Jumatatu, 27 Januari 2014

NILIITWA MWANAMKE MBAYA KULIKO WOTE DUNIANI, LAKINI UZURI UPO NDANI YANGU -- LIZZIE


Mwanadada Lizzie Velasquize (24) mzaliwa wa Texas Marekani ambaye ameitwa majina na maneno mbalimbali mabaya kutokana na watu kudai ni mwanamke mwenye muonekana mbaya zaidi duniani amesema uzuri upo ndani ya mtu na si nje kama wengi wanavyodhani.

Jumapili, 26 Januari 2014

MWALIMU LILIAN NDEGI AKAMIA KUUKOMBOA UZAO WA MWANAMKE

Ritha Chuwalo,
GK Guest Contributor

Mwalimu Lilian Ndegi akizungumza jambo kuhusu kitabu chake.
Wito umetolewa kwa wanawake wajawazito, wakina mama walio katika malezi pamoja na mabinti kusoma kitabu cha Mungu na Uzao Wangu kilichoandikwa na Mwalimu Lilian Ndegi wa Kanisa la Living Water Centre chini ya mtume Onesmo Ndegi lililopo Kawe jijini Dar-es-salaa, Tanzania.

Akitoa wito huo katika uzinduzi wa kitabu hicho hivi karibuni, Mwalimu Lilian Ndegi amesema kuwa, kitabu hicho ni msaada mkubwa kwa wakinamama wajawazito kwani watapata maarifa ya Ki-Mungu yatakayowasaidia kuwaondoa katika uharibifu wa mimba tangu inapotungwa, inapolelewa, pamoja na wakati wa kujifungua mtoto na kwamba hiyo inawahusu pia na mabinti ili kuwasaidia kuwa na uzazi mwema hapo baadae.

Akifafanua zaidi amesema kuwa Serikali ya Tanzania imeweka utaratibu mzuri wa kujenga vituo vya afya kuwasaidia wakina mama wajawazito, na kwamba mila na desturi nazo zina kanuni zake, lakini wakati umefika kwa Kanisa kujihoji Mungu anasema nini juu ya uzao wa Mwenye Haki na kwamba litembee katika kanuni zipi ili kuweza kupata ushindi mkubwa katika Uzazi.

HOJA YA ASKOFU GAMANYWA: FALSAFA YA UMILIKAJI KWA MUJIBU WA BIBLIA (3)


Rais wa WAPO Mission International, Askofu Sylvester Gamanywa.
Katika makala yaliyopita tulisoma habari kuhusu “Mpango wa pili wa Mungu ukombozi wa binadamu” ambao uliambatana na “Majibu ya maswali nyeti kuhusu falsafa ya kumiliki” aidha niliahidi katika makala hii kwamba nitaweka bayana tofauti kati ya “Hi Falsafa ya umilikishaji kwa mujibu wa Biblia na “Injili ya utajirisho”. Leo naanza na muhutasari wake:

Jumamosi, 25 Januari 2014

HARUSI YA KANA (wedding in Cana of Galilee) * sehemu ya 1 & 2 *

Na mtumishi Gasper Madumla.
“ Na siku ya tatu palikuwa na harusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.” Yoh.2:1-2
Nakusalimu mpendwa;
Bwana Yesu asifiwe…
Karibu tuendelee sasa;
KANA ni mji wa magharibi mwa ziwa Galilaya,mahali ambapo Bwana Yesu Kristo alifanya muujiza wake wa kwanza wa kubadili maji kuwa divai. Muujiza huu ulikuwa mkubwa sana maana Biblia inasema kupitia muujiza huo,Bwana Yesu akaudhihirisha UTUKUFU wake,
nao wanafunzi wake wakamuamini.

Ijumaa, 24 Januari 2014

HABARI NJEMA KWA WAPENZI WA KUNDI LA GLORIOUS WANARUDI TENA KILA IJUMAA


Baada ya kupumzika kwa takribani miaka miwili toka wasimamishe ibada za kusifu na kuabudu siku za Ijumaa jioni, kundi la Glorious Worship Team (GWT) chini ya kiongozi wake Emanuel Mabisa kundi hilo limetangaza kuanza upya tena ibada hizo kuanzia ijumaa ya kwanza ya mwezi wa pili mwaka huu ingawa bado hawajatangaza mahali watakapokuwa wakifanyia maonyesho hayo awali kabla ya kusimamisha walikuwa wakifanyia katika ukumbi wa hoteli ya Atriums iliyopo Sinza jijini Dar es salaam.

Alhamisi, 23 Januari 2014

HIVI NI VIGUMU KUSUBIRI MPAKA NDOA? MBONA WENGINE WANAWEZA, SOMA MWENYEWE


Megan Good na mumewe Devon Franklin walisubiri mpaka ndoa.

Mariah Carey na mumewe Nick Cannon
Suala la kusubiri kuingia kwenye uhusiano wa mke na mume kabla ya ndoa limekuwa na matatizo kwa watu wengi haijalishi cheo au imani zao, kutokana na kitendo hiki watu wengi wamejikuta wakiangukia dhambini kwakuanza kuishi kama mke na mume kabla ya ndoa ama baada ya kukaa kwa muda mrefu na kujaaliwa watoto ndipo hukumbuka kurudi kanisani kubariki ndoa zao. lakini pia kuna wale ambao wanataka kujaribu na kujikuta wakipanda madhabahuni tayari wamechoka, ndoa ambazo zimeongezeka kwa kasi sana nchini.

AINA NNE ZA KUSIKILIZA - MCHUNGAJI MITIMINGI


Mkurugenzi wa huduma ya VHM mchungaji Peter Mitimingi.
1. Kusikiliza kwa Kumkubali Mtu (Appreciative Listening)
a. Unamwangalia mtu kwa mtazamo wanje na unam“Judge” kama utamsikiliza au la.
b. Madereva Taxi wengi Humangalia mtu kwa nje akiwa amevaa vizuri kapendeza wanamgombania kumbe mfukoni hana kitu. Aliye vaa hovyo hovyo hakuna anae shughulika naye kumbe huyo mwenye matope katoka Melerani ndio mwenye pesa.

Jumatano, 22 Januari 2014

SOMO : JINSI YA KUFAHAMU MIUJIZA YA SHETANI


Askofu Zachary Kakobe

Nyakati tulizonazo leo,zinzitwa NYAKATI ZA HATARI..Biblia inasema kwamba siku hizi za mwisho,wengine watajitenga na imani,wakisikiliza ROHO ZIDANGANYAZO na MAFUNDISHO YA MASHETANI (2TIMOTHEO 3:1,1TIMOTHEO 4:1).

Roho zidanganyazo zitafanya kila namna,kutudanganya,ili kile cha Mungu tukiite cha shetani,na kile kilicho cha shetani,tukiite cha Mungu.Leo,tunazungukwa na watu wanaosema,jihadhari usiende kule.

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU * sehemu ya mwisho*


Mtumishi Gasper Madumla.

Bwana Yesu asifiwe...
Haleluya...

Nazungumzia habari ya Lazaro wa Bethania,mwenyeji wa mji wa Mariamu na Martha dada yake. Nalikuambia kwamba yapo mambo mengi sana ya kujifunza,lakini tumejaribu kuchambua yale machache tu,kwa sehemu yake.Kama laiti tutazungumzia kila aina ya mstari kupitia ufufuo wa Lazaro,basi ukweli ni kwamba tusingeweza kumaliza fundisho hili siku ya leo,yamkini fundisho hili lingeisha baada ya miezi mitatu hivi.

Jumatatu, 20 Januari 2014

NYOTA WA MUZIKI WA INJILI MAREKANI AFIWA NA BABA YAKE MZAZI


Mwimbaji anayetamba na limbo wake maarufu "Breaks every chains" Tasha Cobbs wa nchini Marekani amefiwa na baba yake mzazi askofu Fritz Cobbs katika taarifa ambayo ilitolewa na mwimbaji mwingine wa injili nchini humo James Fortune kupitia mitandao ya kijamii kwakuwataka wapenzi wa muziki wa injili kumkumbuka katika maombi mwimbaji huyo kwakuwa amefiwa na baba yake mzazi.

Jumapili, 19 Januari 2014

HOJA YA ASKOFU GAMANYWA : FALSAFA YA UMILIKISHAJI KWA MUJIBU WA BIBLIA (2)


Rais wa WAPO Mission International, Askofu Sylvester Gamanywa.

Falsafa ya umikilishaji kwa mujibu wa Biblia

Wiki iliyopita tulianza hoja hii kuhusu falsafa ya kumilikisha kwa mujibu wa Biblia. Aidha, tulipitia vipengele vya Mpango wa kwanza wa Mungu kwa binadamu na jinsi ulivyolenga kumfanya binadamu kutawala nchi na vitu vilivyomo. Kisha tukapitia anguko la binadamu wa kwanza na athari zake. Sasa katika toleo hili tunaendelea na sehemu ya pili kuhusu mpango wa pili wa Mungu wa ukombozi wa binadamu na matokeo yake:

Jumamosi, 18 Januari 2014

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU*sehemu ya tano.*


Mtumishi Gasper Madumla.
Bwana Yesu apewe sifa....
Haleluya....
Nakusalimu katika jina la Bwana...

Najua yapo mengi tumejifunza kwa habari ya Lazaro wa Bethania,ambaye alifufuliwa na Bwana Yesu.

BALOZI AWAONGOZA WATANZANIA NCHINI UINGEREZA KATIKA IBADA KUIOMBEA MAFANIKIO NCHI YAO


Kiongozi wa kanisa la Worldchangers mtume Mathew Jutta akimsifu Mungu kanisani hapo.
Waumini kutoka sehemu mbalimbali za jiji la London nchini Uingereza walikutanika jumapili iliyopita maeneo ya kusini mashariki mwa jiji la London kuombea mpenyo na mafanikio kwa mwaka mpya wa 2014 kwa Taifa la Tanzania chini ya uongozi wa Rais Jakaya Kiwete,maombi ambayo yaliandaliwa na kanisa la Worldchangers ministries chini ya mtumishi na mwanzilishi wake mtume Mathew Jutta na kuhudhuriwa na balozi wa Tanzania nchini Uingereza mheshimiwa Peter Kallaghe.

Alhamisi, 16 Januari 2014

FAMILIA YAUZA KILA KITU ILI KUMUHUBIRI KRISTO KWA MASIKINI


George, mkewe na watoto wao ©indiegogo
Familia ya bwana George na mkewe Vonda Sisneros yenye jumla ya watoto wanne ambao walikuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali za kujipatia kipato huko nchini kwao Marekani, mume akimiliki kampuni ya usafi pamoja na usafishaji wa mazuria huku mke akiwa ni msanii anayejishughulisha na uchoraji wameamua kuuza mali zao zote ili kuwa wamisionari wa kuhubiri habari njema za Yesu huko Guatemala.

Jumatano, 15 Januari 2014

Akef Tayem, Mwislamu Kutoka Palestina Akutana na Bwana Yesu na Kuokoka – Sehemu ya 3

Mpendwa msomaji na mpenzi wa blog hii, naamini ulishasoma sehemu ya 1 na ya 2 za ushuhuda huu wa Akef. Hii ni sehemu ya 3 na ya mwisho inayoonyesha ukuu, upendo na uweza wa Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo, yaani Yesu Kristo. Karibu usome sehemu hii na Bwana Yesu akubariki.

Akef Tayem, Mwislamu Kutoka Palestina Akutana na Bwana Yesu na Kuokoka - Sehemu ya 2

Baada ya Akef Tayem kukataliwa na familia yake kwa sababu amekubali kumpokea Yesu Kristo maishani mwake, alijikuta akikosa kabisa hamu ya kula kwa siku zaidi ya 40 akiwa porini. Mwili wake ulidhoofika sana na kuishiwa maji. Yafuatayo ni mahojiano kati ya mtangazaji, Sid Roth and Akef Tayem:

Sid Roth:
Je, ulimwomba Mungu akunyeshee mvua?


Akef:
Ndiyo. Ndiyo. Nilikuwa na kiu sana, na nilikuwa dhaifu mno.


Sid Roth:
Je, ilionekana kama kuna mvua itanyesha?


Akef:
Hapana. Hakukuwa hata na dalili; wala hata wingu. Nilidhoofika sana kiasi kwamba sikuweza hata kutembea kwenda kwenye kutafuta maji au chochote kingine.


Sid Roth:
Ulinieleza kuwa ngozi yako ilianza kupasukapasuka.

Akef Tayem, Mwislamu Kutoka Palestina Akutana na Bwana Yesu na Kuokoka - Sehemu ya 1

Yafuatayo ni mahojiano kati ya mtangazaji, Sid Roth na Akef Tayem. Akef Tayem anatokea Palestina. Alikuwa ni Mwislamu lakini sasa anamwamini Yesu kama Bwana na Mwokozi wake. Pia anawapenda sana Wayahudi ambao zamani aliwachukia kwa moyo wake wote. Je, nini kilitokea? Hakika Bwana Yesu anahusika humo! Karibu ukutane na Bwana wa mabwana anayeweza kubadilisha maisha yako kwa namna ya kushangaza.
……………

LIPO KUNDI KUBWA LA WATU WALIOCHANGAMANA NDANI YA WOKOVU.



Mtumishi Gasper Madumla.

Bwana Yesu asifiwe...

Nimejaribu kujizuia nisiseme hivi lakini nimeshindwa kujizuia,ni bora leo niseme tu kwa watu wote maana injili yapaswa kuhubiriwa,na kwenda kote katika mataifa,na hiyo ndio kazi tuliyopewa maana maandiko yanatuambia;

Jumanne, 14 Januari 2014

MWANAMUZIKI FEROUZ AKAMATWA NA BANGI, VIJANA NDO HUANGAMIA HIVI

Vijana ni nguvu kazi ya taifa, lakini vijana hao hao wanaweza kuwa chanzo cha taifa kutoendelea na kubomoka. Ubomoaji wa taifa huwa kwa namna nyingi ikiwemo uvivu, ufisadi, na kadha wa kadha. Lakini hapa, tuangalie hili la madawa ya kulevya na bangi.

Ferouz (mwenye kofia) akiwa chini ya ulinzi

Jumapili, 12 Januari 2014

MAKALA : FALSAFA YA UMILIKISHAJI KWA MUJIBU WA BIBLIA :ASKOFU GAMANYWA



Mwaka mpya wa 2014, Askofu Sylvester Gamanywa, ambaye ni Mwangalizi Mkuu wa kitaifa na kimataifa wa WAPO MISSION INTERNATIONAL, amezindua kampeni mpya inayoitwa OPERESHENI MILIKISHA. Madhumuni ya kampeni hii ni kuendelea kuelimisha waamini na jamii kwa jumla ukweli kuhusu mpango wa Mungu kuhusu haki na mamlaka ya kila binadamu kumiliki uchumi endelevu. Kupitia makala haya Askofu Gamanywa anafundisha kuhusu Falsafa ya Umilikishaji kwa mujibu wa Biblia:

WAKRISTO WA TANZANIA HATARINI, RIPOTI

Tanzania imeshika nafasi ya 49 kati ya nchi 50 ambazo Shirika la Open Doors la Marekani katika ripoti yake ya mwaka "2014 Watch List" imesema ndio nchi hatari zaidi duniani kwa wakristo kuishi. Katika ripoti hiyo Open doors wameiweka Tanzania katika kundi ambalo wakristo huishi kwa wasiwasi huku pia likitoa idadi ya nchi 10 ambazo ni hatari zaidi duniani kuwa Mkristo. Open doors hujishughulisha na kusaidia wakristo waliopo vifungoni wakiwa katika hatari ya kuuwawa kutokana na kutetea ama kuhubiri injili ya Yesu Kristo.
Katika orodha iliyotoa, shirika hilo limeonyesha nchi ambazo wakristo wanaishi kwa kujificha, manyanyaso, kutekwa lakini pia wakiwa katika hatari ya kuuwawa na serikali za nchi hizo ama vikundi hatari vya dini vya watu wenye msimamo mkali wa dini.

Jumamosi, 11 Januari 2014

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU


Mtumishi Gasper Madumla.
Karibu tuendelee kujifunza zaidi siku ya leo,ikiwa leo ni siku ya nne ya fundisho hili.
Tunajifunza mambo mengi sana kupitia habari ya Lazaro wa Bethania mwenyeji wa mji wa Mariumu,yule aliyefufuliwa na Bwana Yesu.Yapo mambo ambayo ni msaada kwetu,na kupitia hayo tutavuka,
Basi nakusalimu katika jina la Bwana Yesu;

Ijumaa, 10 Januari 2014

Ujumbe kutoka kwa Mwalimu Christopher Mwakasege:IKIMBIENI ZINAA

Je! Unaamini ya kuwa Mungu anaweza kusema na watu kwa njia ya ndoto? Najua ni rahisi kuamini kuwa Mungu alisema na watu zamani kwa njia ya ndoto kama tunavyosoma katika Biblia; lakini je! Unaamini ya kuwa Mungu anasema na watu kwa njia ya ndoto siku hizi?

Mwl Christopher Mwakasege

Najua kuna watu wanaoamini na wengine hawaamini. Sijui wewe uko upande gani.
Lakini nataka nikueleze hivi; Kufuatana na Biblia kuna ndoto za aina tatu;
(a) Kuna ndoto kutoka kwa Mungu. Soma kitabu cha Hesabu 12:6, na Yoeli 2:28.
(b) Kuna ndoto zinakuja kwa sababu ya shughuli nyingi. Soma kitabu cha Mhubiri 5:3.
(c) Kuna ndoto za uongo zinazotoka kwa shetani aliye baba wa uongo. Soma kitabu cha Yeremia 23:52 na Yohana 8:44.

Mwl Christopher Mwakasege atoa shuhuda juu ya kifo Fanuel Sedekia


Mwalimu Christopher Mwakasege

Mwalimu Christopher Mwakasege ametoa ushuhuda huo kati seminazake katika viwanja vya Furahisha jijini Mwanza Semina hiyo yenye somo linaloitwa namna ambavyo Roho Mtakatifu awezavyo kukusaidia ili upokee kile unachokiomba imeanza tar 19-07-2011 na inatazamiwa kuisha tar 23-07-2011.

JIFUNZE KULINDA NA KULISIMAMIA WAZO LA MUNGU NDANI YAKO (Part 2)

Huu ni muendelezo kutoka Somo la jumatatu wiki iliyopita lenye kichwa cha habari JIFUNZE KULINDA NA KULISIMAMIA WAZO LA MUNGU NDANI YAKO (Part 1) Kutoka kwa Mwl Sanga.Namna ya kutoka kwenye tatizo ambalo uliingia kupitia maamuzi uliyoyatekeleza. Kumbuka kwenye sehemu ya kwanza ya somo hili niliandika kwamba; Maisha (future) ya mtu ni matokeo ya mawazo jumlisha maamuzi anayotekeleza kwenye maisha yake. Mawazo na maamuzi yako yataamua kile utakachozaa/kitakachofunuliwa, Utakachozaa kitaamua future yako na future yako itaamua mwisho (destiny) yako.

JIFUNZE KUMTEGEMEA MUNGU KATIKA MAAMUZI YAKO

Katika maisha yetu kila siku ni rahisi kufanya maamuzi kwa mazoea kwa kua ndivyo tulivyozoea au ndivyo tulivyozoeshwa. Biblia inasema "Tazama Mtu akiwa ndani kristo amekua kiumbe kipya 2kor2:17".

ALIYEMUONA AMINA CHIFUPA MSUKULENI ATOA USHUHUDA KWA MARA NYINGINE

ILITOLEWA Monday, June 24, 2013

Maelfu ya watu kutoka ndani ya jiji la Dar es salaam na viunga vyake walikusanyika hapo jana katika ibada kubwa ya matendo makuu ya Mungu iliyoambatana na tamasha kubwa la uimbaji katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe jijini Dar es salaam ambako ndiko makao makuu ya kanisa kubwa la Ufufuo na Uzima lililo chini ya askofu Josephat Gwajima.

Moja kati ya matukio yaliyomrudishia utukufu Mungu ni

ANGALIA VIDEO KWANINI KANISA LA GWAJIMA HAWAJAMUOMBEA AMINA CHIFUPA KURUDI HAI


Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia ©CloudsFm.
GK imefanikiwa kuiona video hii ambayo mchungaji Josephat Gwajima mwanzilishi wa kanisa la Ufufuo na Uzima Duniani likiwa na makao makuu yake viwanja vya Tanganyika Packers jijini Dar es salaam, akifafanua kwanini hawajamuombea kumrudisha duniani aliyekuwa mbunge wa viti maalumu wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mtangazaji wa kituo cha Clouds Fm cha jijini Dar es salaam, Tanzania marehemu Amina Chifupa Mpakanjia.

Alhamisi, 9 Januari 2014

INJILI YA UPOTOFU YA IBUKA, NABII HUYU ANAOMBEA WATU KWA KUWAGANYAGA KISHA ANAWALISHA MAJANI KAMA MBUZI NA KUWAAMBIA ETI YANATOKA MBINGUNI,,ONA PICHA ZOTE.


Mdada akila majani ambayo huduma hiyo wanasema ni chakula kutoka mbinguni mwe!
Kuna mengi ambayo yamekuwa yakizungumzwa kuhusu huduma za watumishi mbalimbali, moja wapo ni hii huduma iitwayo Rabboni Centre ministries iliyopo Pretoria nchini Afrika ya kusini, huduma hii iliyochini ya mwanzilishi wake mwalimu ,mchungaji na nabii Daniel Lesego ilianza mwaka 2002. Ni huduma ambayo kwa watu wasioabudu hapo huitilia mashaka kutokana na mwenendo wake.

Kwasasa wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na hatimaye wanaishia kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo akisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni.

Inaelezwa kwamba mara baada ya maombi waumini wengi huanza kutapika jambo ambalo kanisani hapo huashiria kwamba mtu amejazwa Roho Mtakatifu.

Lakini kama haitoshi nabii Lesego hufanya maombi huku amewakanyaga watu. Huduma hii imekuwa gumzo nchini humo na nchi jirani kwa jinsi mambo yao yanavyokwenda.

Mnasemaje watumishi kuhusu jambo hili? mwe kula manyasi kweli? mma!


Hapa nabii huyo akikanyaga watu kama njia ya mafundisho yake.


Haa!! angalia jamani, sasa ng'ombe watakula nini jamani???


Mungu tufunulie macho ya rohoni kuyajua mambo haya kama ni wewe au sisi kha!


Hajamaliza bado.

Baada ya manyasi ni mwendo wa kutapika sasa

Jiandae kwa kurudi kwa Bwana! Sehemu ya 2

Mpendwa msomaji wa blog hii na mwana wa Mungu aliye hai, hii ni Sehemu ya 2 ya ushuhuda huu. Katika Sehemu ya 1, tuliona safari ya kwanza mbinguni ya dada Bernarda. Katika sehemu hii, anatueleza kile kilichotokea pale Bwana Yesu alipomchukua kwa mara ya pili na kwenda naye mbinguni kisha akamrudisha.
Safari Yangu ya Pili
Siku moja tulikuwa sote kwenye maombi; tulikuwa watu takribani ishirini. Kama kawaida, tulianza kwa kumsifu na kumtukuza Bwana.


Ghafla, tulihisi uwepo wa Mungu. Ulikuwa na nguvu sana kana kwamba ilikuwa ni siku ya Pentekoste. Nakumbuka mama mkwe wangu, bibi mzee ambaye alijitoa kwa Mungu, aliniambia, “Bernarda, hebu tupunguze kelele wakati wa kusifu. Tunapaza mno sauti.”

Jumatano, 8 Januari 2014

SOMO : KUISIKIA SAUTI YA MUNGU BY MCHUNGAJI GWAJIMA


Josephat Gwajima

Mara nyingi tunamwomba Mungu lakini hatufahamu kuisikia sauti yake anaposema nasi Kuna namna kadha wa kadha za kuisikia sauti ya Mungu.
i. Katika maono
ii. Katika ndoto
iii. Katika neno la Mungu
iv. katika njia ya manabii wake
v. sauti ya ndani ya Roho Mtakatifu
vi. Kupitia mzingira
vii. kupitia walimu wa Neno la Mungu

Jumatatu, 6 Januari 2014

IANDAE KUPOKEA KUTOKA SHANGILIENI KWAYA ARUSHA

Hii ni habari njema kwa wapenzi wa kwaya ya Tumaini Shangilieni ya mkoani Arusha pamoja na wapenzi wa nyimbo za injili kwani kwaya hiyo ipo bize kwa wakati huu ikiendelea na kurekodi video yao mpya ya tano kutoka katika album yao ya "Nisamehe" ambayo video yake walianza kurekodi nchini Afrika ya kusini walipotembelea mwishoni mwa mwaka jana.


Video hiyo ikikamilika itakuwa ni video ya tano ya kwaya hiyo ambayo ilitamba na video yao ya kwanza inayoitwa Shangilieni na kufuatiwa na Shangilieni part 2, video ya tatu Unishike huku video ya nne ni ya nyimbo za matumaini (Tenzi za Rohoni) ambayo walirekodi live na sasa wanaandaa ya tano itakayoitwa "Nisamehe.

Mambo yakipamba moto, hapana shaka wimbo huu ni Nisamehe

Jumapili, 5 Januari 2014

MAPEPO YAGUNDULIKA KUWA VYANZO VYA MATATIZO MENGI YA WATU

Akifundisha katika Mkutano wa maelfu ya watu Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima alieleza kuwa mapepo(mashetani au majini) ndio vyanzo vya matatizo yanayowakumba watu wengi leo hii. Baada ya kufundisha kwa dakika chache Mchungaji alianza kufundisha kwa vitendo na alipoanza tu mapepo yaliyokuwa ndani ya watu mbalimbali yalidhirika na baada ya uponyaji watu hao walielezea matatizo yalikuwa yanawasumbua muda mrefu ambayo yalitokana na kupagawa na pepo waliowangia ndani yao.

Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Amina Salum (Chini katika picha) ambaye hapo awali kabla ya kuokoka alikuwa muislamu, alikuja katika mkutano wa Ufufuo na Uzima akisumbuliwa na magonjwa mbalimbali.


Akieelezea tatizo lake, Amina alisema kuwa alikuwa na tatizo la tumbo ambalo alikuwa akisikia kuwa tumbo linachoma choma ndani kiasi cha kushindwa kula. Tatizo ambalo lilimdhoofisha mwili siku hadi siku.


Wakati Mchungaji Gwajima akipita katikati ya makutano alimkuta amekaa na mapepo yaliyokuwa ndani yake walipomuona mchungaji wakadhihirika kutokea ndani yake ambapo na baadaye yalipewa amri yamtoke mtu huyo. Baada ya hapo dada huyo alipona kabisa magonjwa yake papo hapo.

IBADA YA MWAKA MPYA NA CHAKULA CHA BWANA LUTHERAN LONDON



Hapo jana katika kanisa la Kilutheri usharika wa mtakatifu Anne's jijini London kumefanyika ibada ya kiswahili ya jumapili ya kwanza ya mwezi kama ilivyoada ikiongozwa na mchungaji kiongozi Tumaini Shekhalage akisaidiwa na mchungaji Moses.

