Jumanne, 7 Oktoba 2014

Biblia inasemaje juu ya kutoa fungu la kumi ama Sadaka ya Michango ?

Hawa ni wataalamu wa injili kwa watu wote GFAP wakiwa katika picha ya pamoja huko ROMBO KILIMANJARO

Jibu: Kutoa fungu la kumi ni jambo ambalo wakristo wengi hung’ang’ana nalo. Katika makanisa mengine kutoa fungu la kumi imesisitizwa kupita kiasi. Wakristo wengi pia hukataa kutii agizo la kutoa sadaka kwa Bwana. Kutoa fungu la kumi au sadaka inahitajika kuwa ni kitendo cha furaha na baraka. Lakini sivyo katika makanisa ya sasa.

Kutoa fungu la kumi ni agizo la agano la kale. Hili lilikuwa sharti la kila mwenye kupata zao au mfugo alete sehemu ya kumi ya pato hekaluni (mambo ya walawi 27:30; hesabu 18:26; kumbukumbu la torati 14;24; mambo ya nyakati ya pili 31:5). Wengine huchukulia ya kuwa fungu la kumi, katika agano la kale ilikuwa kama sehemu ya ushuru uliokuwa ukitolewa kwa ajili ya makuhani na walawi. Agano jipya haiamrishi wala kupendekeza mfumo halali wa kutolea fungu la kumi. Paulo asisitiza kuwa waumini watenge sehemu ya mapato yao kwa ajili ya kusimamia kanisa (wakorintho wa kwanza 16:1-2).
(1 Wakorintho 16 : 1-24
16.1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi
fanyeni vivyo.
16.2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili
kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;)

Agano jipya halielezi kiasi cha pato ambacho ni kitengwe kwa ajili ya kusimamia kanisa. (wakorintho wa kwanza 16:2). Kanisa la kikristo leo limechukua kile kiwango cha fungu la kumi kutoka kwa agano la kale na kukisisitiza kuwa ndicho kiwango cha chini cha mkristo kutoa. ijapokuwa agano jipya haitoi kiwango cha kutoa, inaelezea umuhimu na manufaa ya kutoa.

Ni watoe sawa na uwezo wao “ kulengana na pato lake.” Wakati mwingine ina maana ya kutoa zaidi ya fungu la kumi,

 Yote hutegemea uwezo wa mkristo mwenyewe na mahitaji ya kanisa. Kila mkristo sharti aombe na kutafuta hekima kutoka kwa Mungu juu ya swala hili (Yakobo 1:5). “ kila mtu niatoe kile alicho azimia kutoa kutoka ndani ya moyo wake, si kwa manung’uniko wala kulazimishwa, kwa kuwa Mungu hupenda kwenye kutoa kwa moyo mkunjufu” (wakorintho wa pili 9:7).

Pia hilo andiko nalipeleka kwa wale watumishi wa MUNGU wanao wapangia watu kiasi cha kutoa hususani kwenye michango,hakika jambo hili sio jema kwani kutoa kwa Toka KWA BWANA na haipendezi kumpangia mtu atoe nini bali kama alivyo sikia MOYONI mwake.

Pia katika makanisa ya leo usipo toa wanakuona kama mtu asiye endana nao yaani ajenti au msaliti hili sio sahihi kwani mtu kama mimisiwezi kutoa bila kusikia kwa hiyo hata msisitizo wakibina damu huwe mkubwa kiasi gani ni lazima nisikie kwa BWANA ama sivyo utakuwa tuu ni mchango na haifai kutoa kisha kunung'unika.

Siku njema na endelea kuetmbelea www.mwanakondooinjili.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni