Jumapili, 16 Machi 2014

SOMO : MAONO NA NDOTO * sehemu ya nne na ya tano*

Mtumishi Gasper Madumla.
Bwana Yesu apewe sifa...
Nakusalimu mpendwa katika jina la Bwana,nikisema;
Haleluya...
Leo ni siku ya nne ya fundisho hili mahali hapa.Wengi waliokuwa wakifuatilia fundisho hili kwa njia ya mtandao wanasema;
wamebarikiwa sana na wamepokea mafunuo mengi kupitia fundisho hili.
Kumbuka;
Tulikuwa tukijifunza namna ya maono yanavyoweza kukamilishwa.Tukaangalia njia mbili ambazo MAONO hukamilika,njia hizo ni njia ambazo maono yanaweza kupitia,nazo ni;

a)Maono kwa njia ya macho ya wazi wazi.
b)Maono kwa njia ya usingizi./Kuzimia kwa roho.
(Fuatilia sehemu zilizopita,ili uelewe vizuri mahali tulipotoka)

Haleluya...
Sasa tunaendelea;

Biblia inasema;

" Nalikuwa katika Roho,siku ya Bwana;nikasikia sauti kuu nyuma yangu,kama sauti ya baragumu," Yohana 1:10

Katika andiko hilo,tunaposoma ya kwamba "nikasikia.....sauti kama ya baragumu"
lile neno " nikasikia..."
lina maanisha kwamba,
masikio ya rohoni ndio yalisikia ile sauti iliyo kama ya baragumu kwa sababu Yohana alikuwa katika roho.

Kwa lugha nyingine Yohana hakusikia ile sauti kwa masikio yake ya damu na nyama,Bali alisikia kwa masikio ya rohoni. Hivyo basi ikiwa Yohana alipata kusikia sauti pindi alipokuwa rohoni,basi;inaonesha yapo masikio ya rohoni yenye kusikia sauti ya BWANA MUNGU.

Yohana ilipokuwa akiyapata maono hayo alikuwa kama mtu aliyekufa (Yohana 1:17). Ndio maana maono haya hujulikana kama maono kwa njia ya usingizi.

Haleluya...

Sasa unisikilize tena;
Tumeaona watu waliopata maono makubwa kama akina Yohana,Musa,akina Ezekieli,pamoja na Samueli,pamoja na Petro,pamoja na Kornelio,N.K ;
hao wote wakiwa wamepata maono kwa njia ya usingizi/kuzimia kwa roho au kwa njia ya macho ya wazi wazi kama tulivyojifunza hapo awali.

Watu hao waliopata maono,walikuwa ni watu wa rohoni. Watu wenye kubeba kusudi la Mungu. Nasi leo hii tukitaka kuwa na MAONO makubwa kama hayo ni lazima tuwe watu wa rohoni kweli kweli.

Mungu huzungumza nasi kwa njia nyingi,na kwa njia tofauti tofauti; miongoni mwa njia hizo ni njia ya MAONO.Shida moja tuliyokuwa nayo leo ni kukosa MAONO. Ikiwa tunakosa maono,



Basi ipo shida ndani yetu.
Si kana kwamba Mungu hasemi nasi siku za leo,Au
Si kana kwamba Mungu hakuachilia nguvu ya maono kwa watu wake,Bali maono yamekwisha achiliwa (Matendo 1:17) lakini shida tuliyonayo sisi ni MIKAO yetu tuliyokaa ndani ya maisha ya ukristo,mikao yetu hayampendezi BWANA MUNGU.

Sasa,
Ikiwa kama tunataka kuwa na maono makubwa kama waliyoyaona watu wa Mungu wa kipindi kile,basi ni lazima tubadili mikao yetu mbele za BWANA MUNGU.Mikao yetu ya kubadili ni kukubali kutoka rohoni kuishi maisha ya utakatifu na kuzichukia dhambi zote.

Sikia;

Watumishi wa Mungu wa kipindi kile walikuwa hawafanyi jambo lolote pasipo kuoneshwa katika MAONO. Watumishi wa Mungu walihitaji kupewa ufafanuzi na maelekezo juu ya kazi waliyoitiwa,mfano;
Musa alipopata maono ( Kutoka 3:1-3) pale alipotumwa aende kwa Farao.

Musa alihitaji kujua maelezo sahihi,namna ya kuanza na kumaliza kazi aliyopewa na BWANA MUNGU,ndio maana Mungu anaanza kumuelekeza ya kwamba yeye ni Mungu wa namna gani aliyemtokea,anaanza kumwambia ya kwambaYeye Mungu anaitwa nani/jina lake Mungu ni lipi,kisha anamtuma.

Hayo yalikuwa maelezo muhimu sana kwa Musa.Pia watu wa Mungu walikuwa wakihitaji kuona MAONO juu ya kazi yoyote ile waliyopewa na Bwana Mungu.
Walikuwa hawaendi kuifanya kazi ya Mungu kwa shauli lao.

Leo,watumishi wamekosa MAONO,Bwana Mungu hakujifunua kwao,kwa sababu ya maisha yao ya dhambi,na wengi huenda kwa kutumia akili zao,na ndio maana huduma inakuwa ngumu sana sababu MAONO hakuna.

Bwana Yesu asifiwe...

Ni maombi yangu,ya kwamba Mungu akaturehemu sisi watumishi wa Mungu wa Tanzania ili tuweze kupata MAONO juu ya huduma tuzifanyazo.

Haleluya...

Nasema;
Maono tuliyojifunza,ni maono kama ishara ya picha. Tafsiri hiyo ya maono kama ishara ya picha ni moja ya tafsiri kubwa sana ambayo waandishi hata walimu wengi hawaielezei kiundani kama sisi tulivyojifunza takribani siku nne mfululizo.

Sasa ;
Imefika wakati wa kukupa tafsiri nyingine ya Maono. Ninaomba uwe makini kabisa kunifuta,ili uelewe vizuri.

Naanza hivi;

Kila mwanadamu aliyeumbwa,aliumbwa kwa maana na kusudi kamili la BWANA MUNGU mwenyewe. Mwanadamu hakuumbwa kwa hasara. Ndio maana Mungu alipomuumba mwanadamu na vitu vingine akaona ya kuwa ni vjema. (Mwanzo 1:31)

Na ikumbukwe ya kwamba, Mungu alihakikisha anamuwekea mwanadamu kila kitu tayari ili mwanadamu aje afanye kazi ya kuvitawala vile vilivyoumbwa…




MAONO NA NDOTO * sehemu ya tano *

Bwana Yesu asifiwe...
Haleluya...

Tunasoma;
" Itakuwa siku za mwisho,asema Mungu,nitawamwagia watu wote Roho yangu,na wana wenu na binti zenu watatabiri;na vijana wenu wataona maono;na wazee wenu wataota ndoto." Matendo 2:17

Haleluya....
Jina la Bwana libarikiwe....

Andiko tulilolisoma hapo juu,ndilo andiko letu la kusimamia fundisho letu zuri. Kupitia andiko hilo,tulijifunza kuhusu KUTABIRI kwa mujibu wa maandiko matakatifu na tukaangalia mifano ya watu waliopata kutabiri,kisha tukajifunza kuhusu MAONO.

Leo ni siku ya tano tukijifunza juu ya MAONO.Tulijifunza kuhusu maono kama ishara ya picha halisi juu ya tukio lijalo lenye kuonekana katika ulimwengu wa kiroho,tukaenda kiundani sana kuangalia na aina za maono,pamoja na mifano yake( Fuatilia sehemu zilizopita)

Leo tunajifunza kuhusu maono kwa mtizamo mwingine.
Kumbuka;
Nilikuwaambia kwamba,kila mwanadamu chini ya jua ameumbwa kwa maana na kusudi maalumu la Mungu mwenyewe. Nikakuambia ya kwamba,hakuna mwanadamu aliyeumbwa kwa bahati mbaya.

Haijalishi wewe ni mkristo au si mkristo lakini ujue ya kwamba hukuumbwa kwa bahati mbaya.Mungu anakuhitaji akuokoe kwa wokovu ulio mkuu kupitia jina la Yesu Kristo wa Nazareti.
Hivyo basi kama hukuumbwa kwa bahati mbaya ,basi uliumbwa kwa bahati nzuri ya kuyafanya mapenzi ya Baba wa mbinguni.

Ikiwa ni hivyo basi,
Tafsiri nyingine ya MAONO ni ipi?

MAONO ni ufumbuzi wa kusudi la Mungu na mpango wa Mungu ndani ya maisha yako.

Haleluya...

Nasema MAONO ni ufumbuzi wa mpango na malengo ya Mungu ndani ya maisha yako,
Au,
Kwa lugha nyingine mmoja anaweza sema MAONO ni Kusudi la ki-Mungu uliloumbiwa. Yaani ni kwa nini uliumbwa mwanadamu,ile sababu iliyokufanya uumbwe hivyo ulivyo wewe mwanadamu,sababu hiyo ndio inaitwa MAONO.

Bwana Yesu asifiwe...

Kama ningekuwa nakufundisha kwa lugha ya kiingereza ningekuambia;
VISION is the discovery of divine purpose and plan in your life.

Dhumuni kubwa la kuumbwa mwanadamu ni kumuakilisha BWANA MUNGU hapa duniani. Katika kumuakilisha BWANA MUNGU hapa chini ya jua,ndio namna ya kuyafanya mapenzi yake katika DHUMUNI na LENGO fulani la Mungu mwenyewe.

Hilo dhumuni na lengo fulani lililofichika ndilo huitwa MAONO au VISION.
Mfano;
BWANA MUNGU anataburisha dhumuni la kumuumba Yeremia akisema;

" Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua,na kabla hujatoka tumboni,nalikutakasa;nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. " Yeremia 1:5

Bwana Mungu anaelezea dhumuni na lengo kamili la kuumbwa kwa Yeremia,kwamba Yeremia aliumbwa ili awe nabii wa mataifa.

Lile dhumuni la kutengwa kwa Yeremia,awe nabii ndio MAONO.
Maono hayo yalikuwa katika hali ya kufichika,kwamba hakuna mwanadamu mwenye kuyajua hayo,isipokuwa ni Mungu pekee ndiye aliyekuwa akijua MAONO ya kuumbwa kwa Yeremia.

Haleluya...

Hata wewe,kabla hujaumbwa katika tumbo la mama yako,BWANA alikujua,alikutakasa,na alikutenga kuwa mtu fulani katika kazi yake Mungu hapa chini ya jua. Hiyo " kazi fulani ya Mungu hapa chini ya jua uliyoumbiwa..." Ndio hujulikana kama MAONO.

Mungu alikujua kabla hujaumbwa tumboni,na pia alikutakasa,na zaidi ya yote ulitengwa kwa kazi ya Bwana.
Ngoja nikupe mfano mwingine hapo;
BWANA MUNGU anatambulisha pia dhumuni la kumuumba Yohana mbatizaji.

Tunasoma;
" Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana;hatakunywa divai wala kileo;naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye. Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao."Luka 1: 15-16

Bwana Mungu anazidi kutuelezea dhumuni na lengo la kumuumba Yohana mbatizaji. Anasema Yohona alikusudiwa kuwalejeza wengi katika Waisraeli,kuwalejeza kwa Bwana Mungu wao kwa njia ya toba ya ubatizo wa maji.Yohana ndiye aliyepewa kusudi la kutengeneza njia ya Bwana Yesu.

Haleluya..

Maono ni ufumbuzi wa kazi ya ki-Mungu ndani ya maisha ya mtu.

Ngoja niendelee kukupa mifano zaidi kuhusu maono katika mtazamo huu wa pili.
Bwana Mungu anazidi kutueleza kusudi la uumbaji kwa watu wake. Na hapa anatueleza kusudi na lengo maalumu la kumuumba Sauli,

Tunasoma;
" Kesho wakati kama huu,nitakuletea mtu kutoka nchi ya Benyamini,nawe mtie mafuta ili awe mkuu juu ya watu wangu Israeli,naye atawaokoa watu wangu na mikono ya Wafilisti;maana nimewaangalia watu wangu,kwa sababu kilio chao kimenifikilia."1 Samweli 9:16.

Maono ya kuumbwa kwa Sauli,yalikuwa ni kuwaokoa wana wa Israeli kutoka katika mikono ya Wafilisti,maana kilio chao kilimfikilia Bwana Mungu.

Sauli hakuwa na maono ya ubatizaji,Bali maono ya kuwaokoa Waisraeli kutoka kwa Wafilisti.

Alikadhalika tunaona dhumuni na kusudi la kuumbwa kwa mtume Paulo,Paulo hakuumbwa awe mbashiri wa ndoto,Bali aliumbwa ili awe mtume wa mataifa.Kuwa mtume wa mataifa ni maono ambayo yalikuwa ndani ya Paulo hata kama hapo awali alikuwa ni muuaji,lakini Bwana Mungu alikwisha mtenga awe mtume wa mataifa. (Wagalatia 1:15-16)

Haleluya,.....
Glory to God...

Pia tunaona Maono ya ujio wa Bwana Yesu Kristo chini ya mbingu.Maono ya ujio wa Bwana Yesu Kristo yalikuwa ni kuokoa kile kilichopotea.Kuwaokoa watu na dhambi zao. Pia Yesu Kristo amebeba kusudi la kurejesha ushirika wa Roho mtakatifu,ushirika ule uliopotea pale katika bustani ya Edeni.

*Sasa hayo yote yalikuwa ni MAONO...

ITAENDELEA...

*Usikose fundisho lijalo,tutakapokwenda kuangalia maono yatupasayo kuyapata.

Kwa huduma ya maombi na maombezi,basi usisite kunipigia simu kama wengine wanipigiavyo kwa namba hii;
0655-111149.

UBARIKIWE.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni