
Mwimbaji nyota Emmy Kosgei wa nchini Kenya ambaye ameolewa na mtume Anselm Madubuko wa Nigeria, amekanusha vikali taarifa zilizotolewa na blog mbalimbali za nchini Kenya kwamba anadai talaka kutoka kwa mumewe ikiwa ndio kwanza miezi sita toka wafunge ndoa yao.

Emmy ni mmoja kati ya waimbaji nyota wa injili nchini Kenya ambaye toka ameanza kutoa album
zake za injili ambazo amekuwa akiimba sana lugha ya kwao pamoja na ubunifu wa mavazi yake na kundi lake zimekuwa zikipokelewa vyema na kumfanya apate mialiko mingi ndani na nje ya nchi yake ya Kenya.
Ambapo hivi majuzi ameachia video mpya katika album yake ijayo ikiwa kama utangulizi. Mdau wa GK kwa taarifa hii, si ya kusoma na kuiacha hewani cha muhimu ingia magotini umuinue mtumishi huyu wa Mungu aendelee kusimama katika ndoa yake na maneno yote yasemwayo juu yake basi shetani asijiinue na kuharibu huduma yake ambayo imefanyika baraka kwa wengi.

Emmy Kosgei siku ya harusi yake na mtume Madubuko wa Nigeria.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni