Jumatatu, 20 Oktoba 2014

MAMBO MAKUU NNE (4) KATIKA UOKOVU WAKO


Wapili kutoka kushoto ndie Mtumishi Jeremiah Mlawa akiwa na watumishi wenzake katika maeneo ya Ibada, (Picha na Makitaba)
Na Mtumishi Jeremiah Mlawa
1.Uwe na Imani,Hakikisha ndani ya uokovu wako uwe ni mtu wa  imani,jiamini na pia amini sehemu unayoabudu.
2.Uwe Mkweli,Epuka kuwa muongo na penda kuwa mkweli kwa kushuhudia kweli ya MUNGU,pia usiwe mzungumzaji kwa mtu ambaye unajua atahadhiri uokovu wako.Unapo mshuhudia mtu kuhusu uokovu hakikisha wewe mwenye ni msafi ndani ya moyo wako na ukifanya hivyo jina la MUNGU halitatukanwa na ushuhuda wako utakuwa barua.
3.Uwe Mtii,Hakikisha kwenye eneo unalolelewa unatii unaloambiwa,usiwe mwepesi wa kuitikia na kutokutii.Unapo weka ahadi kwa mtumishi ama mpendwa hakikisha unatii.Penda kutii muda wako katika maswala yako yakimaisha kama ibada inaanza saa 2 kamili hakikisha unatekeleza ama kutimiza hilo,Baraka za MUNGU huenda na wampendao.
4.Uwe ni Mtu wa Haki.Hakikisha kwenye maisha yako unaishi kwa haki na watu wote,na mwenendo wako uwe wa haki,tafuta amani na watu wote.Usijiesabie haki kwa kumuona mtu Fulani ambae ni mwenye dhambi anahatia na wewe ni bora kuliko yeye,Mungu wetu ni Mungu wa wote wenye mwili.Kama unawaona wako kinyume wewe waombe.

Ukiyazingatia haya hakika hali yako ya kiroho itakuwa ya utofauti kwa viwango vikubwa mno.MUNGU wetu wa mbinguni na BWANA YESU akuwezeshe kutii hayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni