Jumamosi, 30 Novemba 2013

KWAYA YA KWETU PAZURI WAKO NCHINI ZAMBIA


Ambassadors of Christ wakiimba katika tamasha la pasaka jijini Mbeya mapema mwaka huu.

Kwaya ya Ambassadors of Christ kutoka Kigali nchini Rwanda maarufu kama Kwetu Pazuri wapo nchini Zambia kwa ziara ya siku tano ukiwa ni mwaliko wa kanisa la Wasabato Libala la jijini Lusaka ambapo kwaya hiyo itashiriki katika maonyesho makubwa matatu nchini humo yanayotarajiwa kuanza siku ya jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kundi hilo matamasha hayo ambayo yatakuwa na viingilio ili kusaidia ujenzi na huduma ya kanisa la Libala yatafanyika katika ukumbi wa Blessing centre kisha uwanja wa mpira wa Levy Mwanawasa uliopo Ndola na kumalizia katika ukumbi wa New Government complex siku ya tarehe 2. Kwaya hiyo ambayo ilipata umaarufu sana nchini Tanzania mwaka 2011 kutokana na album yao ya Kwetu pazuri, imekuwa ikipata mialiko katika nchi mbalimbali za Afrika ambako wameonyesha kiu ya kuwaona waimbaji hao.

Ambapo kwa mwaka huu Ambassadors walishiriki tamasha la pasaka nchini Tanzania, tamasha ambalo hata hivyo liliwaweka katika wakati mgumu na makanisa ya kisabato nchini kutokana na kukubali kushiriki tamasha hilo, lakini pia walikuwa nchini Uganda pamoja na Goma nchini Kongo ambako wameshiriki katika matamasha mbalimbali ya kusaidia huduma za makanisa ya Kisabato.



Uwanja wa Levy Mwanawasa ulipo Ndola nchini Zambia,ambapo Ambassadors of Christ wataimba siku ya jumapili.

Jumatano, 27 Novemba 2013

WACHAWI WADONDOKA MKUTANO WA GWAJIMA TANGA, MWINGINE AKAMATWA AKIMWAGA CHUMVI UWANJANI




Zikiwa zimepita siku nne tangu mkutano wa injili unaoendeshwa na kanisa la Ufufuo na uzima viwanja vya Tangamano jijini Tanga uanze, matukio mengi tayari yamekuwa yakitukia katika viwanja hivyo ikiwemo wachawi kudondoka wakati wa maombi, popo wasio na idadi kutimka majira ya saa 10 za jioni katia viwanja hivyo, pamoja na matukio ya watu kuja kumwaga chumvi viwanjani hapo.

Tukio la wachawi watatu kudondoka lilitokea juzi wakati mkutano huo ukiendelea ambapo mmoja wao ni mama mtu mzima huku wengine waliangukia walipokaa watu ambao walianza kuwapiga kabla hawajaokolewa na timu ya kanisa hilo ambao waliwachukua na kuwapandisha jukwaani kwa mahojiano huku watu wakipiga kelele za kuwataka washushwe ili wawaadhibu, lakini mchungaji Josephat Gwajima aliwaelewesha watu hao juu ya jambo walilokuwa wanataka kulifanya kwamba si jema zaidi ya kuwaombea ambapo maelfu hayo yalisikia sauti ya mchungaji Gwajima nakuwasamehe.

Matukio mengine uwanjani hapo ni watu wazima ambao walikamatwa majira ya mchana kwa nyakati tofauti, mmoja akiwa mwanamke alionekana akimwaga chumvi uwanjani hapo lakini alikamatwa akitaka kuelekea madhabahuni ambapo watumishi wa kanisa hilo walipokuwa wakianza kumhoji walitokea polisi ambao waliamua kumchukua kumfungulia mashtaka kituoni hata hivyo haikujulikana kama kweli alienda kufunguliwa mashitaka hayo.

Bibi aliyedondoka uwanjani hapo akiwa kwenye mambo yake ya ushirikina.

MAKALA: HUU MCHEZO UNA NIA GANI MBALI NA BURUDANI


© Desktop Nexus

Mara ya mwisho tuliona ni namna gani kuna ushabiki mkubwa hata kwa timu zinazojiita mashetani. Ninashukuru kwa wasomaji waliopata fursa ya kutuma maoni na kuelezea mtazamo wao kuhusiana na jambo hilo. Baadhi waliendelea kutoa mifano zaidi, wakifika hata kwa jogoo Liverpool, dragon wa Chelsea, majani ya Arsenal, na hata kufikia kwenye barcodes na noti tutumiazo, na kadha wa kadha, ilimradi kupinga ama kukubaliana na jambo hilo – kuwa shetani anatumia vema mambo ambayo tunayapenda kufanya shughuli yake. Hebu na tusalie kwenye mpira huu wa miguu, wengine huita kabumbu, gozi, ilimradi tu mbwembwe.

JE UNAFAHAMU UZURI WA MBINGUNI?


ZACHARY KAKOBE

Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        
Tovuti       : www.bishopzacharykakobe.org
Somo:   Je Unafahamu uzuri wa Mbinguni?
Mpendwa msomaji, pole sana na shughuli nyingi za kila siku.  Ninajua kwamba muda wako ni mchache sana, kutokana na shughuli zako nyingi.  Hata hivyo ninakuomba muda wako mfupi tu, ili tuzungumze juu ya jambo muhimu ambalo nimeona kwamba ni vema nikushirikishe.  Je umekubali ombi langu?  Natumaini umekubali.  Asante sana.  Basi ninakusihi tufuatane pamoja katika mazungumzo haya.
Mpendwa msomaji, huenda utakuwa umewasikia watu wengi wanaofiwa na ndugu, jamaa au marafiki zao wapendwa, wakisema, “Mungu waweke mahali pema peponi“.  Jambo hili linadhihirisha jinsi kila mmoja wetu anavyoamini kwamba kuna mahali pema peponi yaani mbinguni na tena inaonyesha jinsi sisi sote tunavyopenda kwenda huko, sisi na jamaa zetu.  Je wewe una shauku ya kwenda mahali pema peponi au mbinguni, baada ya kuiaga dunia hii?  Najua wewe pia una shauku ya kwenda mbinguni siku moja.  Hata hivyo, shauku yako itaongezeka zaidi utakapokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu uzuri wa mbinguni.  Peponi au mbinguni, ni wapi na kukoje?  Peponi au mbinguni, kuna uzuri usioweza kufananishwa.  Tukifahamu jinsi mbinguni kulivyo kuzuri, kila mmoja wetu atazidi kuwa na shauku ya kufika huko siku moja.  Mpendwa msomaji, tufuatane basi ili upate ufahamu wa kutosha kuhusu mbinguni au peponi.
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
     Peponi au mbinguni ni wapi na kukoje?
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 
Mbinguni au peponi, ni juu sana, mbingu ya tatu.  Biblia inasema katika 2 WAKORINTHO 12: 2-4,“Namjua mtu mmoja katika kristo,……Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu.  Nami namjua mtu huyo…….ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi………”   Mbingu ya tatu ni wapi?  Mbingu ya kwanza, ni hii iliyo na mawingu yanayoleta mvua, na mawingu mengine.  Ni anga hili lililo juu ambalo sehemu yake huonekana kwa macho ya kawaida.  Ndege au eropleni zote zinazobeba abiria, huruka katika mbingu hii ya kwanza.  Mbingu ya pilini  mbingu iliyo mbali zaidi yenye sayari na nyota zote. Sayari zilizoko katika mbingu ya pili ni pamoja na Zebaki, Zuhura, Mars, Mshtarii, Zahali, Uranus, Neptune, na Pluto.  Sayari nyingine ziko mbali sana.  Kwa mfano umbali wa dunia yetu kutoka kwenye jua ni maili 93 milioni (kilometa 148,800,000), lakini umbali wa sayari ya pluto kutoka kwenye jua ni maili 3,666 milioni (Karibu kilometa 5,900 milioni).  Nyota ziko nyingi sana, zinakisiwa kufikia 400 bilioni! Nyota ziko mbali sana na dunia yetu.  Nyota iliyo karibu zaidi na dunia, iko karibu maili 26,000 bilioni (karibu kilometa 42,000 bilioni).  Sasa basi, baada ya sayari zote hizi na nyota hizi, ndiyo tunafika mbingu ya tatu.  Mbingu ya tatu, au mbinguni, au Peponi, kwa msingi huu ni kilometa mabilioni kwa mabilioni kutoka hapa duniani.  Yesu kristo alipopokelewa na wingu, na kupaa kwenda juu mbinguni (MATENDO 1:9-11), alikwenda mbali sana kiasi hiki.  Huko ndiko waliko watakatifu waliotutangulia.
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .  Mbinguni au peponi, ni kilometa mabilioni kwa mabilioni kutoka hapa duniani
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Tupige hatua tena na kuangalia mambo mengine.  Sasa je, mtu anapokufa, anasafirije kwenda mbinguni, mbali kiasi hiki?  Hatupaswi kuogopa kifo, ikiwa tunaishi maisha yaliyo mbali na dhambi.  Biblia inasema katika ZABURI 116:15Ina thamani machoni pa Bwana, mauti ya wacha Mungu wake.  Kufa kwa watakatifu ni faida (WAFILIPI 1:21).  Ni heri kwa wafu wafao katika Bwana (UFUNUOWA YOHANA 14:13).  Kufa kwa mtu anayeishi maisha yaliyo mbali na dhambi, ni mwanzo tu wa utukufu.  Mtu anayeishi maisha mbali na dhambi, anapokufa, roho yake humiminwa katika mwili mwingine wa roho unaitwa mwili wa mbinguni, kama mafuta yaliyo katika chombo kibovu kinachovuja, yanavyoweza kumiminwa katika chombo kingine kilicho kizuri.  Kufa ni kumiminwa!  Mtume Paulo aliyepata neema ya kuchukuliwa na kupelekwa mpaka mbingu ya tatu wakati wa uhai wake (2 WAKORINTHO 12:2-4), ulipofika wakati wa kufariki kwake, alijua ni wakati mzuri wa kumiminwa.  Kwa maneno yake, katika 2 TIMOTHEO 4:6, alisema, Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
Kuhusu miili ya mbinguni, Biblia inasema katika 1 WAKORINTHO 15:40-41, 44Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani, lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.  Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota……Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.  Miili hii tuliyo nayo ni mibaya sana.  Ni kama vyombo vibovu. Fahari yake, yaani uzuri wa ile miili ya mbinguni ni zaidi sana kuliko miili hii tuliyo nayo.  Miili ya mbinguni inang`aa mno na kupendeza sana.  Mtu huwa na mwili mzuri zaidi ya ule wa malaika! Mtakatifu anapokata roho, roho yake mara moja humiminwa katika mwili mzuri wa jinsi hii.   Mtu akiwa katika mwili wa mbinguni, atapenda kujitazama wakati wote.  Mwili huu hauna makovu wala ulema wala hauna makunyanzi ya uzee!  Baada ya mtu kuwa na mwili mzuri wa jinsi hii, huvikwa mavazi mazuri meupe sana yanayometameta sana.  Weupe wa mavazi haya, ni weupe usio na mfano duniani (UFUNUO WA YOHANA 3:4-5;  UFUNUO WA YOHANA 7:9;  MARKO 9:2-3).   Baada ya kuvikwa mavazi haya, mtu hufunguliwa mlango wa gari na malaika, na kuingizwa katika gari zuri sana lisilokuwa na mfano duniani. Yako mabilioni ya magari ya Mungu, yanayowasubiri watakatifu.  Biblia inasema katika ZABURI 68:17Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu.  Mtu huchukuliwa na malaika katika magari haya yanayoitwa magari ya moto, yanayoambatana na farasi wa moto na kuchukuliwa kwenda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli (LUKA 16:22;  2 WAFALME 2:11).
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
Mtu hufunguliwa mlango wa gari na malaika, na kuingizwa katika gari zuri sana

Jumapili, 24 Novemba 2013

VIWANJA VYA TANGAMANO JIJINI TANGA VYAANDIKA HISTORIA MPYA

Ikiwa ni siku ya kwanza ya mkutano wa kanisa la Ufufuo na uzima linaloongozwa na mchungaji Josephat Gwajima unaofanyika mjini Tanga maelfu ya watu wamejitokeza katika mkutano huo na kusababisha uwanja wa Tangamano ambapo mkutano unafanyika kutokutosha maelfu ya watu hao.


Mchungaji Josephat Gwajima akifundisha katika mkutano mjini Tanga









Maelfu ya wakazi wa mji wa Tanga wakimshangilia Mungu wakati wakisimsikiliza Mchungaji Josephat Gwajima leo




Mchungaji Gwajima akihubiri mjini Tanga 


Jackson Bent akimuimbia Mungu katika mkutano wa Ufufuo na Uzima jijini Arusha

ISHARA ZA ZAMANI HIZI

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : http://www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : http://www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : http://www.youtube.com/user/bishopkakobe
SIKU YA KUICHAMBUA BIBLIA

SOMO: ISHARA ZA ZAMANI HIZI (MATHAYO 16:1-4)
Katika MATHAYO 16:1-4, tunaona Yesu akizungumza juu ya watu ambao ni mabingwa wa kutambua majira ya mvua kwa kuangalia ishara za kutanda mawingu, au ishara nyinginezo na kufanya maandalizi mapema ya kuanua nguo zilizowekwa nje au kuuingiza ndani unga uliotandazwa nje kwenye jamvi au mkeka ili ukauke n.k.; lakini hawajui kuzitambua ishara za majira waliyo nayo, na kufanya maandalizi ya kujikinga na madhara yatakayowapata. Ujumbe huu ni hai kabisa kwetu

AMRI KUU

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SIKU YA KUICHAMBUA BIBLIA

SOMO: AMRI MPYA


L


eo, tena, Bwana ametupa neema ya kuendelea kujifunza Kitabu cha YOHANA, katika Biblia zetu. Leo, tutatafakari YOHANA 13:33-38, na YOHANA 14:1-3. Katika mistari hii, pamoja na mambo mengine, tutajifunza kuhusu “AMRI MPYA“. Tutayagawa mafundisho tunayoyapata katika mistari hii katika vipengele tisa:-

(1) ENYI WATOTO WADOGO (MST. 33);

BWANA NDIE JIBU,MTATUAJI WA KILA AINA YA TATIZO * sehemu ya mwisho *


Mtumishi Gasper Madumla.
Haleluya...
Bwana Yesu asifiwe...

Siku ya leo,Bwana Mungu akuhudumie kwa namna ya tofauti tunapomalizia hii tafakari.

Kumbuka, tulikuwa tumekwamia kuchimba kiundani katika tafakari,

Tukijifunza juu ya njia moja ya kwanza ya kupokea muujiza/jibu lako kutoka kwa mwenye majibu ambaye ndie wa milele,

Ni Bwana wa mabwana,
Mfalme wa wafalme,
Mungu mwenyezi,
JEHOVA aliyekuwepo,aliyepo na atakayekuwapo milele na milele.

Tulijifunza njia moja ya kupokea jibu lako nayo hiyo njia nilikuamba ni kujisalimisha kwake BWANA.

Leo tunajifunza njia nyingine ya kupokea jibu lako.
Kumbuka kwamba,
Kila jibu juu ya swali ulilonalo lipo kwa BWANA.

Labda kabla hatujaangalia njia nyingine itupasayo kupokea majibu kutoka kwa Bwana,
Niseme hivi;

Katika njia hiyo ya kujisalimisha kwa Bwana,ipo gharama ikupasayo kuilipa.

Gharama yenyewe ni ya kuidharau aibu.

Aibu ni gharama,
Aibu hutesa maisha yetu,
Wengi,hatupokei kwa sababu ya kuwa na AIBU.

Mungu leo atusaidie sana tuweze kuidharau aibu.

Ili ujifichue na umfuate Bwana Yesu,lazima ukubali kuacha yote.

Tazama sasa;
jamii inayokuzunguka itakusema vibaya,kwa sababu ya kumfuata Bwana Yesu.

Kujisalimisha kwa Bwana Yesu ni kuokoka.

*kuokoka ni kukutana na Yesu.

MCHUNGAJI IMELDA KISSAVA WA K.K.K.T DAYOSISI YA IRINGA AFARIKI DUNIA



 MAZIKO  YAKE YATAFANYIKA SIKU YA JUMATATU  25.11.2013 KATKA USAHARIKA WA KIHESA IRINGA MJINI
Taarfifa kwa mujibu wa Sadataley.blogspot.com
www.mwakasegebibilia.blogspot.com

Jumamosi, 16 Novemba 2013

HABARI PICHA: APOSTLE NDEGI AHITIMISHA SEMINA ST AUGUSTINE MWANZA


Jiji la Mwanza limepata Neema ya Injili, ambapo wanachuo wa chuo kikuu cha Mtakatifu Agustino wamepata fursa ya kufundishwa na kuhubiriwa kuhusu njia ile nyembamba iendayo Mbinguni, ambapo apostle Ndegi wa kanisa la Living Water amekuwa huko kwa takriban wiki nzima.

Nasema ni Neema kwa kuwa kwenye miji ambapo wanachuo wanakuwepo, huwa kuna kila aina ya tabia, na kama zisipoangaliwa, nyingine huwa ni hatarishi kwa namna nyingi tu. Basi tazama hitimisho la semina hiyo kama ambavyo picha zimeletwa kwenu kwa hisani ya Tunu Bashemela.

BWANA NDIE JIBU,MTATUAJI WA KILA AINA YA TATIZO.*sehemu ya nne *


Mtumishi Gasper Madumla.
Tunasoma;
"Katika shida yangu nalimwita BWANA;
BWANA akanijibu akaniweka panapo nafasi."
Zab 118:5,
(Andiko la kusimamia fundisho hili)

Alhamisi, 14 Novemba 2013

BWANA NDIE JIBU,MTATUAJI WA KILA AINA YA TATIZO.* sehemu ya tatu *


Mtumishi Gasper Madumla
Tunasoma,;

"Katika shida yangu nalimwita BWANA;
BWANA akanijibu akaniweka panapo nafasi." Zab 118:5
Andiko hilo ni andiko letu la kusimamia fundisho hili.

Haleluya…
Nasema Bwana Yesu asifiwe…
Jina la Bwana libarikiwe.

Bwana ana majibu yako juu ya tatizo ulilonalo.Shida haiko kwa Bwana bali shida iko kwako wewe mwenyewe jinsi umuendeavyo Bwana.
Majibu yapo tayari kwa ajili yako,
Nafasi ipo tayari kwa ajili yako,Ila ni wewe mwenyewe unajichelewesha kupokea,sababu ya njia unayoitumia.

BABA WA GWIJI LA MUZIKI WA GOSPEL DUNIANI AFARIKI DUNIA


Donnie McClurkin.
Baba mzazi wa gwiji la muziki wa injili duniani Donnie McClurkin's aitwaye Donald Andy McClurkin amefariki dunia hapo jana majira ya saa 10 alfajiri kwasaa za Marekani. Mzee huyo amefariki dunia ikiwa ni wiki moja tangu alazwe kutokana na kufanyiwa upasuaji wa dharura katika hospitali ya Palmetta Baptist Medical iliyoko kaskazini mwa mji wa Carolina.

Jumanne, 12 Novemba 2013

MAKALA: KUMBE SHETANI NAE ANA MASHABIKI WA KUTOSHA


©Desktop Nexus
Weekend hii ilikuwa njema na chungu kwa baadhi ya wadau wa soka. Nazungumza hivyo nikitazama matokeo ya mechi la ligi kuu kadhaa kuanzia ya nyumbani ambayo pazia la msimu wa kwanza limehitimishwa, huku pia kwa Uingereza, ligi yenye wadau wengi duniani - ikikutanisha Manchester United na Arsenal, ambapo matokeo, ni ushindi kwa Man U, goli moja kwa bila. Si nia yangu kujadili matokeo wala kuwakumbusha baadhi ya watu machungu, nia haswa ni kutazama ushabiki wetu na majina ya hizi timu.

Jumatatu, 11 Novemba 2013

PRAISE POWER WAONYESHA MFANO WA DINI ILIYO BORA


Baadhi ya mali ambazo zimekabidhiwa kijiji cha wazee, Msimbazi jijini Dar es Salaam.


Wikiendi hii kuna mengi yametokea, mazuri kwa mabaya ndani yake humohumo. Kati ya zuri mojawapo, ni kitendo cha baadhi ya wafanyakazi wa kituo cha Redio cha Praise Power Radio kutembelea kambi ya wazee eneo la Msimbazi, jijini Dar es Salaam, na kuwapatia misaada mbalimbali kwa kadri ya uwezo wao.


Tukio hili ambalo hakika likanikumbusha kuwa kila mtu atazeeka (Kwa Neema), basi likanipa faraja nikijitazama miaka 97 ijayo, na kuona kundi la watu wakitia kambi ghafla kwenye makazi yangu kunipa maneno ya faraja na zawadi mbalimbali, inapendeza.


Gospel Kitaa ambayo ilishuhudia tukio hilo, ilipata fursa ya kumhoji meneja wa Praise Power, Bwana George Mpella, ambaye anasema kuwa msukumo wa kufanya jambo hilo unatokana na kituo chao cha Redio, yaani Faraja ya Watu , kwa hiyo licha ya kuwashauri watu kiimani zaidi, pia mwisho wa siku ni muhimu kufanya kitu kama hiki kimwili.

Kuna kinamama wana matatizo ya fistula, wakatengwa na jamii na kuna watoto wana matatizo ya kuwa na vichwa vikubwa - hawa wote wamekuwa wakipata misaada kwa namna mbalimbali, lakini ukiangalia wazee - hili ni kundi la watu waliosahaulika, ndio maana Praise Power Radio - Faraja ya Watu ikafanya jambo hilo, baada ya kufanya utafiti kujua hasa wazee hao wana uhitaji wa aina gani.

Baada ya kufanya hapa, wiki hii wanaendelea - na hapa ni kwa ajili ya wahanga wa kiafya, yaani wale waliojifungua kwa matatizo kwenye hospitali ya CCRBT. Japo hawana pesa nyingi

Mwisho wa yote Bwana Mpella anaiasa jamii ijifunze kukumbuka wasiojiweza, "sisi sote ni vijana, ila mwisho wa yote nasi tutafikia umri huo - hivyo ni vema kujifunza ni mambo gani unaweza kukutana nayo." anamaliza kusema George Mpella.


Tazama baadhi ya picha za tukio hilo kama ambavyo lilitokea.



Muimbaji Mess Jacob Chengula wa katikati akiwa na George Mpella pamoja na mtangazaji wa ppr John Kisaka





wadau mbalimbali wakifuatilia tukio hilo







Muimbaji Mess Jacob Chengula akiongoza kuimba



Maombi yalikuwa sehemu mojawapo ya siku hiyo muhimu.





Hapo kale, bibi huyu alikuwa binti, kama ulivyo mdada wewe.



Muda wa kujenga mwili ulikuwepo











Waandishi kazini, Boniphace Magupa akiwahoji wazee







Mratibu wa tukio hili, Bwana Mahunja akinena jambo wakati wa ukabidhi wa zawadi mbalimbali












Furaha katika picha ya pamoja



Mwakilishi wa GK, Silas Mbise akiwa pamoja na wadau.

MUNGU BADO ANATENDA, SOMA SHUHUDA HIZI ZA KUTISHA

Soma shuhuda mbalimbali kutoka matawi ya kanisa la Ufufuo na Uzima nchini. kama zilivyotolewa katika mitandao ya kijamii ya kanisa hilo.


Ushanga aliokuwa nao mtoto huyo.
Yakikasirika majeshi, kuzimu lazima itapike watu wa Mungu iliyowameza, Ni mtoto wa miaka 11 kama uonavyo pichani alifungishwa ndoa na kuzimu na kuzaa watoto 4, Unaweza kuona ni jinsi gani shetani asivyokuwa na aibu, Bibi mzaa baba ndo alifanikisha ndoa hiyo kwa kumkabidhi mjukuu wake, pichani, pete na hereni hizo ambazo zilikuwa ndio muunganisho baina ya kijana Hussein ambaye alikuwa mume wa kijini wa binti IVONNE. Alipoletwa katika bonde la kukata maneno la Ufufuo na Uzima kwa ajili ya maombezi, Maneno yote yakakatika.



Mchungaji Kiongozi wa kanisa la Ufufuo Arusha Frank Andrew kushoto akionyesha pete aliyokuwa nayo mtoto huyo.

TUKIO LA AJABU TANGAMkuu wa TANGA etekwa..

Tukiwa Mjini Tanga Leo, tukiupeleleza mji Na Mkuu wa Operation ya Saa ya Ufufuo Na Uzima, kamanda kamili wa Jeshi la Bwana, Baba yetu Josephat Gwajima, nyayo zetu zikakanyaga uwanja wa TANGAMANO ambao ndipo Mkutano Utapokitwa, kuanzia jumapili ya tarehe 24 mwezi huu, tukaona tukio la ajabu. Baada ya kuingia tu hapo uwanjani tukiwa tumepaki Gari mbali na wakaazi wengi wa mji wakifanya shughuli zao za maisha maeneo hayo, tukamwona Kijana mmoja anaelekea maeneo tuliyowaza kuweka madhabahu. Akavua nguo. Akawa Kama anabishana Na watu tusiowaona. Baba akamwendea akamuuliza unafanya nini, kijana akatoa macho Kwa hofu akijitetea, "Mzee, Mzee sio Mimi ni walee wanakimbia, mie nimekuja kujisaidia tu, Niambie nikawakamate niwalete" baba akamwambia kawalete.. Akavaa suruale Na kuondoka, hatukumfuatilia ila mara akarudi tena, Hadi tulipo Na kuanza kulalamika mwenyewe "huu uwanja ni wangu, ni wa urithi, mie siwapi ng'o " baba akamkazia macho, akaondoka akipiga kelele "Eee Mola, Walah Inshallah!, nipunguzie adhabu ya Moto wa Jehanam Kwa Sababu nimewaona Wakristo" Tulishangaa sana, amejuaje sisi ni Wakristo, uwanja Wa serikali huyu anasema ni urithi wake. Na wale aliokuwa anaongea nao ni kina nani..ni Viumbe vya Kiroho, vinajua Tanga Sasa inakwenda kutekwa. Mkutano wa Tanga utakuwa Mkubwa sana.





Mchungaji Josephat Gwajima alipotembelea Tanga hivi karibuni.
Maria John arudishwa kutoka chini ya maji ziwani Tanganyika!!