano mkubwa wa injili utakaohubiriwa na maaskofu wa kanisa hilo nchini na nchi jirani ya Kenya pamoja na maaskofu kutoka jumuiya ya Kikristo nchini (CCT) wakiongozwa na mwenyekiti wake askofu mkuu wa Kanisa la Kilutheri nchini Dkt. Alex Gehaz Malasusa.

Ambapo kilele cha maadhimisho hayo kinatarajiwa kuwa siku ya jumapili, kwa kuanza kwa maandamano kuelekea uwanja wa Kambarage sambamba na shughuli ya uchangiaji wa pesa kwa ajili ya kuchangia shule ya dayosisi hiyo Bishop Nkola school yatakayoongozwa na waziri mkuu mstaafu ambaye pia ni mbunge wa Monduli mheshimiwa Edward Lowasa pamoja na mhamasishaji akiwa ni mchungaji matarajiwa bwana Masanja Mkandamizaji, huku kwaya maarufu ya AIC Chang'ombe Vijana (CVC) wanatarajiwa kunogesha zaidi maadhimisho hayo.



Askofu wa Dayosisi ya Pwani Askofu Salala pamoja na mwenyeji wake Askofu Dr Nkola wakiendelea kufuatilia hitimisho la tamasha la uimbaji.


Waimbaji mahiri wa AIC Shinyanga Choir wana wa kung'ang'ania wakisukuma sauti.


AIC Shinyinga Choir.

JE, NIKWELI YESU ALIBADILI MAJI KUWA POMBE?

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SIKU YA KUICHAMBUA BIBLIA

SOMO: YESU ALIBADILI MAJI KUWA POMBE?

L


eo, tunaendelea tena kujifunza Kitabu cha YOHANA katika Biblia zetu. Leo, tunajifunza YOHANA 2:1-11. Kuna mengi ya kujifunza katika mistari hii ingawa kichwa cha somo letu ni “YESU ALIBADILI MAJI KUWA POMBE? Tutayagawa mafundisho tunayoyapata katika mistari hii katika vipengele vinane:-

(1)RIPOTI YA UTENDAJI WA KAZI YA MUNGU KILA SIKU (Mst. 1);

(2)KUALIKWA YESU ARUSINI (Mst. 2);

(3)KUTINDIKA KWA DIVAI (Mst. 3);

(4)WAJIBU WA KUKUBALI KUKEMEWA (Mst. 4);

(5)SAA YA MIUJIZA (Mst. 4);

(6)LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI (Mst. 5-9);

(7)KUITENDA KAZI YA MUNGU BILA UKUU (Mst. 8-9);

(8)YESU ALIBADILI MAJI KUWA POMBE? (Mst. 9-11).



(1) RIPOTI YA UTENDAJI WA KAZI YA MUNGU KILA SIKU (Mst. 1)

Hapa tunajifunza utendaji wa kazi ya Mungu aliokuwa anaufanya Yesu. Kulikuwa na ripoti yake ya utendakazi KILA SIKU! “Na siku ya tatu palikuwa (Mst. 1), pamoja na “Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate“ (YOHANA 1:43); ni maneno yanayotufundisha kutoa ripoti ya utendaji wetu kila siku. Ni muhimu kila mmoja wetu kujiulizaKILA SIKU, “Je leo nimefanya nini katika utendaji wa kazi ya Mungu? Nimefanya nini leo kwa ajili ya Ufalme wa Mungu?“ Ikiwa majibu yetu ni kwamba hatukufanya lolote ila tumefanya mambo ya dunia hii tu yanayopita, au tumefanya mambo ya kujibariki tu na siyo kuwabariki wengine kiroho; tujue kwamba hatuishi kwa kufuata mfano wa Bwana wetu Yesu Kristo. Yesu hakuwa na siku hata moja ya kupoteza! Kila siku ilikuwa ni siku ya kumtendea kazi Mungu. Sisi nasi, ni wajibu wetu kuukomboa wakati. Hatuna muda mrefu wa kuishi. Tukipoteza siku moja na tukaiacha ipite bila kumtendea Mungu kazi, siku hiyo hairudi tena, tumepoteza kitu cha thamani kubwa (WAEFESO 5:15-16; WAKOLOSAI 4:5). Ripoti za watendakazi wengi zinasomeka “SIKUFANYA LOLOTE“ siku ya Jumatatu, Jumatano, Jumapili na siku nyinginezo, kwa visingizio mbalimbali. Huku siyo kumfuata Kristo Yesu!

Jumapili, 20 Oktoba 2013

HALELUYA, ASKOFU KAKOBE ANAWASHA MOTO WA INJILI KONGO


Askofu Kakobe akiwaombea wachungaji katika semina mjini Lubumbashi jana.
Baada ya mkutano mkubwa wenye mafanikio alioufanya jijini Toronto nchini Canada mapema mwezi wa sita mwaka huu, Askofu Zachary Kakobe amerejea tena mjini Lubumbashi nchini Kongo ambako anafanya mkutano mkubwa wa injili uliopewa jina la "Great Miracle Healing Crusade" ambao umeanza jana ijumaa tarehe 18/10/2013 na utamalizika hapo kesho siku ya jumapili.

Kabla ya kuanza mkutano huo ambao umekusanya maelfu ya wakazi wa jiji la Lubumbashi, askofu Kakobe alianza na semina maalumu kwa wachungaji wa makanisa mbalimbali ya kiroho nchini humo iliyofanyika kwa siku mbili Alhamis na jana ijumaa ambapo pia alipata kuwaombea ujazo wa Roho Mtakatifu wachungaji hao ambao kwa mujibu wa taarifa kutoka huduma ya askofu Kakobe wachungaji hao wameshukuru kwakujazwa nguvu mpya katika kuitenda kazi ya Mungu katika makanisa yao.

VIPINDI SABA VYA MAONGOZI YA MUNGU

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO: VIPINDI SABA VYA MAONGOZI YA MUNGU

Leo tunajifunza somo muhimu sana kwa kila mtu anayependa kuyafahamu mapenzi ya Mungu na kuyafanya. Tutaligawa somo letu katika vipengele vitano:-

( 1 ). MUNGU KAMA MFANYA SHERIA

( 2 ) UMUHIMU WA KUTAMBUA MAJIRA AU KUJUA NYAKATI

( 3 ) VIPINDI SABA VYA MAONGOZI YA MUNGU

( 4 ) TOFAUTI YA MAONGOZI KATIKA VIPINDI HIVI SABA

( 5 ) YATUPASAYO KUFANYA KATIKA MAJIRA TULIYONAYO

( 1 ). MUNGU KAMA MFANYA SHERIA.

Mungu wetu ndiye mfanya sheria wetu na mwamuzi wetu (ISAYA 33:22). Kwasababu yeye ndiye mfanya sheria, ana haki kuweka sheria fulani au kuiondoa na kuweka nyingine. Hatupaswi kushindana naye wala kumuuliza kwa nini anaiondoa sheria hii na kuiweka nyingine. Uamzi wake ni wa mwisho. Yeye ndiye mwamzi wetu. Ole wake ashindanaye naye ( ISAYA 45;9 ; WARUMI 9:19-20). Kazi yetu wanadamu , ni kuitekeleza sheria ile anayotupa.

( 2 ). UMUHIMU WA KUTAMBUA MAJIRA AU KUJUA NYAKATI

Sheria anazotupa Mungu wetu hubadilika kulingana na wakati kama apendavyo yeye. Kazi yetu wanadamu kama watekelezaji wa sheria ni kujua nyakati tulizonazo na mambo yapi tunayopaswa kuyatenda katika nyakati tulizonazo ( 1NYAKATI 12:32 ). Serikali ya Tanzania siku za nyuma iliweka sheria kwamba ni mabasi ya UDA tu yanayotakiwa kutoa huduma za usafiri Dar es salaam. Kwa wakati ule, ilikuwa ni kosa kwa gari lolote kufanya huduma hizo. Sheria hii baadaye ilibadilishwa na kile kilichokuwa si halali kwa wakati ule, sasa ni halali. Hatupaswi kushikiria tu sheria ile ya mwanzo wakati tayari imebadilishwa. Ni kazi ya raia wa Tanzania kujua wakati au majira na kujua ni sheria ipi inayohusiana na wakati wa sasa. Sura za noti zetu pia hubadiilishwa kulingana na wakati. Noti ya sh: 100/= ya mwaka 1966, ilikuwa ina thamani wakati ule lakini sasa mtu aliyenayo, ni kama ameshikilia karatasi tu! Vivyo hivyo wanadamu, tunapaswa kuyatambua majira ya Mungu na sheria zinazotenda kazi katika kila majira. Hatupaswo kuzidiwa maarifa na koikoi, mbayuwayu au korongo ambao ni ndege tu wa angani (YEREMIA 8:7; LUKA 12:54-56).

( 3 ). VIPINDI SABA VYA MAONGOZI YA MUNGU.

Mungu wetu, mfanya sheria weti ameweka vipindi saba katika maongozi yake, na kila kipindi kina sheria zake zinazotenda kazi. Vipindi hivi saba, ni hivi vifuatavyo:-

1.Siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika ( MATHAYO 24:38 )

Kuanzia Uumbaji wa mbingu na Nchi na vyote viijazavyo pamoja na Adamu na Hawa mpaka wakati wa Gharika kuu wakati wa Nuhu.

2. Siku za Wazee wetu au siku za Mababa ( MATENDO 7:8-9; YOHANA 7:22; WAEBRANIA 7:4 ).

Kuanzia baada ya Gharika mpaka siku ile wana wa Israeli walipotoka Misri.

3. Siku za Torati na Manabii au Sheria ya Musa ( MATHAYO 22:40; WAEBRANIA 10:28; MATENDO 28:23 )..

Kuanzia siku ile wana wa Israeli walipotoka Misri mpaka siku ile Yesu Kristo alipokuja duniani mara ya kwanza kwa kuzaliwa na Mariamu.

4. Majira ya Mataifa au Majira ya Neema au Majira ya Kanisa ( LUKA 21:24; MATENDO 14:26-27; WARUMI 6:14 ).

Kuanzia siku ile Yesu alipozaliwa duniani mpaka siku atakapokuja kulinyakua Kanisa .

MAJESHI YA BWANA KAZINI, MOSHI KAENI CHONJO


Mkutano wa injili ambao umeandaliwa na kanisa la Utukufu wa Kristo (Glory of Christ) maarufu kwa jina la Ufufuo na Uzima, hatimaye utaendelea jijini Moshi baada ya miujiza kufanyika Arusha, ambapo maelfu kwa maelfu wameokoka na kufunguliwa kutoka vifungo vya kila aina.


Mkutano huo ambao umepelekea kuanzishwa kwa tawi la kanisa hilo Arusha eneo la Engo Sheraton, unatarajia kupelekea maajabu ya nguvu za Mungu kwenye kila mkoa watakapopita, na pindi wakimaliza Moshi tarehe 20 - 27 Oktoba, wataelekea Tanga, mahali ambapo kwa hakika inatarajiwa kuwa mapinduzi makubwa yatafanyika.


Zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo Gospel Kitaa imezipiga katikati ya wiki kwenye viwanja vya kanisa hilo, shuhudia mwenyewe kilichojiri, ambapo watu hufundishwa kuhusu Neno la Mungu, na kidogo kidogo, utaona wameshaanza pia kuwa jeshi kamili - haoa jeshi liko kazini, linapiga kwelikweli.







IMENIPASA KUWAMO KATIKA NYUMBA YA BABA YANGU

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe
MASOMO YA MAKANISA YA NYUMBANI

SOMO LA 10: IMENIPASA KUWAMO KATIKA NYUMBA YA BABA YANGU

NENO LA MSINGI:

LUKA 2:49:

“Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa IMENIPASA KUWAMO KATIKA NYUMBA YA BABA YANGU?”

I
shara mojawapo kubwa itakayoonekana kwa mtu aliyezaliwa mara ya pili na kufanyika mtoto wa Mungu, ni shauku ya kuzijua njia za Mungu, kufurahi kumkaribia Mungu na kumtafuta Mungu kila siku.

ISAYA 58:2:

“Walakini wanitafuta kila siku; hupenda kujua njia zangu; kama vile taifa waliotenda haki; wasioacha sheria ya Mungu wao, hutaka kwangu amri za haki; hufurahi kumkaribia Mungu.”

Mtoto wa Mungu atapenda kujisomea Biblia, na kufanya maombi kila mara anapopata nafasi nyumbani mwake. Maisha yetu ya kiroho nyumbani, ni lazima yaambatane na kujisomea Biblia na kuyatafakari yaliyomo, pamoja na kufanya maombi mara kwa mara. Hata hivyo, haitoshi tu kujisomea Biblia na kufanya maombi nyumbani na kudhani kwamba hakuna umuhimu wowote wa kwenda Kanisani. Kwenda Kanisani, ni agizo la Mungu kwa kila mtu aliyeokoka. Ni lazima tukutane pamoja na wenzetu katika kusanyiko mahali alipopachagua Mungu. NI AMRI YA MUNGU kwa kila mtu aliyeokoka kwenda Kanisani na kukusanyika pamoja na wenzake. ANGALIA MAANDIKO:

KUMBUKUMBU LA TORATI 12:5

“Lakini mahali atakapopachagua BWANA, Mungu wenu,………………..apaweke jina lake, maana ni makao yake, ELEKEZENI NYUSO ZENU HAPO, NAWE WENDE HUKO.” Maneno haya “Nawe wende huko”, katika Biblia ya Kiingereza ya tafsiri inayoitwa “New International Version”, yanasomeka “TO THAT PLACE YOU MUST GO.” Tungeweza kutafsiri “MAHALI HAPO, NI LAZIMA UENDE.”

Unaona! Mungu anasema ni lazima twende Kanisani, katika Nyumba ya Bwana. Angalia zaidi Maandiko:

WAEBRANIA 10:25

“Wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine……. na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.”

Yesu Kristo mwenyewe alionyesha wazi jinsi ilivyo lazima kwa kila mkristo kuwamo nyumbani mwa BWANA au Kanisani. Yusufu na Mariamu walipomtafuta kwa huzuni Yesu Kristo baada ya kumkosa kwa siku tatu, walipomwona; Yesu aliwaambia:

LUKA 2:49:

“Akawaambia, kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa IMENIPASA (ni lazima kwangu) KUWAMO KATIKA NYUMBA YA BABA YANGU?”

Ikiwa Yesu Kristo kwake ilikuwa ni lazima kwenda Kanisani, basi ni zaidi sana kwa kila mtu anayesema Yesu Kristo anakaa ndani yake. Biblia inasema kwamba yeyote anayesema Yesu Kristo anakaa ndani yake, imempasa kuenenda VILEVILE kama Yeye (Yesu) alivyoenenda alipokuwa duniani [1 YOHANA 2:6]. Ikiwa wewe umeokolewa na ni mkristo unayefuata chapa zake Yesu, basi kwako itakuwa niLAZIMA kwenda Kanisani na utafurahia kufanya hivyo. Daudi alifurahi mno alipoambiwa aende nyumbani mwa BWANA au Kanisani [SOMA ZABURI 122:1].

Ukitaka kufanikiwa kama Daudi, inakubidi uwe na furaha kumkaribia Mungu kwa kwenda Kanisani. Watakatifu wa zamani walikuwa na shauku ya ajabu ya kwenda Kanisani na waliona Nyumba ya BWANA ikipendeza mno kwao. Kwao siku moja Kanisani ilikuwa ni bora kuliko sikuelfu (zaidi kidogo ya miaka mitatu) katika shughuli za dunia au hema za uovu [SOMA ZABURI 84:1-2, 10].

Mtu anaonyesha jinsi ambavyo amekomaa kiroho kwa jinsi ambavyo ana shauku kubwa ya kwenda Kanisani. Ikiwa mtu anajiona kuwa ni Nabii na hana haja ya kwenda Kanisani, huyo ni nabii wa uongo. Nabii wa kweli Ana binti Fanueli, kila siku alikuwa Kanisani [SOMA LUKA 2:36-37].

Ikiwa mtu anajiona amekua sana kiroho, na kufikia kiwango cha mitume kumi na wawili wa Yesu; na kujiona kuwa hana haja ya kwenda Kanisani, basi huyo ni mtume wa uongo. Mitume wa Yesu kila siku walikuwa Kanisani [SOMA LUKA 24:53]. Ikiwa mtu anajiona kuwa ana karama zilizo kuu kama Petro na Yohana, na kuona kuwa hana haja ya kwenda Kanisani; mtu huyu hawajui Petro na Yohana. Watu hao walikuwa wanakwenda Kanisani na walitunza mno hata muda uliopangwa wa kukusanyika Kanisani. [SOMA MATENDO 3:1].

Mtume Paulo naye alijua mno ulazima wa kwenda kusali Kanisani na alimwona Yesu kwa njia ya kipekee akiwa yuko Kanisani akisali [SOMA MATENDO 22:17].

Watu waliookoka katika Kanisa la Kwanza walijua mno ulazima wa kuwa Kanisani kila siku.

MATENDO 2:46

“Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu ………………”.

Haikuwa Jumapili tu, kama watu wengine wanavyofanya leo. Haikuwa tu siku fulani ya sikukuu! SIKU ZOTE! Mtu aliyeokolewa, anaonyesha tofauti iliyopo kati yake na wasiomcha Mungu kwa jinsi ambavyo anakwenda Kanisani zaidi ya siku moja kwa wiki. Wako wakristo wa jina (ambao hawajaokolewa) wanaokwenda kila Jumapili kanisani. Ni lazima kuwepo tofauti. Kila siku ya ibada Kanisani inatubidi kwenda ili kukusanyika pamoja na wenzetu. Ni lazima kujihadhari na masumbufu ya dunia (hema ya uovu) ambayo yanatufanya twende Kanisani mara moja kwa wiki au mara moja kwa mwezi. Ni lazima tuombe kufunguliwa katika hali hiyo ili kila mmoja ahudhurie siku zote za Ibada Kanisani.

SABABU SITA ZA ULAZIMA WA KUKUSANYIKA PAMOJA KANISANI

1. MUNGU KAMA BABA YETU, HUSEMA NASI KIPEKEE TUNAPOKUSANYIKA PAMOJA KAMAWATOTO WAKE

Baba anaweza kusema na mtoto mmoja mmoja juu ya mambo kadha. Hata hivyo, mambo ya undani mno yanayohusu watoto wake, Baba hupenda kuyazungumza baada ya kuwakusanya kwanza watoto wake ili wasikie wote. Angalia mfano huu katika Biblia:

MWANZO 49:1-2:

“Yakobo akawaita wanawe, akasema, KUSANYIKENI, ili niwaambie yatakayowapata siku za mwisho. Kusanyikeni msikie, enyi wana wa Yakobo. Msikilizeni Israeli, BABA YENU.”

Watu tuliookoka, ni wana wa Israeli wa kizazi hiki. Baba yetu aliye mbinguni hupenda tukusanyike wote pamoja, ili azungumze nasi kipekee. Wakati wote hupenda tukusanywe kwanza ili atueleze mambo muhimu tunayopaswa kuyafahamu. Angalia anavyosema katika:

ZABURI 50:5:

“Nikusanyieni wacha Mungu wangu waliofanya agano nami kwa dhabihu.”

Mungu husema nasi mmoja mmoja tunaposoma Neno lake na kuomba, kila mtu akiwa nyumbani kwake. Hata hivyo, tunapokusanyika pamoja, Mungu husema nasi kwa namna ya kipekee.

1. MUNGU HUJITUKUZA KIPEKEE KATIKA KUSANYIKO

Watoto wake Mungu wanapokusanyika pamoja kwa jina lake, yaani kutokana na agizo lake; na kumsifu Mungu na kumwabudu Kanisani, Mungu hujitukuza kipekee kati yao. Utukufu wa kipekee wa Mungu hudhihirishwa, kusanyiko la watu wa Mungu linapojihudhurisha mbele za Mungu. Angalia mifano katika:[1WAFALME 8:10-11; 2 NYAKATI 5:13; KUMBUKUMBU LA TORATI 4:10-12].

2. MUNGU HUTUFUNDISHA KIPEKEE KANISANI

Yesu Kristo alikuwa akifundisha katika hekalu au Kanisani kila siku [YOHANA 8:2; MARKO 14:49]. Mafundisho ya Yesu hekaluni yalikuwa yamejaa mafunuo ya kipekee katika Neno la Mungu. Baada ya Yesu kuondoka kwetu, Roho Mtakatifu ameweka WENGINE (sio sote) kuwa WAALIMU ili kuwakamilisha watakatifu [WAEFESO 4:11-15; 1 WAKORINTHO 12:28-29]. Yesu alituonyesha mfano wa kwenda Kanisani na kuwasikiliza waalimu wakilitafsiri Neno la Mungu na kutufundisha, na kisha kuwauliza maswali:

LUKA 2:46:

“Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.”

Sisi nasi inatupasa kumfuata Yesu kielelezo chetu. Pamoja na kujifunza nyumbani kwetu, inatubidi tukusanyike pamoja Kanisani ili tuwasikilize waalimu waliowekwa na Roho Mtakatifu na kuwauliza maswali.

3. MUNGU HUZIFUNUA DHAMBI TUNAZOZITENDA BILA KUJUA,TUNAPOKUWA NYUMBANI MWAKE

Dhambi ni nini?

(a) Dhambi ni kufanya yasiyotupasa kuyafanya;

(b) Dhambi ni kutokufanya yanayotupasa kuyafanya.

Pasipo kufahamu na tena bila kukusudia, unaweza ukatenda dhambi bila kujua kuwa ni dhambi. Mbele za Mungu ukifanya dhambi pasipo kujua kuwa ni dhambi bado unakuwa na hatia:

MAMBO YA WALAWI 5:17:

“Na kama mtu akifanya dhambi, na kutenda mambo hayo mojawapo ambayo BWANA alizuilia yasifanywe, AJAPOKUWA HAKUYAJUA, ni mwenye hatia vivyo, naye atachukua uovu wake.”

Kwa sababu hiyo, Mungu mwenyewe anatushauri kwamba tutunze miguu yetu na kuitumia vema kutupeleka nyumbani kwa Mungu (Kanisani); ili tusikie yale yanayotupasa kuyafanya, na pia yale yasiyotupasa kuyafanya; ili tusijikute tunafanya kama wafanyavyo wapumbavu.

MHUBIRI 5:1:

“Jitunzeni mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; maana ni heri kukaribia ili usikie, kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; ambao hawajui kuwa wafanya mabaya.”

Kwa kuwa Mungu anatupenda, hutufunulia waziwazi dhambi hizo tunapokuwa tunamsikiliza Mtumishi wake Kanisani na kutuepusha na hatia. Unapokuwa peke yako tu nyumbani, ni rahisi kuyashikilia tu yale uliyoyazoea na kuona siyo dhambi, na hata Mungu akisema nawe kwa Roho wake, mara nyingi huwezi kuchukua hatua. Inahitaji njia ya wazi zaidi. Mungu hufanya hivyo Kanisani na kutufunulia yote kwa njia ya wazi kwa kuwatumia watumishi wake.

4. MUNGU HUTUPA MAJIBU YA MASWALI YETU NA KUYAFUMBUA MATATIZO YETU KANISANI

Unapokuwa unalitafakari Neno la Mungu mwenyewe nyumbani, unaweza ukabaki na mafumbo mengi. Mungu anafahamu hali hiyo. Unaweza pia ukawa na matatizo katika kuyafahamu mapenzi yake katika jambo fulani linalokuhusu. Mungu anafahamu hali hiyo. Unapokwenda Kanisani, Mungu hutafuta njia ya kukupa ufumbuzi wa tatizo lako katika ujumbe wa Neno la Mungu au kwa njia nyingi nyinginezo Kanisani, iwe ni ushuhuda wa mtu mwingine, uimbaji n.k.

ZABURI 73:16-17:

“Nami nalifikiri jinsi ya kufahamu hayo; ikawa taabu machoni pangu; hata nilipoingia katika patakatifu pa Mungu nitautafakari mwisho wao.”

5. KARAMA MBALIMBALI ZA ROHO HUTUMIKA KANISANI KWA KUJENGANA:

Katikati ya watoto wa Mungu, pana tofauti za karama, tofauti za huduma na tofauti za kutenda kazi. Tunapokutanika pamoja, inakuwa ni rahisi mmoja kumjenga mwenzie kadri ya alivyopewa na Roho kwa neema. [1 WAKORINTHO 12:4-7; 1 WAKORINTHO 14:26].

AINA MBILI ZA MAKUSANYIKO KATIKA BIBLIA:

(a) Kanisa la Nyumbani:

[MATENDO 12:12; WAKOLOSAI 4:15; 1 WAKORINTHO 16:19]

- Makusanyiko ya watu wachache katika nyumba za waaminio kwa lengo la kuwa

karibu zaidi, kufahamiana kindugu na kusaidiana kiroho na kimwili; huku tukidumu katika Neno la Mungu na kuomba.

(b) Kanisa Kuu:

[MATENDO 2:42, 46-47; MATENDO 15:4; MATENDO 14:27; 1 WAKORINTHO 1:2; 1 WATHESALONIKE 1:1:]

Kusanyiko kuu linalojumuisha waaminio wote katika siku ya BWANA Jumapili na siku nyinginezo zilizopangwa.

Ni muhimu kwa kila mmoja kuhakikisha anahudhuria katika Kanisa la Nyumbani, na Kanisa Kuu bila kukosa; kama ilivyokuwa desturi ya watakatifu wengine katika Kanisa la Kwanza. Huku ndiko kufurahi kumkaribia Mungu na kumtafuta KILA SIKU.

UCHAGUZI WA KANISA KUU

Tunapaswa mno kuwa waangalifu katika kuchagua Kanisa ambapo tutatambulika kwamba ni Washirika, na kuhudhuria hapo katika ibada za Jumapili na siku nyinginezo za wiki. Uchaguzi wetu ukiwa mbaya unaweza kabisa ukatugharimu kukosa uzima wa milele. Jambo hili linaweza likakushitua sana! Lakini ebu jaribu kuwaza pamoja nami. Je! mtoto mchanga anayenyonya akiwekwa juu ya matiti ya mama aliyekufa kwamba anyonye, mtoto huyo ataendelea kuishi? Jibu ni hapana: Mtoto huyo naye lazima atakufa. Biblia inasema kumcha BWANA ni MWANZO wa hekima [MITHALI 9:10]. Unapokata shauri kuokolewa, unakuwa ndiyo mwanzo wa kuwa na hekima. Hata hivyo inakupasa kuelimishwa ili uzidi kuwa na hekima, au siyo giza zito litakufunika [SOMA MITHALI 9:9]. Kwa hiyo jambo la kufanya ni kutafuta Kanisa ambalo limejaa hekima ya Mungu. Ukikaa hapo, na wewe utakuwa na hekima ya kukuwezesha kuingia mbinguni.

MITHALI 13:20a:

“Enenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima.”

Kanisa vuguvugu, litamfanya yeyote anayeingia pale awe vuguvugu na mwishowe atapikwe siku ya mwisho. Kanisa lililo mbali na kweli yote ya Mungu, litawafanya wale wote waingiao hapo waongozwe mbali na kweli na kuangamia. [EBU SOMA KWA MAKINI: MITHALI 16:29; MITHALI 22:24-25; 1 WAKORINTHO 8:10-11; WAGALATIA 5:7-9; YEREMIA 23:15; WARUMI 11:16]. Katika maandiko haya unaona jinsi ilivyo rahisi mtu kufuata nyayo za mahali pale alipo au watu alio pamoja nao. Neno la Mungu ni kweli.

Katika Ufunuo wa Yohana sura ya pili na sura ya tatu, tunaelezwa juu ya makanisa saba. Inakuwa ni vigumu mno kushinda na kupewa matunda ya uzima ukiwa katika Kanisa la Efeso; Pegamo; Thiatira; Sardi na Laodikia. Ukiwa katika Kanisa la Filadelfia ambalo linalitunza Neno la Mungu lote kwa gharama yoyote, utakuwa na nafasi kubwa mno ya kushinda.



Katika hekima ya dunia, wazazi huzunguka kumtafutia mtoto wao shule ambayo waalimu wake wana sifa ya kufundisha kwa bidii, ufahamu mkubwa; na wenye rekodi nzuri ya kupasisha wanafunzi wengi katika mtihani wa mwisho. Katika shule ya namna hiyo kunakuwa na nafasi nzuri ya mtoto huyo kushinda mtihani. Katika mambo ya rohoni ambayo ni ya milele ni lazima tuwe na maarifa hayo na zaidi!



MAMBO MATANO YA KUANGALIA KATIKA UCHAGUZI WA KANISA LAKO



1. USICHAGUE KANISA KWA SABABU LIKO JIRANI NA UNAPOISHI




Biblia inatuagiza kuutafuta Ufahamu wa Neno la Mungu kama:

(a) Fedha;

(b) Hazina iliyositirika (iliyofichika) [SOMA MITHALI 2:3-4]

Je fedha zinatafutwaje? Ukitaka kuzipata fedha inakubidi uwe tayari kuzitafuta hata ziwe mbali namna gani! Watu wanatoa nauli kwenda kufanya kazi ofisi au kiwanda kilicho mbali mno na pale wanapoishi. Watu wamehama makwao na kwenda maili nyingi sana na kujenga huko wakitafuta fedha, lakini hawako tayari kufanya hivyo wakitafuta Ufahamu wa Neno la Mungu. Je mkulima akitaka kulima mahali karibu na yeye tu, atapata fedha zinazotokana na mazao ya Kilimo? Watu, wako tayari kuyafuata mabonde yenye rutuba hata kama yako mbali namna gani! Ukitaka kulima mpunga kwenye Uwanja wa nyumba yako kwa kukwepa shida ya kulima mbali, unajua matokeo yake!



Je hazina iliyofichika inatafutwaje? Ni lazima uwe tayari kuchimba chini sana kwa gharama yoyote. Huwezi kupata madini ya thamani bila kuwa tayari kugharimika. Tanzania imetumia mamilioni ya fedha kufanya utafiti wa kupata petroli. Watu katika utafiti huo wana kwenda mbali sana na kuchimba chini sana. Kuchagua Kanisa kwa kuwa liko jirani na wewe, siyo kuchimba chini sana. Siyo kutafuta hazina iliyositirika. Katika MATHAYO 13:44-46, Yesu anaufananisha Ufalme wa Mungu na:-



(a) HAZINA ILIYOSITIRIKA KATIKA SHAMBA: (Msitari wa 44)

Mungu anasema ukimtafuta kwa bidii ndipo ataonekana kwako. Ufalme wa Mungu ni hazina iliyositirika katika shamba. Ni lazima uwe tayari kuitafuta kwa bidii hata kama iko mbali kiasi gani. Katika msitari wa 44, mtu yule alipoiona hazina hiyo aliuza VYOTE ALIVYO NAVYO na kulinunua shamba hilo. Ni lazima uwe tayari kutumia nauli au kutembea mwendo mrefu, kutafuta kweli ya Ufalme wa Mungu. Ukiridhika na vitu vinavyoonekana karibu, ujue hayo ni mawe tu na siyo hazina ya thamani.

Ijumaa, 18 Oktoba 2013

IJUWE FURAHA YA MUNGU KWA WATENDAKAZI

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe
SOMO: FURAHA YA MUNGU KWA WATENDAKAZI

Tunajifunza somo la msingi katika mfululizo wa masomo ya Shule ya Uinjilisti, kwa kuligawa katika vipengele vinne:-

( 1 ). KAZI TULIYOPEWA WATU TULIOOKOLEWA

( 2 ). UINJILISTI NI NINI?

( 3 ). NANI ANAHUSIKA NA UINJILISTI?

( 4 ). FURAHA YA MUNGU KWA WATENDAKAZI

( 1 ). KAZI TULIOPEWA WATU TULIOOKOLEWA

Siku chache kabla ya Yesu Kristo kupaa mbinguni, alitukabidhi kazi ya muhimu sana ya kufanya. Kazi hiyo, ni kuenenda ulimwenguni mwote na kuhubiri Injili kwa kila kiumbe, na kuwafanya mataifa au watu wasiookolewa, kuwa wanafunzi wa Yesu, na kuwafundisha kuyashika yote tuliyoamuriwa, baada ya wanafunzi hao kubatizwa kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Akasema kwamba, tukishiriki kufanya kazi hii, atakuwa pamoja nasi siku zote, hata ukamilifu wa dahari hata wakati atakaporudi tena ( MARKO 16:15; MATHAYO 28:19-20 ). Hili ni Agizo Kuu la Yesu Kristo kwetu. Wengi wetu tuliookolewa, hatumwoni Yesu Kristo akiwa pamoja nasi siku zote, kwa sababu hatushiriki kikamilifu kuifanya kazi aliyotupa Yesu katika Agizo Kuu hili. Kufanya kazi hii, ni kufanya kazi ya Uinjilisti.. Hili sasa, linatuleta katika kipengele cha pili cha somo letu.

( 2 ). UINJILISTI NI NINI?

WATUHUMIWA WA UCHOMAJI KANISA MBAGALA WAACHIWA



Na Happy Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewaachia huru, Hamed Sekondo na wenzie wanane waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha, kisha kulichoma moto Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Usharika wa Mbagala, baada ya kuwaona hawana kesi ya kujibu.

Uvamizi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema, ambaye alianza kwa kuikumbusha mahakama kuwa kesi hiyo ya jinai namba 294/2012 ilikuwa imekuja kwa ajili ya mahakama kutoa uamuzi wa ama kuwaona washtakiwa wana kesi ya kujibu au la.

ANGALIA JUMBA LA KIFAHARI LA ASKOFU KIUNA WA KENYA


Askofu Kiuna na mkewe.

Angalia nyumba ya kifahari ya Askofu Allan Kiuna iliyopo maneo ya Runda huko nchini Kenya, nyumba hiyo ni gumzo kutokana na uzuri wake, hasa ikiwa na huduma mbalimbali kama ilivyo kwa hoteli za hadhi ya juu, angalia picha hizi kama zilivyotolewa na mtandao wa SoftKenya.com

Askofu Kiuna anatunza kanisa kubwa la Jubilee Christian Centre (JCC) lililopo jijini Nairobi nchini Kenya,ni mume wa mchungaji Kathy Kiuna na baba wa watoto watatu. Pamoja na mafanikio yote hayo askofu Kiuna amekuwa akipitia majaribu mengi ikiwemo kuvumishiwa kwamba amegeuza nyumba ya Mungu kuwa sehemu ya biashara kutokana na utajiri wake, lakini pia kama haitoshi ametajwa kuwapa kazi vijana wenye uwezo mkubwa wa kuzungumza kiingereza ili kuvutia vijana wengi zaidi kujumuika kanisani kwake.

ANGALIA PICHA ZA JUMBA HILO LA MPAKWA MAFUTA WA MUNGU



Alhamisi, 17 Oktoba 2013

SARA MVUNGI;SIJAWALAZIMISHA WATOTO WANGU KUOKOKA.





Makala na Imelda Mtema

Sara amebarikiwa kupata watoto wawili, Nicolas (22) na Neema (1O). Anaishi Kigogo, jijini Dar. Kigogo anaishi na Neema, Nicolas anaishi na babu yake Afrika Kusini.
Ili kujua jinsi gani anavyoishi na mwanaye huyo, ungana nami katika mahojiano niliyofanya naye:
Staa na Mwana: Mambo dada Sara habari za hapa nyumbani?
Sara: Salama tu karibu nyumbani.
Staa na Mwana: Kwanza kabisa wasomaji wa Staa na Mwana wangependa kufahamu kuna tofauti yoyote maisha wanayoishi watoto wako na watoto wengine ambao siyo wa staa?
Sara: Hapana, hakuna tofauti maisha ya wanangu ni ya kawaida sana. Mimi mwenyewe sipendi waishi maisha tofauti na watu wa kawaida.
Staa na Mwana: Kwa nini? Maana mastaa wengine hutofautisha watoto wao na watoto wa kawaida.
Sara: Kwangu mimi sioni kama ni malezi kwa sababu mimi mwenyewe nililelewa maisha ya kawaida kabisa.
Staa na Mwana: Nini ambacho unajivunia kutoka kwa watoto wako?
Sara: Kwa kweli ni watoto ambao wananipenda sana na kunithamini, wao ndiyo kila kitu maana hakuna faraja ambayo ninayo zaidi ya watoto wangu.
Staa na Mwana: Kwa nini iwe watato na si baba yao?
Sara: Hakuna, maishani ni mimi, watoto wangu na Mungu tu.
Staa na Mwana: Kwani huishi na baba yao?