Ibada hiyo ya mwaka iliyopambwa na waimbaji wa Furaha kwaya ama kwaya kuu iliambatana na ibada ya chakula cha Bwana pamoja na neno la Mungu lililohuburiwa na mchungaji Tumaini aliyewakumbusha waumini waliohudhuria kanisani hapo kukumbuka kusamehe na kuachilia ili wapate kuendelea katika mambo yao kwakuwa chuki si nzuri ni kikwazo cha maendeleo lakini pia ni dhambi kwa Mungu.

Aidha mchungaji Tumaini aliwataka watu kukumbuka kushikilia vyema nafasi walizopewa ili waendelee kuishi kwa amani na maendeleo, akiwataka wenye ndoa kulinda ndoa zao, maboss makazini kulinda nafasi zao na sio kuzipoteza kwa makatibu mukhatasi wao pindi wanaporuhusu mambo mengine kufanyika na kujikuta heshima ya ubosi kupotea. Katika ibada hiyo pia mchungaji Tumaini aliwatambulisha watoto watakaoanza darasa la kipaimara kwa mwaka huu pamoja na kuwepo kwa ibada ya kumsimika askofu mkuu wa lutheran Uingereza itakayofanyika mji wa Liverpool nchini humo.

Ibada nyingine ya kiswahili inatarajiwa kufanyika tarehe 19 mwezi huu kuanzia saa nane mchana.



Mchungaji Tumaini akihubiri.




Baadhi ya waumini wakisikiliza ujumbe wa neno la Mungu.

Jumamosi, 4 Januari 2014

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU *sehemu ya pili*


Mtumishi Gasper Madumla.
"Naye Yesu aliposikia,alisema,Ugonjwa huu si wa mauti,bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu,ili Mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo." Yoh 11:4

Basi,nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo wa Nazareti aliye hai;
Bwana Yesu asifiwe...
Haleluya...

Neno linasema,"...Ugonjwa huu si wa mauti..."
Yamkini upo ugonjwa kwako,
Yamkini upo ugonjwa kwa mwanao,
Yamkini upo ugonjwa kwa mumeo/mkeo,
Yamkini mtu mmoja anaumwa hapa,
Ooh..Nasema Yamkini yapo mateso kwako,
Yawezekana una kisukari,
Yawezekana una presha,
Yawezekana una pumu,
Yawezekana una maralia isiyosikia dawa,
Yawezekana una uvimbe ndani yako.

Saa 8 mbinguni - Sehemu ya 2



Mchungaji Ricardo Cid
Ndugu msomaji wa blog hii, katika sehemu ya kwanza ya ushuhuda huu tuliona jinsi ambavyo Ricardo amechukuliwa na malaika wa Bwana kupelekwa mbinguni kukutana na Bwana Yesu. Walikuwa wamepita mbingu ya kwanza na wako kwenye mbingu ya pili. Wakati akiwa anaangalia shughuli mbalimbali za mapepo kwenye mbingu hiyo, kwa mbali aliona nyota yenye mwanga mkali ikiwajia pale. Je, hiyo ilikuwa ni nyota ya namna gani? Na je, nini kiliendelea baada ya hapo? Tafadhali karibu kwenye sehemu ya 2 na ya mwisho ya ushuhuda huu wenye ujumbe muhimu kwa Kanisa.

MKUMBUKE KATIKA MAOMBI MWIMBAJI HUYU WA NG'ANG'ANIA SHINYANGA


Getruda Ngassa akiimba na wenzake wa AIC Shinyanga walipokuwa mkoani Dodoma wakati wa Krismasi.
Hii ni kwa wote wakristo na wapenzi wa muziki wa injili, mkumbuke mama Getruda Ngassa mwimbaji nyota na solo wa kwaya maarufu ya AIC Shinyanga wana wa ng'ang'ania baraka za BWANA ambaye amelazwa katika hospitali ya Amana Ilala jijini Dar es salaam kutokana na tatizo la presha ya kushuka(Low Blood Pressure).

TAFSIRI YA NAMBA 14 KIMAANDIKO!


Pastor Peter Mitimingi, mkurugenzi Voice of Hope Ministry(VHM)

1. Namba 14 ni namba ya Wokovu na Ukombozi (Salvation ;Deliverance)
2. Mwaka 2014 ni mwaka wa Wokovu na Kufunguliwa.
3. Kulikuwa na Vizazi 14 kutoka Abraham mpaka Daudi
4. Kulikuwa na Vizazi 14 kutoka Daudi mpaka Utumwani Babeli.
5. Kulikuwa na vizazi 14 Kutoka Utumwani Babeli hadi Kristo.
Mathayo 1:1- 17

Alhamisi, 2 Januari 2014

MLIPUKO TENA ARUSHA, JESHI LA POLISI WATUHUMIWA,,WALENGWA NI KWAYA.

Polisi wa idara mbalimbali wakiwa eneo la tukio kwenye tukio la mlipuko wa bomu jijini Arusha mnamo mwezi Mei 2013. Picha zaidi za tukio hilo
Taarifa ambazo zimetufikia kupitia kituo cha WAPO Radio FM zinaeleza kwamba kuna bomu limelipuliwa kwenye kanisa katoliki la Mtakatifu Karoli, Ruanga huko USA River jijini Arusha, ambapo wanakwaya takriban 6 wamejeruhiwa.

Jumatano, 1 Januari 2014

TUNAJIFUNZA NINI KWA HABARI YA LAZARO ALIYEFUFULIWA NA BWANA YESU.


Mtumishi Gasper Madumla.
Bwana Yesu asifiwe....
Haleluya....

Kupitia Biblia maandiko matakatifu,wapo Lazaro wawili tuwasomao.
Lazaro wa kwanza ni yule aliyekuwa muombaji,mtu aliyekuwa akiwekwa mlangoni mwa tajiri mmoja,akishibishwa kwa makombo,mtu aliyekuwa maskini. (Luka 16:19-31).

Lazaro wa pili ndio yule ambaye alikuwa hawezi na baadaye akafa. Huyu alikuwa ni mkazi wa Bethania,mwenyeji wa mji wa Mariamu.Lazaro huyu alikuwa pia mfuasi wa Kristo Yesu,pia alikuwa rafiki wa Bwana Yesu Kristo.Kupitia habari za Lazaro huyu wa pili,ndio nataka tujifunze kidogo.

Wengi wetu tulishasoma habari zake Lazaro kipitia kitabu cha Yoh.11:1-44
Lakini si wote wenye kuelewa fundisho la Lazaro.
Lakini leo ipo Neema ya pekee mahali hapa ya kujifunza zaidi kwa habari hii.
Yapo mengi ya kujifunza kupitia habari ya Lazaro,nasi tutajifunza kwa kadri ya Roho apendavyo.

Biblia inatuambia yakwamba Lazaro alikuwa mkazi wa Bethania,ambapo neno
BETH ni neno lenye asiri ya kiebrania lenye maana NYUMBA(House)

Pia na neno,
..ANIA.. Ni neno lenye asiri ya kiebrania lenye maana YA KIMASKINI (of poor)
Hivyo ukiyaunganisha maneno haya,utapata hivi;
BETHANIA=Nyumba ya kimaskini(the house of poor)
Au ukanda wa kimaskini.

USHUHUDA WA NYISAKI



USHUHUDA WA MAONO YA JEHANAMU NA NYISAKI CHAULA

S.L.P. 2262

UYOLE – MBEYA

TANZANIA

YALIYOMO:

UTANGULIZI:

Sura ya 1: Kuitwa

Sura ya 2: Jehanamu sehemu ya kwanza na Mangojeo ya Wafu.

Sura ya 3: Jerusalem Mpya.

Sura ya 4: Mangojeo ya Jehanamu sehemu ya Pili
Unachotakiwa kufanya.

UTANGULIZI:
Ndugu yangu kuna shuhuda nyingi sana zinazoanguka duniani, lakini wachache wanaozingatia kwa vile watoaji si wa dini zao au si wa madhehebu yao wala hawajulikani makanisani. Sasa ninakuomba ewe msomaji, tafuta mahali pa utulivu, mwombe Mungu na kusoma ushuhuda huu ili upokee kile ambacho Bwana amekuletea leo.

Msichana Nyisaki Chaula alionyeshwa na Bwana ushuhuda huu akiwa na umri wa miaka 16 mara baada ya kuhitimu elimu ya msingi. Ushuhuda huu alionyeshwa akiwa ameokoka na si kwamba alikufa bali aliona maono. Maono haya alionyeshwa kati ya tarehe 30 – 31/12/1991; yaani kwa siku mbili tofauti.

Msichana huyu hivi sasa ameolewa na Mwinjilistii Lemsy Mheni pale Uyole Mbeya kwa lengo la kukuza huduma yao. Kabila lake ni Mkinga wa Makete, Msichana huyu anapatikana Uyole njia panda ya Malawi – Zambia na Dar es Salaam pembeni mwa kituo cha mafuta ya magari pale Uyole, Bwana awatangulie katika usomaji.

SURA YA 1

KUITWA: