Jumanne, 24 Desemba 2013

HATUA SABA ZA KUIMARISHA USHIRIKA WAKO NA MUNGU.(maamuzi saba) (2)

WAKWANZA KULIA NI MCH. WA KANISA HILI LA VICTORY CENTRE ALOYCE MBUGHI NA WA KWANZA KUSHOTO NI MAMA MCH. CATHERINE MBUGHI.
Ninayo furaha ya hali ya juu kukukaribisha hususani ewe uliye mpenzi wa blogu hii ya www.mwakasegeinjili.blogspot.com,  siku ya leo kama ilivyo kuwa jana ninakuletea muendelezo wa somo la HATUA SABA ZA KUIMARISHA USHIRIKA WAKO NA MUNGU.(maamuzi saba).

Kwa uwezo wa YESU KRISTO na tumaini tutakuwa pamoja na kufanyika kazi,kabla hatuja endelea na hatua ya pili, tafadhali kama uliikosa hatu ya kwanza bonyeza link hii ili usome sehemu ya kwanza kisha ndipo uendelee na sehemu hii ya pili, http://mwakasegeinjili.blogspot.com/2013/12/hatua-saba-za-kuimarisha-ushirika-wako.html#more

Kabla ya kukujuza hatua ya pili kwanza tujikumbe mstari wetu wa kusimamia,
ZAB 27:4 Neno moja nimelitaka kwa Bwana  nalo ndilo nitakalolitafuta,nikae nyumbani mwa Bwana siku zote za  maisha yangu niutazame uzuri wa BWANA nakutafakari hekaluni mwake.

Andiko hili linatufundisha ya kwamba Daudi alilipa kipaumbele jambo hili ili atafakari uzuri wa MUNGU.
Hatua ya pili, HUUISHA JUUDI YAKO KUTAKA KUMJUA YEYE KWA UKARIBU ZAIDI.(yeye maana yake ni MUNGU, Neno kuuwisha maana yake kufufu)

Tafadhali soma name mstari huu,WAFILIP 3:10 ILI NI MJUE YEYE, NA UWEZA WA KUFUFUKA KWAKE , NA USHIRIKA WA MATESO YAKE NIKIFANISHWA NA KUFA KWAKE .

Kwa ajili ya YESU Paulo aliacha mambo ambayo yalikuwa ya mpe au yaliyomfanya aonekane kama ni mtu mwenye sifa na heshima kubwa sana kwa watu kwani alikuwa ni msomi wa hali ya juu na mwalimu wa torati na pia litoka katika kabila la Benjamini ambalo ndilo kabila la kwanza kumtoa mfalume ambae ni Sauli pia alikuwa ni mwebrani aliye kijua kiebrania.Ila kwa ajili ya Mungu aliviacha hivyo vote.

Mpendwa MUNGU hujifunua kwa mtu kulingana na kiu na shahuku aliyonayo  kwake.Wanathiolojia wanasema ya kwamba wakati Paulo antoa kauli hiyo alikuwa na mika thelathi ya kutembea na YESU KRISTO lakini bado kwake haikutosha kutokuwa na shahuku ya kuendelea kumjua MUNGU.

Paulo alihitaji kuzama ndani zaidi yaani hakutaka kuwa na uhusiano wa juu juu, ndugu msomaji siju shahuku yako ni ipi ila mtume PAULO shahuku yake ilikuwa ni kumjua MUNGU.

Katika shahuku hii yake ndipo MUNGU alijifunua kwake zaidi kwani ndie mwenye mchango mkubwa zaidi kweyne AGANO JIPYA ,,unapo soma karama tano,HUDUMA TANO ni mtume PAULO.

Hayo yote ni matunda na matokeo yake kutokakana na shahuku yake ya kumjua MUNGU,,Wanatheolojia wanasema ya kwamba katika ulimwengu alioishi PAULO hakukwepo mtu aliye mcha MUNGU kama yeye.

Laiti kama dunia ingemtafuta MUNGU kama inavvyo tafuta fedha kwani watu huamka alufajiri,huamua kuchimba madini na shuhuli ngumu ili wapate fedha ila kwa MUNGU wengi ni wavivu hadi wasukumwe, Ila PAULO hakuwa hivyo alijiwekeza kwa MUNGU zaidi.

Tuachane na ukristo wa kidini dini, tuzame ndani zaidi,Ukiwa na ushirika wa karibu na MUNGU utaitambua sauti yake .
YOHANA 10:4  NAYE  AWATOAPO NJE KONDOO WAKE WOTE,HUWATANGULIA; NA WALE KONDOO HUMFWATA KWA MAANA WAIJUA SAUTI YAKE.

Kuna mmarekani mmoja alienda mashariki ya kati na kuwakuta wachungaji wakilaza kondoo katika pango moja na inapofika asubuhi mchungaji moja huwaita kondoo wake nao humfwata na mmarekani Yule alijaribu kuvaa nguo zayule mchungaji akawaita lakini hawakuja,kwa nini ? kwa sabau hawakuijua sauti zake.
Tazama tena andiko hili,

ZAB 103:7 ALIMJULISHA MUSA NJIA ZAKE WANAWAIZIRAELI MATENDO YAKE.
Pia tembelea andiko hili,KUTOKA 33:1-10     Utaona jinsi ambavyo MUSA alivyo kuwa akishirikiana na MUNGU.,NI vizuri kuyajua matendo ya MUNGU kama wana waiziraeli, ila ni vizuri zaidi kuzijua njia zake kama MUSA.Wanahistoria wanasema ya kwamba hakujawai kutokea nabii ambae alitembea na MUNGU kama MUSA.
Musa aliijua sauti ya MUNGU haraka,,Njia za kumjua MUNGU ni kusoma NENO kwa bidii kwani unaposoma NENO MUNGU husema nawe, pia MAOMBI na KUABUDU,KUSHUKURU,KUSIFU, na pia SADAKA.

1TIMOTHEO 2.1 BASI KABLA YA MAMBO YOTE NA TAKA DUA,
DUA ni maombi ya kusihi.
SALA ni mazungumzo kati yako na MUNGU. Kukemea sio maombi kwani maombi ni yale ambayo yanaelekea kwa MUNGU.
MAOMBEZI, ni pale unapo ombea kanisa,nchi mtu au sehemu Fulani pia SHUKURANI ni maombezi.

Hatuwezi kumjua MUNGU pasipo NENO, MUNGU wetu anaishi katika NENO.Lazima uwe na kawaida ya kulisoma NENO kila uchwao.
Unapo endelea kumsogelea MUNGU hautahitaji maombi kwani yataondoka yenyewe kwani MUNGU wetu ni moto ulao, kwenye moto mende na nzi hawasoge.

Tatizo la wakisto wanataka kuishi leo kama enzi za agano la kale kwani zamani watu wache ndio waliokuwa wakiingia kwenye PATAKATIFU-PATAKATIFU ila toka pazia lipasukuke pale YESU akiwa msalabanii sasa kila mtu anayo haki ya kumwendea MUNGU wetu.

Tutazame kitabu cha,
DANIELI 11:12  NA WALE WAMJUAE MUNGU WATAKUWA HODARI NA WATENDA MAMBO MAKUU.
Maana yake watu wasiomjua MUNGU wao hawawezi kuwa hodari na hawataweza kufanya mambo makuu,Danieli alipitia nyakati Ngumu lakini alishinda kwani alimjua MUNGU wake,Danieli alikuwa ni mtu wa maombi hata pale walipo tafuta makosa kwake waliyakosa hadi ikabidi wayatafute kwa ushirika wake na MUNGU wake; ilibidi wa mtupe kwenye simba.Simba hawezi kumtafuna mtu mwenye ukaribu na MUNGU.

Unaweza kuishi kama mfalume utumwanai kama unamjua MUNGU,
Ujumbe huu umetolewa leo madhabahuni katika kanisa la VICTORY CENTRE LA TAG lililopo hapa mkoani ARUSHA eneo la kwa MOROMBO na mwalimu EZEKIELI JOSEPH kutoka jijini DR ES-SALAAM,      

LANGU JINA NI OSCAR SAMBA, nimeokoka na ninampenddaa YESU WEWE JE?
Kama bado basi ungana nami kwenye sala hii kisha utaokoka kumbuka kuokoka sio dini mpya bali ni mwanzo mpya na MUNGU WETU ALIYE MBINGUNI , tuanze sasa;
“Ee MUNGU WANGU ULIYE MBINGUNI MIMI NI MWENYYE DHAMBI NA MIMESIKIA HABARI ZAKO NA KUZIAMINI EWE YESU NI SAFISHE KWADAMU YAKO NA UNIKOWE”
Ongera kwa kuokoka na sasa tafuta kanisa la walokole linalo hubiri injli iliyo hai,siku njema na endelea kuifwatilia blogu hii ya www.mwakasegeinjili.blogspot.com
                       SIKUKUU NJEMA


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni