Jumanne, 4 Machi 2014

KONGAMANO LA MOYO WA MWANAMKE KUANZA LEO HII LIVING WATER DSM

Kwa wale ambao wako jijini Dar es Salaam, kinadada kwa kina mama, hili ni tukio la kipekee ambalo unapata kufunguliwa kwayo, kwani kutakuwa na wazungumzaji wenye uzoefu mbalimbali kwa habari ya wakina mama, ambapo wenyeji wa kongamano la Moyo wa Mwanamke, Mtume Onesmo Ndegi na Mwalimu Lilian Ndegi, watakuwa pamoja na waalikwa kutoka mataifa tofauti tofauti barani Afrika kuzungumza juu ya mada ya Nguvu ya Maarifa katika Maisha ya Mwanamke.

Tukio hili lipo Living Water, Makuti Kawe, kuanzia leo Jumatano hadi tarehe 9 Machi, yaani Jumapili, hakuna kiingilio.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni