Jumamosi, 25 Januari 2014

HARUSI YA KANA (wedding in Cana of Galilee) * sehemu ya 1 & 2 *

Na mtumishi Gasper Madumla.
“ Na siku ya tatu palikuwa na harusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.
Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.” Yoh.2:1-2
Nakusalimu mpendwa;
Bwana Yesu asifiwe…
Karibu tuendelee sasa;
KANA ni mji wa magharibi mwa ziwa Galilaya,mahali ambapo Bwana Yesu Kristo alifanya muujiza wake wa kwanza wa kubadili maji kuwa divai. Muujiza huu ulikuwa mkubwa sana maana Biblia inasema kupitia muujiza huo,Bwana Yesu akaudhihirisha UTUKUFU wake,
nao wanafunzi wake wakamuamini.
KANA ya Galilaya ndipo alikozaliwa Nathanieli,yule muisraeli safi kweli kweli,ingawa Nathanieli hapo awali alikuwa na wasi wasi kwa kwa habari ya Yesu kutoka Nazareti,naye akamuuliza Filipo ya kwamba neno jema ilitatoka Nazareti.?

Yoh.1:46
“Nathanaeli akamwambia, Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone.”
Alikadhalika ukisoma katika( Yoh.21:1-2,)utaona kwamba mahali ambapo Nathanieli alipozaliwa.

KANA ya Galilaya, ndipo mahali ambapo Bwana Yesu alipofanya muujiza wa pili baada ya kutoka uyahudini.
Muujiza huu wa pili ulikuwani uponyaji wa mtoto wa diwani mmoja wa Karpenaumu.(Yoh.4:46-50.)
Mji huu wa Kana ya Galilaya, haukutajwa katika agano la kale,ila umetajwa katika agano jipya.
Ulikuwa ni mji wa kawaida tu,lakini leo sio wa kawaida tena kwa sababu mji huu umekuwa sehemu ya maandiko matakatifu kwa kile tukisomacho.

Ninafahamu ya kwamba umeshawahi kualikwa harusini labda sio mara chache bali yawezekana umealikwa mara nyingi zaidi.Yeye anayealikwa harusini ni yule anayekuja kushuhudia kufungwa kwa ndoa na kusherekea pamoja na watu wote kwa furaha.
Mualikwa huwa sio muhusika mkuu harusini,
Mualikwa ni yule mwenye kupewa mualiko wa kuhudhulia arusini tu.
Yeye anayestahili kuingia arusini ni yule aliyealikwa tu.

Katika Yoh.2:1-2,(andiko la hapo juu),tunaona ya kwamba naye Yesu amealikwa tu harusini,Yeye pamoja na wanafunzi wake.
Yeye pomoja na wanafunzi wake walikidhi vigezo vya kuingia harusini maana wote walialikwa,hakuwapo hata mmoja aliyejichomeka ili aingie katika harusi hii,bali wote walialikwa.Biblia inatuambia kwamba naye mama yake Yesu alikuwa ndani ya harusi.

Bwana Yesu hakuenda harusini kwa ajili ya kufundisha kama desturi yake ya kufundisha huku na huko, wala hakuenda kwa dhumuni la kutoa mapepo.Bali alikwenda KUSHEREKEA nao washelekeao.
Ilikuwa ni harusi iliyofaana sana,maana baada ya kazi nzito ya Bwana Yesu ya kuchapa injili sasa hatimaye Bwana Yesu amekwenda kujipumzisha naye aweze kushuhudia harusi.

Sasa ona hapa;
“ Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.” Yoh.2:3

Wakati ilipokuwa harusi imenoga,gafla divai ikawatindikia,
KUTINDIKA maana yake kuisha,kukaukiwa,kupungua hadi mwisho.Ilikuwa sio mategemeo yao kutindikiwa na divai namna hii,maana kile walichokiamini ni kwamba divai iliyopigiwa bajeti itajitosheleza.
Ndiposa nikajifunza;

*KATIKA MAISHA YA MWANADAMU KUNA HALI YA KUTINDIKIWA.

Mwanadamu yeyote yule ni lazima atafika wakati wa kutindikiwa katika maisha yake aishiyo,haijalishi anaishi wapi,iwe ni Ulaya au Afrika,Lakini ni lazima apitie hali hiyo.Hali ya kutindikiwa huonesha kwamba mwanadamu hana uwezo wa kujiendesha yeye mwenyewe pasipo Yesu Kristo.

Haleluya…
Nasema;
Haleluya…

Nampenda mama yake Yesu namna anavyotufundisha siku ya leo,Biblia inasema pale walipotindikiwa tu,mama yake Yesu alimfuata Yesu Kristo wa Nazareti.Hii ikionesha na kutufundisha kwamba mama yake Yesu hana uwezo ule alionao Yesu.
Na ndio maana unaona mama huyu alimkimbilia Bwana Yesu,akitufundisha kwamba kila jambo lenye kutindika lipeleke kwa Bwana Yesu,nalo litatinduliwa tu…

HARUSI YA KANA (Wedding in Cana of Galilee)*sehemu ya pili*

Tumeona Bwana Yesu pamoja Na wanafunzi wake,na mama yake wakiwa wamealikwa harusini. Basi kumbe suala la kualikana kwenye maharusi halikuanzia hivi leo,
lilikuwepo hata enzi za Bwana Yesu,lakini suala la kuzamia katika harusi(yaani kwenda kwenye harusi pasipo kualikwa) hilo suala ndio jipya,ni la siku hizi ,
maana zamani huwezi "kuzamia" katika harusi,kwa kuwa tumeona Yesu mwenyewe pomoja na wanafunzi wake wakiwa wamealikwa.

Pale harusi hii ya Kana ya Galilaya ilipokuwa imenoga,gafla tunaona shida inajitokeza,shida ya kuishiwa divai.
Kwa taratibu za Wayahudi,DIVAI ilikuwa kinywaji muhimu sana pindi wafanyapo sherehe.
(Wine was the special pure juice from the grape,normally used in various Hebrew festivals)

Divai sio kileo,
Divai ilikuwa mojawapo ya kinywaji kilichoagizwa kitolewe mbele ya Walawi,(Walawi walikuwa ni watu maalumu waliotengwa kwa ajili ya kazi ya Bwana)Kumb.18:1-5.

Haleluya...

Sasa,
Tazama shida ya kutindikiwa kwa Divai ikijitokeza ndani ya harusi ya Kana.Tunasoma;
" Hata divai ilipowatindikia,mamaye Yesu akamwambia,Hawana divai" Yoh.2:3.

Mamaye Yesu anatufundisha kwamba ikiwa utatindikiwa kwa jambo lolote lile katika maisha yako,
Basi umkimbilie Bwana Yesu tu,Maana Yeye Yesu Kristo atayatindua yale yote yaliyotindika kwako.

Sasa sikia;
Mamaye Yesu hakumkimbilia
Simoni aitwaye Petro,
Wala hakumkimbilia Andrea,
Wala Yakobo wa Zebedayo,
Wala Yohana wa Zebedayo,
Wala Filipo,
Wala Barthomayo,
Wala Tomaso,
Wala Mathayo mtoza ushuru,
Wala Yakobo wa Alfayo,
Wala mama Yesu hakumkimbilia Thadayo;
Wala hukumkimbilia Simoni Mkananayo,
Wala mama huyu hakumuendea Yuda Iskariote,
Maana alijua hawa wote hawana UWEZA kama ule uliokuwa ndani ya Bwana Yesu,

BALI ALIMKIMBILIA YESU WA NAZARETI,akituonesha kwamba hiyo ndio njia ya kweli,maana hakuna aendaye kwa Baba pasipo njia hiyo (Yoh.14:6)-Yesu ndio njia,Kweli,na uzima.

Chakushangaza sasa;
shetani amepotosha fahamu za watu,hata watu kumgeukia mamaye Yesu na kumuomba,
wakati mamaye Yesu mwenyewe anatuonesha njia ya kuiendea na kuomba.
Shetani hana akili kabisa!

Funguka!
Ukaelewe hili,kwamba ni Yesu Kristo pekee anayestahili kuombwa na sio kumuomba mama yake,Mariamu,au mwingine awaye yote.
Mimi nashindwa kumuelewa mtu abadilishaye ukweli huu,maana hata mamaye Yesu mwenyewe ametuonesha yule astahiliye kuombwa,
• kwa nini basi umkimbilie mama yake Yesu,wakati Yesu mwenyewe yupo?

Haleluya..
Jina la Bwana lipewe sifa...

Tunasoma hapa tena,
"Yesu akamwambia, Mama,tuna nini mimi nawe?Saa yangu haijawadia." Yoh.2:4

Unaweza ukajiuliza hivi;
Sasa inakuwaje Bwana Yesu anamjibu mamaye hivyo?
Kwamba mama yake anamuomba jambo,lakini hatuoni Yesu akifanya muujiza pale pale alipoombwa,badala yake naye anamuuliza " tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia"

Hata mimi nilijiuliza hivyo,sijui wewe kama ulijiuliza.
Ndiposa nikagundua kwamba;

UPO WAKATI WA BWANA WA KUJIDHIHILISHA.
• Yaani upo wakati wa kudhihilisha nguvu ya Bwana Mungu.

Bwana ana muda wake wa kujidhihilisha,muda wa Mungu sio sawa na muda wa mwanadamu,vile tupangavyo sio sawa apangavyo Yeye Mungu. Ndio maana Yesu anamwambia mama yake " Saa yangu haijawadia"
Mara nyingi tunapenda Mungu atutendee mambo makubwa kwa muda na wakati tuliojipangia sisi wenyewe,
lakini ni tofauti na vile mungu atakavyo,tazama wale waliokuwa katika harusi ya Kana walitamani muujiza ufanyike muda ule ule,lakini Yesu anamjibu mama yake kwamba WAKATI WANGU BADO.

Ni mara ngapi tunaomba Mungu atutendee ili na lile,lakini kumbe wakati wake bado wa kudhilisha muujiza wake.Ndiposa nikatia akili na ufahamu niliposoma habari hii ya harusi ya Kana.

Kulikuwa na wakati ambao Wayahudi walikuwa wakitafuta kumuua Yesu huko uyahudini,ndugu zake Yesu Kristo wakamwendea Bwana Yesu na kumtaka aende uyahudini ili wanafunzi wakaone ishara na miujiza yake,lakini yeye akawajibu;

“ Maana hata nduguze hawakumwamini.
Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo.” Yoh.7:5-6

Yamkini wewe umekuwa kama mmoja wa ndugu yake Yesu unayetaka Bwana akujibu pale tu uombapo mbele zake,Au
Yamkini umeomba sana pasipo hata kujibiwa,mimi nami nakuambia usikome kuomba maana yawezekana wakati wa Bwana wa kujidhihilisha kwako bado haujafika,wewe endelea kuomba na wakati wa Bwana utakapowadia basi kila kitu kitakuwa sawa…

ITAENDELEA…

• Kwa huduma ya maombezi;
0655-111149.

UBARIKIWE.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni