Jumapili, 20 Aprili 2014

KANISA NI KUSANYIKO LA WAAMINI KATIKA BWANA,Na Oscar Samba

Ashukuriwe MUNGU muumba mbingu nchi an dunia kwa kutukutanisha tena siku hii ya leo katika blogu hii ya www.mwakasegeinjili.blogspot.com kwa ajili ya kusudi lake.
Jioni ya leo nakuletea mafundisho yaliyohubiriwa siku ya leo katika kanisa la VICTORY CHRISTIAN CENTRE T.A.G lilopo hapa mkoani Arusha eneo la Morombo.
Mwalimu ni Mch.Aloyce Mbughi.
Kanisani maana yake ni kusanyo la watu waliokoka ambapo huweza kuwa popote pale hata kama ni chini  ya mti.
Mimi na wewe ndio kanisa,wala si jengo,mchungaji Mbughi anaelezea jinsi alivyoanza kanisa katika wakati mgumu kwani alikuwa mwenyewe na wakati anaza huanza kwa ibada kama wako wengi kwani husema “ tuanze ibada,tusimame” huku akiwa mwenyewe.
Siku moja watu walikuwa wakimjadili ya kwamba “kuna kijana mmoja yuko pale kanisani (jengo la shule) na yuko kama kichaa,na ukimkuta njiani ni mzima ila akiingia pale anakuwa kama kichaa.
Siku nyingine wakina mama wakakubaliana waende kumsikiliza mtu huyu waliodai ya kuwa ni nusu kichaa,wakati akihubiri bila kujua kumbe nje kuna watu waliokuwa wakimsikiliza,siku hiyo alikuwa akihubiri juu ya Lazaro na yule tajiri.
Wakati wakuita watu na kuongoza sala ya toba  alikuwa akiongoza kwa kuacha nafasi mithili ya mtu akiwa akimfatisha wakati akiomba na kukemea vifungo vya shetani.
Mara akasikia kishindo cha mtu akianguaka,kumbe miongoni mwao mmoja wao pepeo lilimtoka,alilazimika kumkimbilia na kwenda kumuhudumia,hapo ndipo watu waliongozana nae na kuwahubria INJILII.
Siku hiyo aliongoza sala ya toba kwa watu watatu,ndipo alipoanza kufundisha somo ijpya la kukulia uokovu,kwa furaha watu walitangaziana ya kwamba “sio KICHAA alafu ni MCHUNGAJI”,siku ya ijumaa kanisa lilisheheni watu kama 20.
Siku hiyo alishuhudia nguvu za Mungu za ajabu,kwa muujiza baadae aliitwa kupewa kiwanja na serikali ya kijiji huko Kibaha eneo la Tumbi alipewa heka 3 kwa shlingi 80,000 ts/= .
Leo kanisa lile lina kiwanja  kikubwa mno na kumbuka lilianzia darasani na mtu mmoja yani mchungaji tuu.
Sasa fahamu mambo makuu 3 yalipasalo kanisa kufanya;
1.Kumfanyia MUNGU ibada.”Ndio maana jumappili,jumatano na ijumaa hukutana kwa ajili yakumwabudu yeye”,hata leo hapa kanisani katika siku hii ya PASAKA tupo kwa ajili ya kufanya hivyo nawe wakati huu unapo soma habari hii unaungana nasi katika kumuabudu yeye aliye mkuu.
2.Kumngoja BWANA,wakati tunamwabudu Bwana tunapaswa kuufahamu kanisa ya kwamba Yesu nakuja kulichukuwa kanisa ,soma zaidi 1petro 1:15,Yohana 14:1-6.Katika kungoja Bwana yatupasa kungoja katika hali ya utakatifu tukijua pale alipo yeye yatupasa nasi kuwepo,hapa duniani hata kama tusipo thaminiwa yatupasa kukumbuka ya kwamba pale aliopo ndipo tutakapo kuwepo nasi,kumbuka ya tupasa kumngoja.
3.KUTIMIZA AGIZO KUU,tunao wajibu wa kuabudu sawa,kumngoja katika hali ya utakatifu sawa,lakini pia yatupasa KUTIMIZA AGIZO KUU,Maana yake ni kupeleka habari njema kwa watu ambao hawajampokea YESU kama BWANA na mwokozi katika maisha yao.; mathayo 28:18-20 Yesu akaja kwao akisema kuwa nimepewa malaka yote duniania na mbinguni basi enendeni mkayafanye mataifa yote  kuwa wanafunzi mkiwabatiza kwa jina la Baba la Mwana na la Roho Mtakatifuna kuwaagiza kuyashika yote niliyo waamuru ninyi na tazamamimi nipo pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari.

Pia waweza kusoma katika kitabu cha Marko 16:15-16.Wakati kanisa linatimiza agizo kuu linamfanya MUNGU atembe nao kwa kiwango kikubwa “natazama mimi ni pamoja nayi siku zote hata ukamilifu wa dahari” kwa hiyo kwa kufanya hivyo MUNGU atakuwa nasi hadi mwisho; kwa mantiki hiyo tusipo fanya hivyo Mungu hawezi kutembea nasi kikamilifu.
 Uinjilisti umegawanyika katika  makundi makuu mawili ambapo la kwanza ni Uinjilisti wa mtu kwa mtu au nyumba kwa nyumba mara zote huwa ni Huduma kwa wote,huweza kufanyaka katika eneo lako la bishara,mashuleni au pale unapoishi kwenye basi au kwenye shuhuli mbalimbali.
Kama umekuwa haufanyi hivyo tafadhali fanya hivi sasa kwani Huduma hii ni ya umuhimu na usipofanya hivyo dhambi zao zitatakwa kwako,usikubali kuwaona watu wakiangamia katika dhambi ungali na uwezo wa  kuwasaidia wao kuondokana na dhambi zinazo wasonga.
Huduma hii haina Gharama wala haihitaji muda mwingi au maalumu kwani huweza kuifanya popote,tofauti na itakayofwata kwani hata wakati wakula chakula  au kupiga gumzo popote huweza kufanya hivyo.Katika hili hakuna “ubize” kwani hapo hapo ulipo wanadamu  unaoishinao hao hao waweza kuwahubiria INJILI.
Unaweza ukatumia mabango,”stika” ambazo zina ujumbe  wa MUNGU ambao kwanamna moja au nyingine huwa na nguvu ya uokovu.
Je! Ni watu wangapi hadi sasa ambao wamesimama katika safari ya imani  kutokana na injili uliyowahubiria? Ongera kama wako,ila kama hawako tafadhali anza leo nawe uliefanikiwa kufanya hivyo vyema endelea kufanya kazi hiii NJEMA kwani ipo taji yako.
Kuhubiri kumbuka hakuna ufundi hakiki hili kupitia kitabu cha  2wafalme 2:2-5 Ona binti huyu alivyo sema “laiti kamaa bwana wangu angalikwepo kule kwetu angalipona” Watu waliosikia hizi habari walitambua ya kwamba uwezekano wa kupona kwa shujaa wao upo.
Je! Wewe unashindwa kuwambia watu ya kwamba YESU akiingia ndani yako ulevi utakwisha au yakushinda kumweleza mlevi ya kwamba laiti kama ungalikwepo kwetu tuliokoka angali acha ulevi” hayo tuu yatosha kuubadilisha maisha ya mwenye dhambi.
Kile unachokijua kuhusu YESU kiseme YOHONA 4:28 Basi Yule mwanamke akauacha mtungi wake akaende mjini akawaambia watu njooni mumuone mtu aliyeniambia mambo yote niliyowahi kuyatenda Je1 hamkini huyu ndiye KRISTO.
Hii haikuhiitaji kozi wala ufundi. Tazama tena LUKA 8:38-93 Na mtu Yule aliyetokwa na pepo alimuomba ruhusa afwatanane nae lakini yeye akamwambia “rudi ukawaambie watu matendo makuu MUNGU  aliyokutendea” Mtu huyu alikuwa Ushuhuda mkubwa kwa watu wengi.
Kumbuka sehemu ya pili katika agizo kuu ni Huduma ambao mara nyingi hufanyika katika makutano makubwa ya watu au vyombo vya habari.

Kwa habari kama hii tafadhali endelea kutemelea hapa www.mwakasegeinjili.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni