Jumanne, 30 Mei 2017

YESU ANAKUJA.

 Na Mtumishi Oscar Samba.
(MWANAKONDOO Ministry)
Ni kweli ndugu yangu Ujio wa Yesu Kristo huu karibu mno na anakuja ili kuuhukumu ulimwengu hali itakayotoa maamuzi ama hatima ya maisha yako. Kama utaenda mbinguni ama Jehanamu ya Moto.

Kumbuka waendao mbinguni ni wale waliomwamini kama Bwana na mwokozi wa Maisha yao. Na kama hauja fanya hivyo ni wangu wito kumua hivyo sasa kwani ukifa hutakuwa na uamuzi katika hilo tena.
Warumi 10:9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Jumatatu, 29 Mei 2017

UHAKIKA BAADA YA KUFA.

Na Mtumishi Oscar Samba.

(MWANAKONDOO Ministry)

Ni jambo jema kuwa na uhakika wa maisha utakayo ishi ama sehemu utakayoenda mara baada ya kufa. Na uhakika huo unatokana na wewe jinsi ulivyo amua kuyaishi maisha unayoishi hivi sasa.
Maandiko yanasema wazi ya kwamba mara baada ya kufa ni hukumu, ikiwa na maana huwezi kutubu baada ya kufa ama hakuna atakayekuamulia mahali pakwenda mara baada ya kifo chako nikiwa na maana ya kwama hata ndugu zako wangekupenda na kukuombea kwa jinsi gani bado isingalikupa tiketi ya kubadilishiwa maisha ama sehemu upaswapo kwenda.

NINA MANTIKI YA KWAMBA, UWAMUZI WA UTAENDA WAPI UNAFANYIKA UNGALI HAPA DUNIANI NA SIO BAADA YA KUTOWEKA AMA KUNYAKULIWA. USIKUBALI KUDANGANYWA NA WIMBI LA UONGO WA MCHANA YA KWAMBA ETI UTAOKOKA MARA BAADA YA KUFA, AU UTATUBU UKIFA. HUO NI UWONGO WALA BIBILIA HAIJASADIFU JAMBO HILO.

Ni yangu rai kukutaka leo kuwamua mahali utakapo kwenda, Na kumbuka kuwa njia zipo mbili. 1. Kwanza ni ile ikupelekayo mbinguni na njia hiyo ni kumuamini Yesu. 2 Ni

MKIMBILIE YESU.


Na Mtumishi Oscar Samba
 (MWANAKONDOO Ministry)
Haijalishi unakumbana na jambo gani, ama unaishi maisha ya aina gani,? Jamii uliyonayo inakuheshimu ama kukudharau. Ila ujumbe ambao Mungu amenipa siku ya leo ni huu; MKIMBILIYE YEYE.

Ukifika kwa Yesu kila kinachokusumbua kitakoma, magonjwa, mateso ya kimaisha, ugumu wa kiuchumi, ndoa kusumbua, taabu za kukataliwa na kutengwa na ndugu. Ama ni tabia za ukahaba, umalaya, wizi ulevi na hata ile ambayo hakuna nayeijua na nivigumu kumwambia mtu mwingine yeyote na mimi siwezi kuitaja hapa maana kimaadili sio vyema.
Katika hayo yote wewe mwendee YESU naye atakusaidia maana amesaidia wengi ikiwemo yule mwanamke aliyeonekana najisi kwa kunuka damu za mwezi na zilimtoka kwa muda wa miaka 12.

Jumamosi, 27 Mei 2017

YESU ANAKUPENDA





Na Mtumishi Oscar Samba.
Wanadamu wanaweza kukuchukia, kukutenga, kukubagua, kukudharau na hata kukunyanyapaa ila huyu YESU hawezi kukutenda hayo badala yake ni wa Upendo daima.

 

Hajui kumchukiwa mtu, hata kama ni Kahaba, Mlevi, Mwizi, Mtukanaji, jamii inamuona kama Kichaa ama aliyechanganyikiwa na Maisha ama kurukwa na Akili.

Ijumaa, 26 Mei 2017

NJOO KWA YESU.

   Na Mtumishi Oscar Samba
Yamkini umekuwa ukisumbuka ama kuangaika kutokana na mambo kadha  wakadha kukusumbua maishani mwako ikiwemo tabia usizozipenda ama masumbufu ya kimaisha. Wangu wito ninakutaka uje kwa Yesu ili akusaidiye ama akuokowe na taabu hizo.

Huyu Yesu ninayemtaja mbele yako amewawezesha wengi kutoka katika adha kama hizo, wapo waliokuwa wezi akawaokoa, akiwemo yule mwizi pale msalabani, makahaba, akiwemo Rahabau. (Waebrania11:31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani )

 

Na wewe mkaribishe Yesu Kristo leo moyoni mwako kwa amani ili akuokowe na kisha kukutoa katika hayo maangamivu ya kudharauliwa au kutengwa pia kuwa hatarini kupata magonjwa kama UKIMWI na madhara kama yakifo ama kubaguliwa daima.

 

Yesu huyu aliyemtoa Paulo Mtume aliyeitwa Sauli kwenye tabia ya uwaji anaweza kukusaidi na wewe. Natumai hivi sasa upo tayari kuokoka ili Yesu awe Msaada wako sasa.

Kama ndio Fwatisha maneno haya kwa Imani’ Sema BWANA YESU, NINAKIRI, YAKWAMBA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA WEWE NI MUNGU NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, INGIA SASA NDANI YANGU NA UNIOKOWE. AMENI.

Hongera kwa kuokoka natafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

MAWASILIANO: SIMU +255 759 859 287. WEB: www.mwanakondooinjili.blogspot.com

Alhamisi, 30 Juni 2016

ROHO MTAKATIFU ANAVYOONGOZA WANA WA MUNGU KUTEMBEA NA MUNGU KATIKA MAENEO MBALIMBALI YA MAISHA YAO

Jina la Yesu Kristo litukuzwe milele!
Leo nataka kuanza mfululizo mwingine wa somo, ambao naamini utakuwa wa msaada sana kwako, katika kuimarisha uhusiano wako na Mungu.
Somo lenyewe ni hili: “ROHO MTAKATIFU ANAVYOONGOZA WANA WA MUNGU KUTEMBEA NA MUNGU KATIKA MAENEO MBALIMBALI YA MAISHA YAO”.
Mfano na 1: Tunaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume 27:10, tunaona jinsi mtume Paulo alivyoarifiwa na Roho Mtakatifu, juu ya hatari iliyokuwa mbele yake, katika safari aliyokuwa nayo na wenzake.
Mtume Paulo akawaambia wenzake hivi: “naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi si ya shehena na marikebu tu, ila na ya maisha yetu pia”. Na jambo hili likatokea kweli kama alivyosema!
Swali la msingi la kujiuliza hapa ni kutaka kujua mtume Paulo alijuaje juu ya hatari ile! Roho Mtakatifu alitumia njia gani kumjulisha kwa uwazi namna ile? Je, na sisi leo Roho Mtakatifu anaweza kutujulisha juu ya hatari zilizo mbele yetu na tukauelewa ujumbe wake?
Mfano na 2: Je! Unafahamu mtume Paulo na wenzake walikuwa wanaamuaje juu ya eneo la kwenda kupeleka neno la Mungu? Ukisoma habari zao kwenye biblia, utajua ya kuwa ni kwa msaada wa uongozi wa Roho Mtakatifu.
Kuna wakati walikuwa wakipita nchi za Frigia na Galatia zilizokuwa Asia, wakitaka kulihubiri neno la Mungu huko. Biblia inasema walikatazwa “na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia” (Matendo ya Mitume 16:6).
Biblia inaendelea kutueleza juu ya safari yao hiyo ya kwamba: “Walipofika kukabili Misia wakajaribu kwenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa” (Matendo ya Mitume 16:7). Na baada ya hapo, Roho akawapa kufahamu kuwa, walitakiwa kwenda Makedonia kuhubiri neno huko. Na ndivyo walivyofanya!
Swali la msingi la kujiuliza hapa, ni kutaka kujua walijuaje kuwa katika wazo walilokuwa nalo, Roho Mtakatifu alikuwa anawakataza wasilifanye, au anawanyima ruhusa wasilifanye? Na ikiwa Roho Mtakatifu ana wazo analotaka walitekeleze walilijuaje?
Je! Kwetu sisi – tulio wana wa Mungu kipindi hiki, tunaweza kupata msaada wa Roho Mtakatifu kuhusu mahali pa kwenda, au mahali pa kutokwenda, kama akina mtume Paulo walivyosaidiwa?
Na ikiwa ni hivyo – ina maana si suala la mtoto wa Mungu kuamua kwenda mahali popote atakavyo, bali hili ni muhimu ajue wazo la Roho Mtakatifu aliye naye ndani yake kuhusu safari yake hiyo!
Mfano na. 3: Roho Mtakatifu ndiye aliyemsaidia Yesu kuchagua wanafunzi wake kumi na wawili. Biblia inasema habari hizi za Yesu ya kuwa: “Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume” (Luka 6:12,13).
Habari hii haituambii moja kwa moja ni kwa namna gani, na kwa njia gani Yesu aliweza kufanya maamuzi ya nani amchague, na nani asimchague “miongoni” mwa wanafunzi wengi aliokuwa nao wakati ule!
Kwa msomaji yeyote wa biblia, anajua ni Roho Mtakatifu aliyemsaidia kufanya uchaguzi wa watu wa kukaa naye karibu! Lakini swali la kujiuliza ni kutaka kujua Roho Mtakatifu alimsaidia kwa njia zipi?
Nina uhakika tukijua jinsi Yesu alivyosaidiwa katika hili, itakuwa ni rahisi kwetu kusaidiwa na Roho Mtakatifu kujua watu wa kuwa nao karibu, na watu wa kukaa nao mbali! Pia naamini tunaweza kujua ni nani wa kushirikiana naye, na ni nani wa kutoshirikiana naye!
Biblia inasema katika Warumi 8:24 tunasoma ya kwamba: “wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu”.
Na Yesu akizungumza juu ya Roho Mtakatifu atakapokuja kwenye maisha ya wanafunzi wake alisema: “Lakini yeye atakapokuja huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote;…na mambo yajayo atawapasha habari yake” (Yohana 16:13).
Nataka ujue ya kuwa, ikiwa wewe ni mtoto au mwana wa Mungu, ni haki yako itokayo kwa Baba yako, yaani Mungu, kuongozwa na kutegemea kuongozwa na Roho Mtakatifu!
Uwe mtumishi wa Mungu au usiwe mtumishi wa Mungu – ili mradi tu wewe ni mtoto wa Mungu; Roho Mtakatifu uliye naye amepewa jukumu la kukusaidia, ikiwa ni pamoja na jukumu la kukuongoza katika maisha yako ya kila siku!
Ndani ya mfululizo wa somo hili, tutajifunza njia kadhaa anazotumia Roho Mtakatifu kumwongoza mwana wa Mungu. Kwa hiyo nakuombea kwa Mungu, akuwezeshe kukaa mkao wa kujifunza somo hili!

Jumamosi, 25 Juni 2016

BLOGU YA MWAKASEGE INJILI KUITWA MWANAKONDOO Kwa hiyo anuani yetu haitakuwa tena www.mwakasegeinjili.blogspot.com BALI ITAITWA www.mwanakondooinjili.blogspot.com

Habari njema ni kwamba, tunaibadilisha blogu hii inayoitwa MWAKASEGE INJILI na itaitwa MWANAKONDOO.
Sababu za mabadiliko haya yanatokana na mtazamo mpya wa uendeshaji wake tafadhali mtaarifu na mwenzako mabadiliko haya .
Kwa hiyo anuani yetu haitakuwa tena www.mwakasegeinjili.blogspot.com BALI ITAITWA www.mwanakondooinjili.blogspot.com

Jumanne, 10 Machi 2015

WAPENDA MIUJIZA MAKANISANI, HII IMEWAPATA WENZENU

Hakika muyaonapo haya jua kwamba ule mwisho umekaribia… habari hii ya kusikitisha ni taa nyekundu kwa wakristo wote wanaotafuta miujiza ya watoto ama utajiri kwa kuhama hama makanisa yao kwa madai ya kutafuta neno la Mungu..

Wanawake na mabinti waliopewa mimba na nabii huyo.

Huko nchini Nigeria wanawake zaidi ya 20 wakiwemo wake za watu na mabinti wamepachikwa mimba na "nabii" wao ambaye amedai aliambiwa na Roho mtakatifu kufanya nao mapenzi wanawake hao. Nabii huyo alifahamika kwa jina la Timothy Ngwu ambaye ni mchungaji kiongozi wa kanisa la Vineyard Ministry of the Holy Trinity huko Enugu tayari anashikiliwa na jeshi la polisi la jimbo hilo kwa kosa la kuwalazimisha kufanya nao mapenzi na wanawake hao.


Mchungaji huyo amedai anatii wito wake wa kinabii na kiroho alioitiwa na kufanya sawa na mapenzi ya Mungu kwa kuwapa mimba yeyote yule aliyechaguliwa na kuwekwa wazi na Roho mtakatifu bila kujali kama mwanamke huyo ameolewa ama la alisema msemaji wa jeshi la polisi Enegu kamanda Ebere Amaraizu akitoa taarifa kwa vyombo vya habari na kudai kwamba mwanamke akijifungua mtoto hubakia kwenye huduma hiyo na mzazi wake


Taarifa kutoka kwa familia za mchungaji huyo zinasema mkewe aitwaye Veronica Ngwu ambaye alichoshwa na tabia ya mumewe hasa alipompa ujauzito mdogo wake na kuamua kumripoti Polisi. Kwa upande wa kaka wa mtuhumiwa ambaye hakutaka jina lake lifahamike ameiambia Vanguard report kwamba amekuwa akimuonya kaka yake juu ya tabia yake kwa muda mrefu lakini hakutaka kusikiliza, amesema gadhabu ya Mungu imeshuka juu ya kaka yake.

"Ngoja niwaambie hasira ya Mungu imemshukia kaka yangu tumekuwa tukimuonya kila siku kuacha alichokuwa akifanya amejaza boma letu kwa kuzaa watoto bila uangalifu na kutuambia tunamuonea wivu kwasababu anafanya maagizo ya Mungu" alisema kaka mtu na kuongeza kwamba angalia majengo yote ya kanisa ameyageuza kuwa ya kwake kwa jina la huduma yake, alimfukuza mkewe wa ndoa waliyezaa naye watoto watatu na kuanza kuwajaza mimba wake za watu na mabinti wadogo, we angalia boma lote limejaa watoto wa jinsia zote alilalamika kaka huyo.

Aidha kaka huyo amesema waumini wote wa kanisa la kaka yake ni wapumbavu kwasababu mwanamke hawezi kumuacha mumewe na kwenda na mwanaume mwingine kwa kisingizio cha kwenda kumuabudu Mungu na kufanya zinaa, na kudai hawezi kujiingiza katika tatizo hilo, "Vero amefungua msaada kwa wamama hao ngoja wayamalize na polisi ila nataka huduma hii ifungwe kabisa" alisema

Ngwu ameiambia NaiJ kwamba kaka yake ana wake wapatao watano na watoto 13 pamoja na wake za watu kwa madai ya kufuata mapenzi ya Mungu. Amedai hajawahi kufanya mapenzi na wake za watu ila amefanya hivyo endapo waume zao wamekubaliana na ombi la Roho mtakatifu. Calista Omeje na Assumpta Odo ni wanawake ambao waliawaacha waume zao ili kuishi na nabii huyo kwakuwa ilikuwa ni upako wa kinabii wa mchungaji huyo.


Calista ambaye ana watoto 10 na mumewe alipewa mimba na mchungaji huyo ila mtoto alikufa, amesema mwanamke huyo alimkabidhi mchungaji huyo binti yake huku Odo naye amesema mchungaji huyo amempa mimba yeye na binti yake.


Chanzo ni Wilfredasuquo
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/03/wapenda-miujiza-makanisani-hii.html#sthash.MeRl5fwF.dpuf

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA


Siku ya jumamosi iliyopita katika ukumbi mkubwa wa Blue Pearl uliopo ndani ya Ubungo Plaza jijini Dar es salaam kulishuhudiwa tukio la Askofu na mwanzilishi wa kanisa la Ufufuo na Uzima nchini Josephat Gwajima akitunukiwa shahada ya udaktari wa heshima ph.D katika thiolojia kwa mchango wake wa uanzilishaji kanisa hilo nchini.

Shahada hiyo ya heshima ilitolewa na chuo kikuu cha Omega Global University cha nchini Afrika ya kusini ambapo pia viongozi wengine walitunikiwa shahada hiyo tukio ambalo pia lilihudhuriwa na wachungaji na watumishi kutoka makanisa mbalimbali nchini pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wa watunukiwa.








- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/03/mchungaji-josephat-gwajima-atunukiwa.html#sthash.qjJr3GVb.dpuf

SOMO: KIFO CHA MTU ALIYEOKOKA - ASKOFU ZACHARY KAKOBE


Askofu Zachary Kakobe

SOMO: KIFO CHA MTU ALIYEOKOKA

Kuna mambo mengi sana ya kujifunza katika Kitabu cha YOHANA. Leo, tunaendelea kujifunza Kitabu hiki katika Biblia zetu, kwa kutafakari kwa makini YOHANA 11:1-16. Katika mistari hii, tunasoma juu ya kifo cha Lazaro, na hivyo kujifunza juu ya KIFO CHA MTU ALIYEOKOKA. Hata hivyo, kuna mafundisho mengi yanayoambatana, tunayojifunza hapa. Tutayagawa mafundisho tunayoyapata katika mistari hii, katika vipengele kumi na moja:-

(1) UPENDO WA KINDUGU KATIKA UGONJWA (MST. 1-3);

(2) KUUGUA KWA WATU WALIOOKOKA (MST. 3);

(3) UGONJWA HUU SI WA MAUTI (MST. 4);

(4) UTUKUFU WA MUNGU HUONEKANA KATIKA MATATIZO (MST. 4);

(5) UPENDO WA MUNGU KATIKA KUCHELEWA KUSHUGHULIKA NA

MATATIZO YETU (MST. 5-6);

(6) KUSAMEHE NA KUSAHAU (MST. 7-8);

(7) MTU AKIENDA MCHANA HAJIKWAI (MST. 9);

(8) YESU KWETU NI RAFIKI (MST. 11);

(9) KIFO CHA MTU ALIYEOKOKA (MST. 11);

(10) UWEZEKANO WA WANAFUNZI WA YESU KUTOKULIELEWA

NENO LA MUNGU (MST. 12-14);

(11) WAJIBU WA KUTIANA MOYO KUSONGA MBELE (MST. 15-16).



(1) UPENDO WA KINDUGU KATIKA UGONJWA (MST. 1-3)

Lazaro alikuwa hawezi, yaani alikuwa mgonjwa. Mtu huyu alikuwa anakaa mji wa Mariamu na Martha, dada yake. Siyo kwamba mji huu ulikuwa mali ya Mariamu na Martha, bali lugha hii ilitumika kueleza kwamba mji huo ndiyo pia walipokuwa wanakaa Mariamu na Martha (YOHANA 1:44). Mariamu huyu, ndiye aliyempaka Yesu marhamu (YOHANA 12:3). Akina dada hawa walipoona kaka yao Lazaro anaumwa, walihusika sana na ugonjwa wake na wakapeleka ujumbe kwa Yesu. Sisi nasi kama watu tuliookoka, inatupasa kuhurumiana na kupendana kama ndugu, kwa kuonyesha upendo wa kindugu kivitendo, katika magonjwa ya ndugu zetu katika Kristo (1 PETRO 3:8; WARUMI 15:1). Katika makanisa yetu ya Nyumbgani, tunapaswa kuangaliana sisi kwa sisi katika hali za ugonjwa, na kumpelekea Yesu ujumbe, na kumweleza juu ya kaka na dada zetu katika Kristo wanaoumwa kwa kuwaombea (WAEBRANIA 10:24; 2 WAFALME 8:29; MST. 3). Ndiyo maana ni muhimu kwa kila mmoja wetu kujiunga na Kanisa mojawapo la Nyumbani ili kupata nafasi ya kuonyesha upendo huu kivitendo. Yesu, anahusika sana na ndugu zetu wanaoumwa tunapomwomba (MARKO 1:29-31).

(2) KUUGUA KWA WATU WALIOOKOKA (MST. 3)

“Yeye umpendaye hawezi“. Yesu alikuwa anampenda Lazaro, kudhihirisha kwamba Lazaro alikuwa ameokoka (YOHANA 14:21). Hata hivyo, hapa tunaona kwamba Lazaro alikuwa anaumwa. Kuugua kwa mtu aliyeokoka, siyo jambo la ajabu (2 WAKORINTHO 5:2-4; 2 TIMOTHEO 4:20; WAFILIPI 2:25-27). Hata hivyo, kwa kuwa Yesu anatupenda, tukimwita katika ugonjwa, ataitika na kutuponya sawasawa na ahadi zake (YEREMIA 33:3; 30:17).

(3) UGONJWA HUU SI WA MAUTI (MST. 4)

Ugonjwa wa mtu aliyeokoka, hata kama ni wa kutisha kiasi gani, si wa mauti; kwa maana kwamba, si wa MAUTI YA MILELE, maana juu yake huyo, mauti ya pili au ya milele, HAINA NGUVU (UFUNUO 20:6). Kwa hali hii, Shetani hapaswi kutubabaisha, kwa kututishia kutuua. Tunajifunza pia hapa kwamba siyo kila ugonjwa unaokuja kwetu unakukja kutuua (YOHANA 9:1-2). Magonjwa mengine anayoleta Shetani kwetu, hatimaye humletea Mungu utukufu mkubwa pale anapotuponya kwa miujiza.



(4) UTUKUFU WA MUNGU HUONEKANA KATIKA MATATIZO (MST.4)

Hatuna haja ya kuogopa kukutana na matatizo au majaribu katika maisha yetu ya kimwili na kiroho. Kwa kutumia matatizo yanayotukabili, Mungu hujipatia utukufu, na kutuonyesha jinsi alivyo na uwezo wa kutupigania. Tukimwomba Mungu halafu akatushindia kwa kututoa katika matatizo hayo, tunajengewa imani zaidi ya kumtumaini na kuwa karibu naye. Uweza wa Mungu, huonekana sana pale tunapokuwa na matatizo au udhaifu na ndipo tunapojengeka kiimani. Kwa sababu hii, Paulo Mtume, hakuogopa matatizo, bali alipendezwa nayo! (2 WAKORINTHO 12:9-10). Bila Bahari ya Shamu, tutauonaje uwezo wa Mungu wa kuigawa bahari? Bwana atupe neema ya kutokubabaishwa na matatizo katika Jina la Yesu.



(5) UPENDO WA MUNGU KATIKA KUCHELEWA KUSHUGHULIKA NA MATATIZO

YETU (MST. 5-6)

Pamoja na Yesu kumpenda Martha na umbu lake yaani, dada yake Mariamu, pamoja na kaka yao Lazaro, hata hivyo, hakushughulikia tatizo lao haraka! Yesu alijua wakati mzuri zaidi wa kujipatia utukufu mkubwa zaidi. Akangoja Lazaro afe, ili amfufue, badala ya kumponya. Angemponya tu katika ugonjwa wake, usingekuwa muujiza mkubwa wa kumpa utukufu mkubwa. Tunapoona Mungu amechelewa kutujibu, siyo kana kwamba hatupendi au tumekosea, la hasha. Yeye anajua wakati mzuri zaidi wa kutupa majibu ya mahitaji yetu, kwa utukufu wake (ISAYA 54:7-8). Wakati tunapoona matumaini yetu yametupotea, ndipo Yesu anapotujulisha kuwa ndiye BWANA muweza yote (EZEKIELI 37:11,13).

(6) KUSAMEHE NA KUSAHAU (MST. 7-8)

Wakati huu, ilikuwa yapata miezi miwili, tangu Yesu Kristo alipotafutwa kupigwa kwa mawe na Wayahudi. Yesu alikwisha kuwasamehe na kusahau, lakini kwa wanafunzi wa Yesu, mambo ya miezi miwili iliyopita, wanayita ya JUZIJUZI! Ndivyo walivyo watu wengi, wanakuwa wagumu kusamehe na kusahau! Tuige mfano wa Yesu na kumwomba atuwezeshe kuwa kama yeye.

(7) MTU AKIENDA MCHANA, HAJIKWAI (MST. 9-10)

Wanafunzi walimwuliza Yesu, “unakwenda huko tena walipotafuta kukupiga kwa mawe?“ Akajibu, mtu akienda mchana hajikwai maana aiona nuru! Maana yake ni kwamba, alikuwa anakwenda kwa sababu alipokea neno, agizo, au ufunuo wa kufanya hivyo kutoka kwa Baba yake. Neno hili, lilikuwa nuru au taa na mwanga wa njia yake, hivyo asingeweza kujikwaa! (ZABURI 119:105). Tukipata ufunuo halisi wa neno kutoka kwa Mungu (RHEMA), neno hilo hutupa imani inayotuhakikishia kutokujikwaa. Ni muhimu kuutafuta uso wa Mungu kabla ya kuamua kwenda mahali pa hatari.

(8) YESU KWETU NI RAFIKI (MST. 11)

Rafiki yetu Lazaro! Yesu, ni rafiki yetu (YOHANA 15:14-15). Kwa kuwa Yesu ni rafiki yetu, anatupenda sana (YOHANA 15:13). Anatupenda katika dhiki zetu, na kutaka kutusaidia. Siyo hilo tu, rafiki hupenda mazungumzo na rafiki yeake. Hivyo Yesu anahuzunika kutuona hatuzungumzi naye katika maombi, ikiwa Yesu kwetu ni rafiki inatukumbusha kufanya yanayompendeza ili tusimwudhi rafiki yetu.

(9) KIFO CHA MTU ALIYEOKOKA (MST. 11)

Lazaro AMELALA! Kufa kwa mtu aliyeokoka, ni sawa na KULALA! Kulala, ni kupumzika baada ya taabu za mchana kutwa. Vivyo hivyo, kufa kwa mtu aliyeokoka, ni kupumzika baada ya taabu za dunia (UFUNUO 14:13). Hatupaswi kuogopa kifo tunapokuwa tumeokoka. Mtu aliyeokoka, anapokufa, roho yake HUMIMINWA na kuwekwa kwenye mwili mzuri sana wa mbinguni, kama mafuta yanayomwagika, yanavyotolewa kwenye chombo kibovu na kumiminwa kwenye chombo kizuri (2 TIMOTHEO 4:6; 1 WAKORINTHO 15:40). Hata hivyo, mtu ambaye hajaokoka haendi kupumzika anapokufa, bali anakwenda kuumizwa kwenye mateso! (LUKA 16:24-25). Wayunani, waliyaita makaburi, “KOIMETERIA“. Kutokana na neno hili tunapata neno la Kiingereza, DORMITORIES au mabweni, mahali pa kulala au kupumzika.

(10) UWEZEKANO WA WANAFUNZI WA YESU KUTOKULIELEWA NENO LA

MUNGU (MST. 12-14)
Yesu aliposema Lazaro amelala, alikuwa anatumia lugha ya Biblia, inayomaanisha amekufa (MWANZO 47:29-30; KUMBUKUMBU 31:16; 2 WAFALME 8:24; MATENDO 7:59-60; 8:2). Hata hivyo, pamoja na wanafunzi wa Yesu kusoma Agano la Kale, hapa hawakumuelewa Yesu. Wakasema ikiwa amelala, atapona. Waliwaza kwamba “Ikiwa Yesu anasema amelala, huenda sasa amepata nafuu ya kuweza kupata usingizi, maana inaelekea mwanzoni, hali ilikuwa mbaya kiasi ya kwamba alikuwa halali“. Hapa tunajifunza uwezekano wa wanafunzi wa Yesu kutokulielewa neno la Mungu. Inatupasa kumwaomba Yesu atufunulie akili, ili tupate kulielewa Neno la Mungu (LUKA 24:44-45).

(11) WAJIBU WA KUTIANA MOYO KUSONGA MBELE (MST. 15-16)

Wanafunzi wa Yesu, walijua kwamba suala la Yesu kwenda Uyahudi tena, ilikuwa kwenda kufa, hivyo hawakuwa na utayari. Hata hivyo, baadaye Tomaso anawaambia wenzake “Twendeni na sisi ili tufe pamoja naye“. Anawatia moyo wenzake kusonga mbele bila kujali majaribu yaliyo mbele yetu. Jina Tomaso linatokana na jina la Kiebrania “THOMIM“, lenye maana “PACHA“.

…………………………………………………………………………………………………………………………………..

Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni? Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14). Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27). Kinyonge ni kipi? Ni yule anayetenda dhambi. Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge! Je, wewe ni mtakatifu? Jibu ni la! Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13; YOHANA 14:6). Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni; “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu. Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi. Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo. Bwana Yesu niwezeshe. Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu. Amen”. Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni. Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!

- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/03/somo-kifo-cha-mtu-aliyeokoka-askofu.html#sthash.WQY77Hz3.dpuf

Jumatatu, 20 Oktoba 2014

MAMBO MAKUU NNE (4) KATIKA UOKOVU WAKO


Wapili kutoka kushoto ndie Mtumishi Jeremiah Mlawa akiwa na watumishi wenzake katika maeneo ya Ibada, (Picha na Makitaba)
Na Mtumishi Jeremiah Mlawa
1.Uwe na Imani,Hakikisha ndani ya uokovu wako uwe ni mtu wa  imani,jiamini na pia amini sehemu unayoabudu.
2.Uwe Mkweli,Epuka kuwa muongo na penda kuwa mkweli kwa kushuhudia kweli ya MUNGU,pia usiwe mzungumzaji kwa mtu ambaye unajua atahadhiri uokovu wako.Unapo mshuhudia mtu kuhusu uokovu hakikisha wewe mwenye ni msafi ndani ya moyo wako na ukifanya hivyo jina la MUNGU halitatukanwa na ushuhuda wako utakuwa barua.
3.Uwe Mtii,Hakikisha kwenye eneo unalolelewa unatii unaloambiwa,usiwe mwepesi wa kuitikia na kutokutii.Unapo weka ahadi kwa mtumishi ama mpendwa hakikisha unatii.Penda kutii muda wako katika maswala yako yakimaisha kama ibada inaanza saa 2 kamili hakikisha unatekeleza ama kutimiza hilo,Baraka za MUNGU huenda na wampendao.
4.Uwe ni Mtu wa Haki.Hakikisha kwenye maisha yako unaishi kwa haki na watu wote,na mwenendo wako uwe wa haki,tafuta amani na watu wote.Usijiesabie haki kwa kumuona mtu Fulani ambae ni mwenye dhambi anahatia na wewe ni bora kuliko yeye,Mungu wetu ni Mungu wa wote wenye mwili.Kama unawaona wako kinyume wewe waombe.

Ukiyazingatia haya hakika hali yako ya kiroho itakuwa ya utofauti kwa viwango vikubwa mno.MUNGU wetu wa mbinguni na BWANA YESU akuwezeshe kutii hayo.

Jumanne, 7 Oktoba 2014

Biblia inasemaje juu ya kutoa fungu la kumi ama Sadaka ya Michango ?

Hawa ni wataalamu wa injili kwa watu wote GFAP wakiwa katika picha ya pamoja huko ROMBO KILIMANJARO

Jibu: Kutoa fungu la kumi ni jambo ambalo wakristo wengi hung’ang’ana nalo. Katika makanisa mengine kutoa fungu la kumi imesisitizwa kupita kiasi. Wakristo wengi pia hukataa kutii agizo la kutoa sadaka kwa Bwana. Kutoa fungu la kumi au sadaka inahitajika kuwa ni kitendo cha furaha na baraka. Lakini sivyo katika makanisa ya sasa.

Kutoa fungu la kumi ni agizo la agano la kale. Hili lilikuwa sharti la kila mwenye kupata zao au mfugo alete sehemu ya kumi ya pato hekaluni (mambo ya walawi 27:30; hesabu 18:26; kumbukumbu la torati 14;24; mambo ya nyakati ya pili 31:5). Wengine huchukulia ya kuwa fungu la kumi, katika agano la kale ilikuwa kama sehemu ya ushuru uliokuwa ukitolewa kwa ajili ya makuhani na walawi. Agano jipya haiamrishi wala kupendekeza mfumo halali wa kutolea fungu la kumi. Paulo asisitiza kuwa waumini watenge sehemu ya mapato yao kwa ajili ya kusimamia kanisa (wakorintho wa kwanza 16:1-2).
(1 Wakorintho 16 : 1-24
16.1 Kwa habari ya ile changizo kwa ajili ya watakatifu, kama vile nilivyoamuru makanisa ya Galatia, nanyi
fanyeni vivyo.
16.2 Siku ya kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake; ili
kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja;)

Agano jipya halielezi kiasi cha pato ambacho ni kitengwe kwa ajili ya kusimamia kanisa. (wakorintho wa kwanza 16:2). Kanisa la kikristo leo limechukua kile kiwango cha fungu la kumi kutoka kwa agano la kale na kukisisitiza kuwa ndicho kiwango cha chini cha mkristo kutoa. ijapokuwa agano jipya haitoi kiwango cha kutoa, inaelezea umuhimu na manufaa ya kutoa.

Ni watoe sawa na uwezo wao “ kulengana na pato lake.” Wakati mwingine ina maana ya kutoa zaidi ya fungu la kumi,

 Yote hutegemea uwezo wa mkristo mwenyewe na mahitaji ya kanisa. Kila mkristo sharti aombe na kutafuta hekima kutoka kwa Mungu juu ya swala hili (Yakobo 1:5). “ kila mtu niatoe kile alicho azimia kutoa kutoka ndani ya moyo wake, si kwa manung’uniko wala kulazimishwa, kwa kuwa Mungu hupenda kwenye kutoa kwa moyo mkunjufu” (wakorintho wa pili 9:7).

Pia hilo andiko nalipeleka kwa wale watumishi wa MUNGU wanao wapangia watu kiasi cha kutoa hususani kwenye michango,hakika jambo hili sio jema kwani kutoa kwa Toka KWA BWANA na haipendezi kumpangia mtu atoe nini bali kama alivyo sikia MOYONI mwake.

Pia katika makanisa ya leo usipo toa wanakuona kama mtu asiye endana nao yaani ajenti au msaliti hili sio sahihi kwani mtu kama mimisiwezi kutoa bila kusikia kwa hiyo hata msisitizo wakibina damu huwe mkubwa kiasi gani ni lazima nisikie kwa BWANA ama sivyo utakuwa tuu ni mchango na haifai kutoa kisha kunung'unika.

Siku njema na endelea kuetmbelea www.mwanakondooinjili.blogspot.com

USUHUDIAJI WA MTU KWA MTU KANISA LA TAG VCC ARUSHA

NA mama Mcungaji CATHERINE MBUGHI
Kushoto ndie mama Mchungaji Catherini Mbughi akisisistiza jambo la MUNGU katika jukwaa la Injili na kulia ndie Baba Mchungaji Aloice Mbughi.Picha na Makitaba.

Ninayo furaha ya hali ya juu kukukaribisha ewe msomaji wa blogu hii ya www.mwakasegeinjili.blogspot.com katika ujumbe huu wa leo kama ulivyotolewa kwenye kanisa la VCC na huyo mtumishi wa MUNGU kwenye mafundisho ya asubuhi ya wanafunzi na maandiko.

Ninae kuandikia ujumbe huu na kukuletea ni mimi OSCAR SAMBA na moja kwa moja tuzame kwenye somo letu la leo ambalo linalenga kukutia moyo wewe uliye okoka kuhusu kuwashuhudia wengine.

Luk 10:23-26
10.23 Akawageukia wanafunzi wake, akasema nao kwa faragha, Heri macho yaonayo mnayoyaona ninyi.
10.24 Kwa kuwa nawaambia ya kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuyaona mnayoyaona
ninyi wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi wasiyasikie.
10.25 Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi
uzima wa milele?
10.26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

Mpendwa kumbuka kuwa Inatupasa kuwashuhudia watu wote, Yohana 3:16, 3.16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu
amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.                    

,Unapo mshuhudia mtu msome NENO la Mungu kwani ndio silaa yetu na haikupasi kwenda vitani bila silaa.
Yohana 14.15 Mkinipenda, mtazishika amri zangu.Mpendwa andiko hili yatupasa kuhakikisha ya kwamba tunalishi hili kama kweli tunalipendana, kwa kuanza kushuhudia, na hii sio amri tuu bali pia ni agizo kuu.

Waambie ya kwamba mshahara wa dhambi ni mauti wala usiwafiche waeleze kuhusu jehanamu na pia wakumbushe uzuri wa mbinguni na waambie mbingu ipo kwa ajili yao tuu kama wakiamini.

Ukisha maliza muulize je, upo tayari kumapa YESU maisha yako akisema ndio muongoze sala  ya toba na akisema laa mulize na sema nae kuhusu hatima ya maisha yake nakumuliza je, anafahamu nini kuhusu hatima ya maisha yake baada ya kufa,mkumbushe kwa herufi KUBWA na msisitizo kinywani kuwa ni hukumu na hukumu yake MUNGU ni ya HAKI.

Mpe mfano wa tajiri na Lazaro kwani mara baada ya kifo kila mmoja alivuna alichopanda, Lazaro mbinguni tena kifuani mwa Ibrahimu na Tajiri motoni.

Hakika kupitia NENO la Mungu inawezekana kuwafanya watu kuingia mbinguni.Maandiko tuliyoyasoma hapo juu yanatutaka tuwapende jirani zetu kama Nafsi zetu pia “1 YOHANA 4-20-21   4.20 Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana
asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona.
4.21 Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.
Kwa hiyo yatupasa kutimiza andiko hili kwa Moyo wote kwani upendo wa kweli kwa Mungu wetu huanza kwa kumpenda jirani yako na upendo wa kweli kwa jirani yako uliyo na matendo ni kumwambia habari za YESU.

Weka mpango na mikakati yakuhakikisha yakwamba ndugu zako na rafiki zako wanaokoka,usikubali waende huko kwani kunatisha mnoo.
Mliliye YESU nasema nae kuhusu ndugu na jamaa zako lakini pia toka ka’a waambie hao watu ya kwamba YESU anaokoa.

MAMBO MUHIMU
1.Uwe na huruma ya KIMUNGU ndani yako,hakikisha unaguswa na tabu zao na mateso yao
2.Uwe na upendo wa MUNGU ndani yako YOHANA 3:16
16 Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu
amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Usikubali juma hili lipite bila kuwaambia habari za YESU,ukikutana nae njiani ama popote pale mwambie YESU anampenda.Hata kama hataokoka leo lakini hakikisha unampandia NENO.
Upendo unagarimu,upendo unahitaji kujitoa kwa hiyo hakikisha unaingi gharama kwa kusugua goti ili watu waende mbinguni.Litumie NENO kwani hili NENO linauwezo wa kumuokoa na kumbadilisha kumbuka IMANI huja kwa kusikia kwa mantiki hiyo hilo NENO huweza kufanyika uponyaji kwake.
Kuna vilio vya aina mbili cha kwanza—ni cha mtu aliyeomba maji akiwa Jehanamu na B yake ni cha mtu aliyeomba ndugu zake wasiende jehanamu.
Luka 16:19-31
“16.19 Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula
sikuzote kwa anasa.
16.20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,
16.21 naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata
mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.
16.22 Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye
akafa, akazikwa.
16.23 Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali,
na Lazaro kifuani mwake.
16.24 Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake
majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.
16.25 Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika
maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.
16.26 Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku
kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.
16.27 Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,
16.28 kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.
16.29 Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.
16.30 Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.
16.31 Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu.”

Embu jiulize angalikuwa ni ndugu yako yuko huko jehanamu ungali jisikiaje ?
Na kilio chapi ni cha mtu uliyemshuhudia na kukataa kuokoka..
Zingatio kuu la somo la leo : TUKIKOSA HURUMA HATUTA VUNA
Naam hadi kufikia hapo ndio mwisho wa ujumbe huu tafadhali endelea kutembelea blogu hii ya www.mwakasegeinjili.blogspot.com kwa makala na habari zaidi.Pia kumbuka siku chache zijazo blogu hii itakuwa na na jina jingine ambalo ni www.ukombozig.blogspot.com na kwa sababu zaidi soma habari iliyopita.


Alhamisi, 25 Septemba 2014

KUHUSU LAANA (MAKALA)

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI JACKLINI AKIMTUKUZA MUNGU KATIKA MKUTANO WA INJILI WA GFAP ULIOFANYIKO HUKO ROMBO MKOANI KILIMANJARO JUMA LILOPITA.

KUHUSU LAANA (Kupakua/Download bonyeza link ifuatayo:
Katika waraka huu tunataka kuangalia juu ya wazo hili la “laana” itokanayo na mambo yaliyopita. Tunataka kuangalia, iwapo laana ya mtu binafsi au itokanayo na vizazi vilivyopita, inaweza kuwafungia wakristo ndani ya vifungo na kuwazuia kutokana na kupokea baraka za Mungu na Urithi wao katika Kristo. Kuanzia hapa mwanzoni mwa makala hii, hebu tuweke wazi kabisa kuwa hapa tunaongelea kuhusu mtu ambaye amehukumiwa kwa tendo la dhambi zake, akatubu na kugeuka kutoka katika dhambi zake, na akamwamini Bwana na Mwokozi Yesu Kristo kwa ajili ya wokovu wake, amezaliwa mara ya pili na kujazwa Roho wa Mungu, ameingizwa katika Agano Jipya ndani na kupitia Yesu Kristo. Hapa, kwa mtu huyo, hakuna zaidi! Hakuna kitu kilicho pungua na kwa wakristo kama ilivyoelezwa katika Agano Jipya, kuwa wakristo wa aina hiyo kama mitume walivyokuwa wakiwaandikia.

Ushahidi wa Agano Jipya

Ni kitu gani basi ambacho mitume wamewaandikia wakristo katika Agano Jipya? Wanayashughulikiaje mambo yanayojitokeza katika makanisa na watu wa Mungu? Wanayatambuaje matatizo hayo na wanatoa ushauri gani na maelekezo yapi kwao? Kwa mafundisho yoyote yale mapya, ambayo yanatoa ushauri na maelekezo yanayohusiana na wakristo, ni lazima mafundisho haya yasimamie katika misingi au yapate kuungwa mkono na maandiko ya mitume au kutoka katika mafundisho ya Yesu mwenyewe.

Kwa hiyo basi, mitume wanasemaje juu ya mafundisho yahusuyo wazo hili la “laana” zilizopita, kwamba zinaweza kuzuia maisha ya wakristo, au ya kanisa au nchi isipate kuendelea! Kwa kweli mitume hawasemi chochote kile, hakuna chochote wasemacho. Hakuna; na halikadhalika, hakuna hata mstari mmoja wa Neno la Mungu unaosema chochote kile! Wala mitume hawajaribu angalao kutamka au kugusia juu ya jambo hilo. Akili zao haziwapi kufikiria kabisa juu ya jambo hili. Yako wapi basi mausia yao wanayoyatoa kwa wakristo katika kuchunguza maisha yao ili kuhakikisha na kuwa makini sana, kwamba laana haitendi kazi yake wakati wanapokuwa katika shida ndani ya mienendo yao binafsi na kiroho? Mausio ya aina hiyo hayapo kabisa. Ni kweli kwamba Mtume Paulo anazungumza kuhusu laana, lakini anaizungumzia katika mtindo wa tofauti kabisa – yaani, anazungumzia kuhusu Kristo “akitukomboa kutoka katika LAANA ya sheria”. Tunakuja kuangalia kwa makini kuhusu jambo hili baadaye kidogo, lakini, hakuna sehemu yoyote ile ndani ya Agano Jipya lote, ambayo hata kutajwa tu kwamba laana kutoka katika mambo yaliyopita au kwamba inaweza kuzuia mwenendo wa kiroho wa mkristo au kanisa au Taifa.

Lakini sasa, sisi tutoe sababu gani tunapoona jambo hili liko kimya katika Biblia? Mafundisho hayo ya kisasa au mapya yako wazi sana na yametiririka kwa undani sana na kwa kuwa ni hivyo, basi bila shaka yangepasa kuwakilisha sehemu muhimu sana na ya lazima katika ukombozi wetu katika huyo Kristo Yesu; ikiwa jambo hili kama lingekuwa lina ukweli wowote ule.

Vitabu vingi sana vimewahi kuandika kuhusiana na jambo hili la laana, basi bila shaka, kwa hakika tungetegemea kupata misingi fulani ya mitume na ya kibiblia ndani ya mafundisho yao hayo mapya. Lakini basi, kwa nini hakuna hata mtume mmoja ndani ya Biblia anayejaribu kulitaja jambo hili katika nyaraka zake wanapoyaandikia makanisa? Je, wao walikuwa ni wajinga kiasi kwamba wameshindwa kuelewa umuhimu wa ukweli huu? Ikiwa ni hivyo basi, wao wanahusika katika kuwaacha ndani ya ujinga huo, sio tu wakristo wa vizazi vingi vijavyo, na kwa hiyo kuwazuilia uhuru wao katika Kristo. Kama ni hiyo, basi mitume wamewaachia umati mkubwa wa watu katika vifungo na giza kupitia katika karne nyingi kwa sababu ya kushindwa kwao kupokea na kufundisha mapokeo haya? Bila shaka yoyote ile, kulikuwepo na uzinzi na mila mbaya nyingi nyakati za Agano Jipya. Kwa hiyo, kwa nini basi, hawa mitume hawakuwaonya watu wa Mungu, ili wafahamu kwamba tatizo lolote lile mnalopata linatokana na laana iliyowatangulia? Kwa nini basi hawakusihi ili kuchunguza maisha yao ili waone iwapo wao wenyewe au mababu zao kama watakuwa wamehusika katika matendo ya kiShetani ambapo wengi wao wangeweza kuwa hivyo, na hivyo wangefanya hima kutubu na kuungama mambo hayo na kisha kutangaza uhuru wao katika Kirsto? Ni wapi ambapo wanashauri kufananishwa na mtu binafsi, kanisa au nchi? Ikiwa mambo hayo ni ya ukweli, basi, hilo sasa ni tatizo kubwa sana.

Hatuwezi kuachwa katika ujinga wetu, wala hatuwezi kuachwa katika vifungo! Lakini cha ajabu ni kwamba, jambo hili la laana ya mababu halitajwi mahala popote pale wachilia mbali kufundishwa pia. Elimu hiyo wanayoitoa kwa watu sio sehemu ya mafundisho ya mitume, ya Yesu Kristo wala Biblia kwa makanisa halikadhalika Agano Jipya halijafundisha hiyo kwa makanisa pia. Hakuna sehemu yoyote ile ya Agano Jipya ambapo Yesu Kristo au hata mitume wanapojaribu kutia laana ya Agano la Kale lililofanywa kati ya Mungu na Waisraeli kuitii kwa wale walioingizwa katika ufalme wa Mungu kwa kupitia uzao mpya wanavyofanya nyakati hizi.

Haya, au pengine labda wakristo wa nyakati za Agano Jipya, wao walikuwa na “usafisho zaidi na kabisa” wakati wlipookoka kuliko wakristo wa nyakati hizi za leo, na kwa hiyo hao hawakuwa na matatizo na hawakuhitaji aina hii ya mafundisho? Lakini kwa hakika mawazo hayo sio ya kweli kulingana na Neno la Mungu linavyotuonyesha. Watu walipata kuokolewa au kupokea ujumbe wa Injili kama mtu binafsi au maelfu ya watu kwa wakati mmoja. Na yawezekana pia kuwa hali ya mioyo ya wengine wao haikuwa safi au walianza vema, lakini hawakuendelea kutembea katika utiifu wa Imani na Upendo. Kama ilivyokuwa nyakati hizo halikadhalika nyakati hizi. Kimsingi, watu ni wa aina ile ile katika kila kizazi na huyapokea mambo kwa njia ya tofauti katika wokovu ambao Mungu amewapa. Na kama vile ilivyo nyakati hizi za leo, kama tusomavyo katika Agano Jipya ndivyo ilivyo kuwa pia nyakati za Agano Jipya – yaani, watu makanisani walikuwa na aina zote za matatizo yanayotofautiana: dhambi, tabia za kimwili, matendo ya uongo, uchungu, mivutano n.k. Jaribu tu kujisomea mwenyewe Wakorintho au Wagalatia, kwa mfano – utagundua haya!

Haya, iwapo wokovu wa Mungu ni ule ule leo kama vile ulivyo kuwa nyakati hizo, na iwapo mwitikio wa watu na matatizo yao ni ule ule leo, kama vile ilivyo kuwa nyakati zile za Agano Jipya; basi sasa ni kwa nini! Oho, jamani! Ni kwa nini basi Yesu Kristo mwenyewe pamoja na mitume wake hawakuwafundisha watakatifu au hata makanisa juu ya mambo hayo (au hata wale wasioamini) kwamba laana zilizopita zinaweza kuwaathiri watu wa Mungu na kuwaweka katika vifungo au giza – kama tunavyoelezwa leo na hao walimu wa kisasa? Kwa nini hawakuweza kabisa kuonyesha kwamba matatizo yetu tunayoyapata sasa tukiwa kama ni watu wa Mungu, yanatokana na laana kutoka mambo yaliyopita? Jambo hili halipaswi liwe kama vile jambo la kudhanidhani au kubuni, au kama kazi ya ubunifu ya mwanadamu. Ni jambo la hatari sana katika utata wake, kwamba ni lazima tuwe makini sana hapo katika kuyagundua mafundisho kutoka katika Agano Jipya; kwa sababu humo katika Biblia mumejazwa taarifa zote zihusuzo ukombozi wetu na wokovu katika Kristo. Lakini hata hivyo hakuna popote pale ndani yake unapoweza kuyaona mafundisho yao hayo!

Kutokana na hilo, basi hii pekee ingetosha kabisa kutuonya sisi leo, kuwa kuna kitu ambacho si cha kweli ndani ya mafundisho yao hayo na kwamba hatupaswi kuyapokea ndani ya mioyo yetu. Hii ni nyongeza yao kwenye Injili. Hii ni sumu ndani ya mioyo yetu iliyokwisha kombolewa na Kristo. Hata kama itatokea baadhi ya watu kuamini kuwa wanaweza kuipata mistari katika Agano la Kale inayounga mkono mawazo yao, bado ni lazima tutambue kuwa, kitu chochote kile kinachotakiwa kwa ajili ya wokovu na ukombozi wetu na maisha ya Ki-Mungu, kimeunganishwa na kufunuliwa hivyo pia ndani ya Agano Jipya. Kazi ya Agano la Kale ni kuonya mbele juu ya wokovu na ukombozi kwa njia mbalimbali na hii inasaidia zaidi na kufafanua na kukielezea vizuri kile kinachofundishwa ndani ya Agano Jipya. Lakini kama tunafundisha kama kwa kulazimisha kwa wokovu wetu au ukombozi kama wakristo na tunajaribu tu kupata maelezo mengine kutoka Agano la Kale kwa ajili ya kukidhi dhamira yetu ya kutaka kuungwa mkono katika jambo hilo, pasipo hata kuliona kwanza jambo hilo likifundishwa pia au kutajwa ndani ya Agano Jipya; basi ikiwa ni hivyo, hapo mafundisho yetu yatakuwa yanapingana na ukweli wa Injili.

Na hiyo sio sawa hata kidogo: hiyo ni hila, nasi tutakuwa tukiwadanganya wengine katika kufundisha hilo. Elimu yao hiyo, inapinga kabisa mafundisho ya Yesu Kirsto na ya kwamba yeye Yesu ndiye aliyesulibiwa. Hiyo ni nyongeza ya kibinadamu katika waraka wa Wagalatia. Bila shaka hakuna kupishana kabisa kati ya Agano la Kale na Agano Jipya, lakini yapo maendeleo na mabadiliko ya kimsingi. Yamechukua sehemu yake kwa sababu ya yale yaliyofanywa pale Kalvari. Kama vile ilivyo kwa makosa mengine mengi, hasa yale ya nyakati hizi za leo; mafundisho hayo hayakutokana na Biblia, bali watu wameyaanzisha au kuyabuni kutokana na mawazo yao au mtindo wao wa kufikiri, kisha wakayafasiri maandiko kulingana na matakwa ya muundo wao. Na wanapindisha na kubadilisha maana halisi ya maandiko, wakayatumia mpaka yakubaliane na muundo wa mawazo yao. Hivyo ndivyo wanavyofanya katika wanachoweza kukitumia katika Agano Jipya ili kuunga mkono mafundisho (mapokeo) yao.
Lakini hebu tutazame jinsi ambavyo watu hao wangejaribu kutafsiri baadhi ya maandiko kutoka katika Agano Jipya, ambayo ndiyo mistari wanayoitumia kunukuu. Yak.3: 7-10 na Ufu. 22:3. Hayo ni baadhi ya maandiko yanayotumiwa kunukuliwa ili kuonyesha watu kuwa laana na kulaaniwa ni vitu vinavyoendelea kuwepo leo. Kwa kadri ilivyo siyo mbaya, lakini pia wao wanaendelea kusema kuwa, kwa sababu laana inaendelea kuwepo, kwa hiyo wakristo wenyewe wanahitajika kutambua kuwa inewezekana kabisa wameshawishiwa na kuzuiwa katika maisha yao kwa laana. Lakini maandiko haya “rukii” kwenye ufahamu wa hatua hiyo wanayodai wao. Kwa kweli maandiko hayo mawili hapo juu wala hayafundishi hivyo; badala yake ingalipo inaendelea siku za leo, na watu wanafanya mambo ambayo hawapaswi kuyafanya, kwa mfano, kuwalaani wengine, na kwamba katika mbingu mpya na nchi mpya hakutakuwepo tena na laana, au tungeweza kusema kuwa, hakutakuwepo tena na hukumu – kwa ajili ya dhambi na uasi. Hata hivyo mistari hiyo hapo juu haileti uhusiano wowote kati ya matatizo ya maisha ya wakristo na laana ambayo ingeweza kuwekwa kwao au kwa mababu zao, kana kwamba hayo ndiyo iwe ni sababu ya mataizo katika maisha yao! Hakuna mahali popote pale katika nyaraka zote za Agano Jipya, ambapo hata kwa umbali tu inahesabiwa au hata kutajwa tu kwamba ndiyo sababu inayosababisha matatizo au mateso katika maisha ya wakristo, (au katika maisha ya mji au taifa). Yakobo hasemi hapo kuwa, “Tazameni, watu wanalaani, kwa hiyo mnajua laana bado inaendelea kuwepo, na kwa hiyo maisha yenu yatazuiwa kwa laana. Na kama mnalo tatizo linaloendelea katika maisha yenu, basi hilo linaweza kuwa limesababishwa na laana zilizopita. Kwa hiyo mnapaswa kuchunguza miienendo ya mababu zenu kwa makini sana ili kugundua kuwa uwezekano wa mizizi ya aina hii ya laana katika maisha yenu, na hivyo kuomba ukombozi kutokana na hilo.” Huu ni upumbavu mkubwa sana kutafsiri maandiko hayo ya Yakobo kwa jinsi hiyo. Anachokifanya Yakobo hapo katika mistari hiyo, ni kutufundisha tu kwa uwazi kwamba maneno yetu tunaposema yasiwe matamu na machungu, uchafu na usafi, baraka na laana. Jambo hilo liko wazi tu hapo, hayo ni mafundisho yenye afya nzuri tu hapo; ni mausia na kukemea kuhusiana na kuokolewa kwetu! Lakini kama nilivyotaja hapo juu, waalimu hao wanajaribu kutumia sura yoyote ile ya maandiko wanayoweza kuitumia, kisha kuipindisha na kuibadilisha, kisha kupanua maana yake halisi.

Yawezakana pia mahala pengine baadhi ya waandishi hawa wanaweza kumnukuu hata Yesu, pale anaposema, “…Wabarikini wale wanaowalaani ninyi” (Luka 6:28). Lakini katika mambo ambayo nimepata kusoma, sijaigundua hata sehemu moja ambapo waandishi hawa wanapelekea kutaja mistari hiyo pale wanapojaribu kuunga mkono mawazo yao kuhusiana na laana. Na yawezekana kuona kuwa ndiyo maana haishangazi, mafundisho hayo ya Yesu “hayapindi” kwa urahisi ili yafananishwe na mtindo wa mawazo yao. Yakobo anatueleza kuwa, anaona watu wanaendelea kulaani, wakati hawapaswi kufanya hivyo. Mafundisho hayo mapya yanasema kuwa eti ikiwa mtu bado anaendelea kulaani, kama vile Yakobo alivyosema, basi maisha ya wakristo yatadhurika kwa laana hiyo ya watu wengine. Lakini Yesu mwenyewe hasemi kuwa kama mtu atakulaani, basi “uwe mwangalifu sana, yawezekana laana hiyo ikakupata. Unauhakika kuwa hujafanya dhambi? Maana unaweza ukawa tayari uko chini ya nguvu za laana katika maisha yako, na lazima uhakikishe kwamba unataka kutoka katika laana hiyo.” Hapana. Haiwi hivyo hata kidogo; kwa sababu hata kabla ya pale Kalvari, Yesu Kristo aliwaambia watu maana halisi ya kuishi kulingana na mapenzi ya Mungu na tabia yake. Yesu alisema, Ikiwa yeyote yule atawalaani, ninyi mbarikini! – Amen! Kwisha! Hakuna zaidi ya hapo. Uwabariki tu! Hayo ndiyo mafundisho yake Yesu Kristo.

Yesu hawezi kutujaza akili zetu na mawazo ya kiushirikina na udanganyifu kuhusu mambo ya uovu yanayoweza kutujia ikiwa watu watatulaani. Hakuna lolote linaloweza kutudhuru iwapo tunafuata yaliyo mema (1 Petro 3:13). Hayo ni marejeo yaliyo adimu kuhusu laana katika Agano Jipya ambamo Yesu Kristo mwenyewe aliyatoa. Kwa hakika Biblia inacho kitu cha tofauti na cha muhimu inachoweza kutufundisha. Ni kumbukumbu za pekee ndani ya Agano Jipya ambazo hutuelekeza cha kufanya na kuelezea pia kwamba tabia zetu zinapaswa kuwaje pale mtu atakapotulaani! Sasa kwa nini basi walimu hawa wanayapinga na kuyakataa yale ambayo Yesu mwenyewe anayasema kuhusu njia ya kuifuata pale mtu atakapolaaniwa? Kwa nini basi wao hawayafundishi yale ambayo Yesu Kristo anayafundisha?

Hivyo ndivyo ilivyo katika Yakobo 3:7–10, na Ufunuo 22:3. Huo ndio “Ushuhuda” wao wanaoutumia kutoka katika Agano Jipya ili kuonyesha kwamba wakristo leo wanaweza kuwa na wamo katika vifungo, giza au magonjwa – eti hiyo yote ni kwa sababu ya laana zilizopita! Na jinsi gani tunapaswa kufuatilia au kugundua laana hizo zilizopita, ambapo inaweza kwa kufanya hivyo kutupeleka nyuma zaidi ya miaka mia moja iliyopita?
Mpendwa msomaji, unafikiriaje? Je, na wewe unaamini kuwa mistari hii inatufundisha mambo hayo wayasemayo? Je, hayo ndiyo mafundisho ya Yesu au Mitume? Je, unaweza kuyapata mafundisho hayo mahala popote pale katika Agano Jipya? Ni jambo la kufurahisha kuona kuwa, bila shaka kitabu maarufu sana na chenye kuvutia na kinavyoshabikia kasoro hizi hapa ulimwenguni pote, hakijaribu hata kidogo kutoa ushahidi wowote ule katika Agano Jipya ili kuunga mkono mafundisho hayo.

TAARIFA YA UBADILISHAJI WA JINA LA BLOGU HII,KUTOKA MWAKASEGE INJILI NAKUWA HUDUMA YA UKOMBOZI GOSPLE NA ANUANI YAKE KUTOKA www.mwakasegeinjili.blogspot.com na kuwa www.ukombozig.blogspot.com

Mkurugenzi wa kampuni ya HAKI LEO ambayo ndiyo inamiliki blogu hii Oscar Samba anayo furaha kuwatangazia kwamaba siku chache zijaro jina na anuani ya blogu hii vitabadilika kama ilivyo ainishwa hapo juu.

Sababu kuu ya mabadiliko hayo  inatokana na uanzishwaji wa huduma mpya itakayokuwa chini yake naitaitwa UKOMBOZI GOSPLE.

Maono yake na malengo yake yatakuwa hatharani rasimi baada ya uzinduzi wa huduma hiyo utakao fanyika siku hiyo ya ubadilishaji wa jina hili.

Pia anaomba radhi kwa usumbufu utakao jitokeza,na tafadhali upatapo tangazo hili mtaarifu na mwenzako.

Jumatatu, 12 Mei 2014

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe;JEHANUM YA MOTO


Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org
Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO LA 6: JEHANUM YA MOTO
Yesu Kristo anatufundisha waziwazi kuhusu Jehanum ya moto, akituonya kumwogopa Mungu mwenye uwezo wa kututupa Jehanum. Anaendelea kutuonya kwamba, ni heri kukubali lolote lile litupate kuliko kwenda kwenye mateso makali ya Jehanum (LUKA 12:5, MATHAYO 5:22, 29-30). Maandiko pia yanaendelea kusisitiza kwa msisitizo mkubwa kwamba, ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai na kutupwa katika Jehanum ya moto (WAEBRANIA 10:26-27, 31). Jehanum hii ya moto inaitwa pia kuzimu (ZABURI 9:17) na tena inaitwa Tofeni (ISAYA 30:33). Hatupaswi kulipuuza jambo hili na kulifanya juu juu tu. Kwa sababu hii, leo, tutajifunza kwa undani kuhusu Jehanum ya moto, na tutaligawa somo letu katika vipengele vinne:-

(1) HUKUMU BAADA TU YA KUFA

(2) JEHANUM YA MOTO IKO WAP?

(3) HALI HALISI YA JEHANUM NA WALE WALIOKO HUKO

(4) JINSI YA KUIKWEPA JEHANUM YA MOTO

( 1 ). HUKUMU BAADA YA KUFA

Biblia inaeleza waziwazi kwamba mtu anapokufa, sekunde ileile ya kufa kwake anakabiliwa na hukumu (WAEBRANIA 9:27). Watu wanaofundisha kinyume na kweli ya neno, hufundisha kwamba mtu anapokufa analala tu na hakuna lolote la hukumu ya mara moja. Wanatumia maandiko yanayozungumzia kulala kwa kuyatafsiri isivyo (MATHAYO 27:52; 1 WAKORINTHO 15:20; YOHANA 11:11-14 n.k ) na pia wanasema wafu hawajui lolote kwa kutumia maandiko kama MHUBIRI 9:5. Ilivyo ni kwamba kinachobaki kaburini ni mwili tu. Nafsi na roho ya mtu huondoka kwa kuvalishwa mwili mwingine ( 1WAKORINTHO 15:40 ). Mwili unaobaki kaburini ndiyo ambao umelala haujui lolote na hauna kumbukumbu, lakini pasipo mwili huo mtu atamwona Mungu ikiwa ameishi katika mapenzi yake(AYUBU 19:26). Mwili hubaki kaburini, lakini roho ya mtu huondoka (MHUBIRI 12:7). Ikiwa mtu ameishi katika mapenzi ya Mungu mara tu ya kufa huchukuliwa mbinguni na malaika kwa kutumia magari maalum ya mbinguni (LUKA 23:43; 16:22; 2WAFALME 2:11-12; ZABURI 68:17; WAEBRANIA 1:7, 14). Ikiwa ameishi katika dhambi hukumu yake huwa kutupwa katika Jehanum ya moto mara tu baada ya kufa (MITHALI 9:13-18; ISAYA 5:11-15; MITHALI 17:24-27).

( 2 ). JEHANUM YA MMOTO IKO WAPI?

Mtu anapokufa tu, huwa kwenye njia panda. Kila mmoja hupenda kwenda mbinguni, hata hivo ikiwa jina lake haliko katika kitabu cha uzima cha mbinguni, hulazimika kwenda Jehanum ya moto. Mtu anayetakiwa kwenda motoni huchachamaa na kukataa kwenda kwenye njia mbaya inayotisha ya motoni na hulazimika kukamatwa na kutupwa Jehanum (UFUNUO 19:20; 20:10). Mbinguni ni juu (mbingu ya tatu) lakini kuzimu au Jehanum ya moto ni chini (pande za chini za nchi) 2WAKORINTHO 12:1-4; ITHALI 15:24; ZABURI 63:9; EZEKIELI 31:14.

( 3 ). HALI HALISI YA JEHANUM NA WALE WALIOKO HUKO

Jehanum ya moto ni kuzimu au shimo kubwa na refu sana lililojaa moto. Moto huu huwashwa mfululizo kwa pumzi ya Bwana (ISAYA 14:15; 30:33). Moto ni mkali kuliko moto wowote tunaoufahamu duniani, uwe gesi, umeme, makaa yam awe au lolote jingine (WAEBRANIA 10:27). Moto huu ni mweusi unaosababisha giza na kufanya mtu awaone wenzake wachache tu wa karibu naye (MATHAYO 11-12; 22:13; 25:30 YUDA 1:6). Moto huu una uwezo wa kula na kutafuna, kwa hiyo huwatafuna au kuwala wale walioko motoni (KUMBUKUMBU LA TORATI 32:22; WAEBRANIA 10:36-27). Hata hivyo, kama jinsi ambavyo chumvi inavyozuia nyama kuharibika, moto humtafuna mtu lakini hamaliziki (MARKO 9:43-49). Ni moto wa milele (MATAYO 25:41). Mafundisho potofu ysnswafariji watu na kusema eti mtu ataunguzwa na moto na kutoweshwa au kupotea na kuangamia kabisa na ndiyo mwisho wake. Wanatumia maandiko kama MATHAYO 10:28 ( kuangamizwa ) na YOHANA 3:16 ( kupotea ). Kuangamia hakumaanishi kualizika kabisa (ESTA 4:16). Kondoo akipotea haimaanishi hayupo kabisa ila ametengwa na mchungaji (angalia ISAYA 57:1-3). Vilevile neno “kuharibu” linapotumika kuhusiana na adhabu ya milele halina maana ya kufanya kitu kisiwepo, bali ni la kuzdhibu vikali ( 1WAKORINTHO 3:16-17 ). Waalimu hawa wa uongo hufundisha pia kwamba ati watu watatoweshwa kama moshi baada kwa kuunguzwa kwa kutumia ZABURI 37:20. Kutoweshwa hapa ni kutenganishwa mbali na Mungu. Moto wa milele, huambatana na madini yanayoitwa kiberiti (lugha ya kitaalam, “sulphur”). Madini haya yakiwaka huwa kama mpira na hutoa harufu kama ya mayai yaliyooza. Harufu ya namna hii inafunika kuzimu yote. Siyo hayo tu, katika moto huu wamo funza maalum ambao huwatafuna watu na kufanya matundu mengi katika miili yao wakiingia na kutoka. Hii hufanya sura zao kuwa mbaya mno kama madude tu! (ISAYA 14:11; MARKO 9:43-49; ISAYA 66:24). Jehanum ya moto, huitwa pia mauti ya pili(UFUNUO 21:8). Uchungu wa mauti unaompata mtu anapokufa, huwa juu ya mtu motoni, milele na milele (UFUNUO 20:10). Watu walioko motoni hujawa wakati wote na vilio na tena husaga meno yao kama mtu anayeona baridi kali MATHAYO 8:12). Kuzimu, urikalo ni pigo lif urikalo ambalo huwachukua wenye dhambi asubuhi, mchana na usiku (ISAYA 28:15, 18-19). Walioko motoni wanajifahamu, na kuwakumbuka wenzao waliowaacha duniani na tena hutoa ndimi zao nje wakitamani maji kidogo kupoza ulimi (LUKA 16:19-24). Juu ya yote hayo, katika vilio vyao, humwomba Mungu awahurumie na kuwasamehe lakini Yeye amekwishasema, “Nami jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma”(EZEKIELI9:10;8:18).

USEMI NA FIKRA ZA WALE WALIOKO MOTONI

Watu walioko motoni hutamani mtu mmoja kati yao aje awashuhudie ndugu zao ili wayoache dhambi na kukwepa mateso yao (LUKA 16:27-31). Wale walioko huko wajiopata mafundisho haya kabla, husema, “Jinsi nilivyochukia maonyo, na na moyo wangu ukadharau kukemewa; wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu, wala sikuwategea sikio langu walionifundisha (MITHALI 5:11-13)” Wakimwona yeyote anayejiunga nao, humwambia, “Jew ewe umekuwa dhaifu kama sisi! Wewe nawe ummekuwa kama sisi!” ( ISAYA 14:9-10).

WALIO MBINGUNI HUPEWA NAFASI YA KUWACHUNGULIA

Walioko mbinguni watatoka kidogo kuwaangalia (ISAYA 66:24) ila hawatakuwa na machozi yoyote juu yao.

TOFAUTI KATI YA JEHANUM YA MOTO NA ZIWA LA MOTO

Jehanum ya moto ni tofauti na ziwa la moto linalotajwa katika UFUNUO 20:14-15; 21:8 kwa jinsi ileile mbingu ya sasa ilivyo tofauti na mbingu mpya inayotajwa katika UFUNUO 21:1. Ziwa la moto kwa sasa halina mkazi ndani yake. Watakaokuwa wa kwanza kuingia humo watakuwa mnyama (Mpinga Kristo)na nabii wa uongo (UFUNUO 19:20). Kisha atafuata ibilisi ambaye atatupwa humo baada ya vita ya Gogu na Magogu (UFUNUO 20:7-10). Baada ya hapo kutafuata hukumu ya jiti cha enzi, kikubwa cheupe. Hukumu hii itatolewa baada ya ufufuo wa pili au ufufuo wa hukumu ambao utawafufua walioko Jehanum ya moto.Baada ya hawa kuelezwa kwa nini wamehukumiwa adhabu ya matesoya milele, ndipo watakapotupwa katika ziwa la moto. Mateso yaliyoko ziwa la moto ni zaidi sana kuliko mateso ya Jehanum ya moto. Ni kama Jehanum walikuwa mahabusu na sasa wanapelekwa gerezani. Kama mbingu mpya itakavyokuwa nzuri zaidi kuliko mbingu ya sasa, vivyo ziwa la moto litakuwa na mateso yaliyokithiri kuliko Jehanum ya moto.

( 4 ). JINSI YA KUIKWEPA JEHANUM YA MOTO

1 .Kuungama dhambi na kuziacha (MITHALI 28:13).

2. Kulishika Neno la Mungu kwa kufanya maagizo yote ya Mungu na kuwakata wafariji wenye kutaabisha wanaosema kufanya hili na lile siyo lazima ( YOHANA 8:51; ZABURI 119:6; AYUBU 16:1-2 ).

3. Kutohesabu sheria kuwa kutu kigeni. Kukubali kuongozwa na sheria ya Kristo. Hakuna mwanafunzi asiyeishi kwa sheria ( HOSEA 8:12; WAGALATIA 6:2; ISAYA 8:16 ).

4. Kuwa mtakatifu na kutoifuatisha namna ya dunia hii katika mavazi, usemi, matendo n.k. ( WAEBRANIA 12:14; WARUMI 12:2; YAKOBO 4:4; 1YOHANA 2:15-17 )

JE! WEWE NAWE UMEKUWA DHAIFU KAMA SISI!

ISAYA 14:9-10
Masomo ya matukio ya mwisho wa Dunia. Unaweza kuingia kwenye link ya kila somo.
1. KUNYAKULIWA KWA KANISA
https://davidcarol719.wordpress.com/2013/01/02/kunyakuliwa-kwa-kanisa/
2. DHIKI KUBWA
https://davidcarol719.wordpress.com/dhiki-kubwa/
3. TAJI KWA WATAKATIFU NA HARUSI YA MWANAKONDOO
https://davidcarol719.wordpress.com/2013/02/10/taji-kwa-watakatifu-na-harusi- ya-mwanakondoo/
4. KUJA KWA YESU KRISTO MARA YA PILI DUNIANI NA VITA VYA HAR-MAGEDONI
https://davidcarol719.wordpress.com/2013/02/10/kuja-kwa-yesu-kristo-mara-ya-pili-duniani-na-vita-ya-har-magedoni/
5. MIAKA 1,000 YA UTAWALA WA YESU KRISTO DUNIANI NA VITA VYA GOGU NA MAGOGU
https://davidcarol719.wordpress.com/miaka-1000-ya-utawala-wa-yesu-kristo-duniani-na-vita-vya-gogu-na-magogu/
6. UFUFU WA WAFU
https://davidcarol719.wordpress.com/187-2/
7. JEHANUM YA MOTO
https://davidcarol719.wordpress.com/jehanum-ya-moto/
8. KITI CHA ENZI KIKUBWA CHEUPE CHA HUKUMU
https://davidcarol719.wordpress.com/229-2/
9. MBINGU MPYA NA NCHI MPYA
https://davidcarol719.wordpress.com/mbingu-mpya-na-nchi-mpya/

. . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

Zipo Baraka nyingi kwa yeyote atakaye “share “ ujumbe huu katika Facebook,Twitter n.k, kwa ndugu, jamaaa na marifiki ili nao wapate nafasi ya kusoma ujumbe huu na kubarikiwa kama wewe ulivyo barikiwa. Kwasababu hii share ujumbe huu kwa kubonyeza neno“ share” lililopo chini ya “note” hii, kwa kufanya hivyo ujumbe huu utafika kwa watu wengi. Hakika, Baraka za Mungu zitakuwa nawe.

UBARIKIWE NA BWANA YESU!!!

ISRAEL HOUGHTON KUIMBA NCHINI UGANDA MWEZI UJAO, HAKUNA KIINGILIO


Watoto Children Choir namba 66 wakiimba kanisani kwao kabla ya kuelekea nchini Australia kwa ziara wiki mbili zilizopita.
Nyota wa muziki wa injili duniani Israel Houghton kutoka nchini Marekani anatarajiwa kuwa mwimbaji mwalikwa katika sherehe za kutimiza miaka 30 ya huduma ya kanisa la Watoto Uganda pamoja na miaka 20 ya huduma ya wanawake na watoto kupitia Watoto child care ministries zote zikiwa chini ya kanisa la Watoto ambalo umaarufu wake umetokana na kwaya ya Watoto children chini ya waanzilishi wa huduma hiyo Gary na Marilyn Skinner zitakazofanyika mwezi wa sita nchini

humo.

Israel na kundi lake la New breed wanatarajiwa kuimba siku ya alhamis tarehe 5 katika kanisa la Watoto west tukio ambalo halitakuwa na kiingilio lililopewa jina la 'Watoto Big Party'. Hii itakuwa si mara ya kwanza kwa mwimbaji huyo kuimba jukwaa moja na Watoto children choir ambao amekuwa akikutana nao sehemu mbalimbali. Mwimbaji huyo atakuwa nchini Uganda wiki moja baada ya kumaliza tamasha lake kubwa la uimbaji litakalofanyika jijini London nchini Uingereza tarehe 27 mwezi wa tano akiwa na kundi lake kamili.

Haya kwa wale wapenzi wa mwanamuziki huyo, ni kujipanga nauli ya kwenda na kurudi na sehemu ya kufikia bila kusahau chakula, onyesho halitakuwa na kiingilio.

Jumamosi, 10 Mei 2014

KAKOBE; UTHIBITISHO KUWA YESU NI MUNGU



Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO: UTHIBITISHO KUWA YESU NI MUNGU

Ni muhimu kufahamu kuwa Yesu Kristo ni Mungu.Ikiwa sisi ni wanafunzi wa Biblia tusiwe kama wengine wanaosema kuwa Yesu si Mungu.Kama huna moyo wa jiwe kama wengine waliotiwa upofu kiroho na kushindwa kuyaelewa maandiko,Je,unaamini kuwa Yesu ni Mungu? Yesu ni Mungu na ushahidi mwingi wa maandiko upo.

Somo hili lipo katika vipengere vinne vifuatavyo:-
KUTAJWA KWA YESU KRISTO NI MUNGU KATIKA BIBLIA.
SABABU SABA ZA KUTHIBITISHA KUWA NI MUNGU.
YESU ALIPOKUWA DUNIANI ALIKUWA EMANUELI MUNGU PAMOJA NASI.
YESU MWANA WA MUNGU.

Kipengere cha kwanza,

1.KUTAJWA KWA YESU KRISTO NI MUNGU KATIKA MAANDIKO.Hapa tunaona maandiko yakimtaja Yesu KriNasto waziwazi kuwa ni Mungu. Katika ( 1YOHANA. 5:20 ) “Nasi twajua kuwa Mwana wa Mungu amekwisha kuja,naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli,nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli.,yaani ndani ya Mwana wake Yesu Kristo.Huyu ndiyeMUNGU WA KWELI NAUZIMA WA MILELE”.. Pia katika ( YOHANA 20:26-29 ) “basi,baada ya siku nane,wanafunzi wake walikuwamo ndani tena,na Tomaso pamoja nao.Akaja Yesu na milango ilikuwa imefungwa,akasimama katikati,akasema,Amani iwe kwenu.Kisha akamwambia Tomasolete hapa kidole chako;uitazame mikono yangu;ulete na mkono wako uutie ubavuni mwangu;wala usiwe asiyeamini;bali aaminiye.Tomaso akajibu akamwambia,BWANA WANGU NA MUNGUWANGU..Yesu akamwambia,wewe kwa kuwa umeniona umesadiki;wa heri wale wasioona wakasadiki”.YESU KRISTO MUNGU MKUU, ( 1TITO 2:13 ) “Tukilitazamia tumaini lenye mafunuo yaKRISTO YESU MUNGU MKUU NA MWOKOZI WETU”.. YESU NI MUNGU aliyejifunua katika mwili (WARUMI 9:5 ) “Na katika hao alitoka KRISTO KWA NJIA YA MWILI,NDIYE ALIYE JUU YA MAMBO YOTE,MUNGU,MWENYE KUHIMIDIWA MILELE.AMINA..Mhalifu msalabani alimwita YESU Mungu na kumuomba YESU atakapokuwa katika ufalme wake amkumbuke mharifu huyo”. ( LUKA 23:39-43 ).Yesu hakukataa kuwa SI MUNGU bali alisema,Amini nakuambia leo hivi,utakuwa pamoja nami peponi.YESU NI MUNGU ALIYEKUJA DUNIANI .( WAFILIPI 2:5-6 ) “Ambaye yeye mwanzo alikuwan yuna namna ya Mungu,naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho,bali alijifanya kuwa hana utukufu,akatwaa namna ya mtumwa,akawa ana mfano wa wanadamu”.YESU alijita-mbulisha kwao kuwa ni MUNGU lakini hawakuelewa ( YOHANA 10:30-33 ) “Yesu akawajibu,kazi njema nyingi niwewaonyesha zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe? Wayahudi wakamjibu,kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe;bali kwa kukufuru,na kwasababu wewe uliye.mwanadamu wajifanya kuwa Mungu. Wayahudi walisema anakufuru kwa kusema kuwa yeye ni Mungu.Kimsingi Yesu ndiye Baba mwenyewe ndio maana anasema huwezi kumtenganisha na Baba; ukimwona yeye umemuona Baba. ( YOHANA 14:7-9 )


Katika mstari 8 na 9 Filipo akamwambia,Bwana,utuonyeshe Baba yatutosha. Yesu akamwambia,Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote,wewe usinijue,Filipo?

Ikiwa tu wanafunzi wa Yesu hatupaswi kubabaishwa na watu ambao hawana Roho wa Mungu.Mtu ambaye hana Roho wa Mungu hawezi kusema Yesu ni Mungu..Kwasababu hiyo,wanatumia akili tu.Hawa ni watu wa tabia ya asili ambao hawawezi kuyaelewa mambo ya kiroho ( 1WAKORITHO 2:14 ) “Basi,mwanadamu wa tabia ya asili hawezi kuyapokea mambo ya Roho wa Mungu;maana kwake ni upuuzi;wala hawezi kuyafahamu;kwa kuwa yanatambulikana kwa jinsi ya rohoni”

2.SABABU SABA ZA KUTHIBITISHA KUWA YESU NI MUNGU.

1.YESU NI MUUMBAJI.

Sifa ya kuumba niya Mungu peke yake ( YOHANA 1:3,14 ) “vyote vilifanyika kwa huyo;wala pasipo yeye hakukufanyika chochote kilichofanyika.Naye Neno alifanyika mwili;nasi tukauona utukufu wake kama utukufu wa Mwana pekee atokaye kwa Baba,amejaa neema na kweli”.Yesu aitwa Neno la Mungu (UFUNUO 19:13) “Kwahiyo Neno ni Mungu “(YOHANA 1:1).. na huyo ndiye aliyevifanya kuwako vitu vyote.Aliyeshuka kutoka juu na kufanyika mwili ni Yesu pekee aliyezaliwa na bikira Mariamu bila mbegu ya kiume kama inavyotokea kwa wanadamu wengine..Katika yeye vtu vyote viliumbwa (WAKOLOSAI 1:13-16) vinavyoonekana na visivyoonekana;vya mbinguni na vya duniani.Maandiko yako wazi kabisa kwa mtu mwenye Roho wa Mungu anaelewa kwa urahisi.

2.YESU ALIKUWEPO KABLA YA VITU VYOTE KUWEPO DUNIANI.

( WAKOLOSAI 1:17 ) “Naye amekuwako kabla ya vitu vyote;na vitu vyote hushikamana katika yeye”.(MIKA 5:2 ) “Basi,wewe Bethlehemu,Efrata,uliyemdogo kuwa miongoni mwa maelfu za Yuda;kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli;ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale;tangu milele“.

Yesu Kristo alikuwako kabla ya Nabii Ibrahimu kuwako(YOHANA 8:52-58). Watu walioambiwa maneno hayo n a Yesu mwenyewe wliokota mawe ili kumpiga Yesu wakisema kuwa anakufuru.Hawa ni watu wa tabia ya mwilini wanaotumia akili kupambanua mambo ya Mungu (mambo ya kiroho huwezi kuyatambua kwa akili maana Mungu ni Roho,( YOHANA 4:24)..YOHANA 17:5,24.WAEBRANIA 7:3 ).Imasema “hana baba,hana nana,hana wazazi,hana mwanzo wa siku zake,wala mwisho wa uhai wake,bali amefananishwa na Mwana wa Mungu;huyo adumu kuhani milele”.YESU ni alfa na omega,wakwanza nawa mwisho kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu yeye alikuwako (UFUNUO 22:13).Bali kwa damu ya thamani,kama ya mwana-kondoo asiye na ila,asiye na waa,yaani ya Kristo.Naye amejulikana kweli tangu zamani,kabla haijawekwa misingi ya dunia,lakini alifunuliwa mwisho wa zamani kwa ajili yetu ( 1PETRO 1:19-20 ).


3.YESU NI MTAWALA JUU YA YOTE. HII NI SIFA YA MUNGU PEKEE.

(YOHANA 330 ) “Yeye ajaye kutoka juu,huyo yu juu ya vyote.Yeye aliye wa dunia asili yake ni ya dunia,naye anena mambo ya duniani,yeye ajaye kutoka mbinguni yuu juu ya yote” . ( YOHANA 13:13 ) “Ninyi mwaniita ,Mwalimu, na Bwana;nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo“. ( WARUMI 14:9 ) “Maana Kristo alikufa akawa hai tena kwa sababu hii,awamiliki waliokufa na walio hai pia”. Nenokumiliki ni kutawala sifa ya kutawala ni sifa ya Mungu pekee.




4,YESU KRISTO NI ZAIDI YA MTU YEYOTE AU NABI AU MTUME YEYOTE YULE..

( WAEBRANIA 3:1-7 ) “Mustari 3 unasema,Kwa maana huyo amehesabiwa kuwa amestahiliutukufu zaidi kuliko Musa,kama vile yeye atengenezayenyumba alivyo na heshima zaidi ya hiyo nyumba”..Anayezungumziwa hapa ni Yesu Kristo Mungu muumbaji. YESU ,ameketi mkono wa kuume wa ukuu huko mbinguni (WAEBRANIA 1;3-4).

5,YESU NDIYE ATAKAYE HUKUMU WALIMWENGU (WATU) WOTE.

( ZABURI 58:11 ), ‘Hakika yuko Mungu anayetawala katika dunia“. (UFUNUO 18;8 ) “Kwasababu hiyo,mapigo yake yatakuja katika siku moja,mauti na huzuni na njaanaye atateketeza kabisa kwa moto.Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu“.Tene ndiye atakaye ihukumu Dunia yote “Tena Baba hamhukumu mtu ye yote,bali amempa Mwana (YESU) hukumu yote“.(MATHAYO 25:31-32 ) “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu (YESU) katika utukufu wake,namalaika watakatifu wote pamoja naye,ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake.Na mataifa yote yatakusanyika mbele zake,naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi” .(MATENDO 10:42 ) “Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudiaya kuwa huyu ndiye (Yesu) aliyeamriwa na Mungu awe mhukumu wa wahai na wafu” ( WARUMI 2:16 ) “Katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu,sawasawa na injili yangu,kwa Kristo Yesu“.( 2TIMOTHEO 4:1 ) “Nakuagiza mmbele za Mungu,na mbele za Kristo Yesu,atakayewahukumu waliohai na waliokufa;kwa kufunuliwa kwake na kwa ufalme wake’.

6.YESU HABADILIKI TENE HANA KIGEUGEU. {WAEBRANIA 13:8} “Yesu Kristo ni yeye yule jana na leohata milele“. ( WAEBRANIA 1:10-12 ) “Wewe ,Bwana,hapo mwanzo uliitia misingi ya nchi.Na mbingu ni kazi ya mikono yako;Hizo zitaharibika,lakini wewe unadumu;Nazo zote zinachakaa kama nguo,Na kama mavazi,utazizinga,nazo zitabadilika;Lakini wewe u yeye yule,na miaka yako haitakoma“. ( MALAKI 3:6 ) “Kwa kuwa mimi,Bwana,sina kigeugeu” ( ZABURI 102:26-27 ) “Hizi zitaharibika,bali wewe utadumu;Naam,hizi zitachakaa kama nguo;na kama mavazi utazibadirisha,nazo zitabadilika.Lakini wewe U yeye yule;na miaka yako haitakoma“. ( YAKOBO 1:17 ) “Kwake hakuna kubadilika,wala kivulu cha kugeukageuka”.
YESU YUPO KILA MAHALI ,KOTEKOTE DUNIANI.

( MATHAYO 18:20 ) “Kwa kuwa walipo wawili watatu,wamekusanyika kwa jina langu,mimi nipo papo hapo katikati yao”. Mwenye uwezo wa kukaa mahali pote ni Mungu.
YESU ALIPOKUWA DUNIANI ALIKUWA EMANUELI(MUNGU PAMOJA NA WANADAMU).

( MATHAYO 1:23-25 ) “Tazama; bikra atachukua mimba; naye atazaa mwana;nao watamwita jina lakeEmanueli; yaani ,Mungu pamoja nasi”.Tabia ya Yesu inaonyesha kuwa kama mwanadamu,kuzaliwa kwake kwa uwezo wa Roho mtakatifu.Hapa tunaona jinsi alivyo na uwezo wa tofauti na wanadamu akiwa anafahamu mambo yote kabla akiwa duniani..Yeye pia ajua yote yaliyomo ndani ya moyo wa mwanadamu (YOHANA 6:64,YOHANA 13:1,YOHANA 13:11,YOHANA 18:4,YOHANA 19:28).Tena Yesu alitabiri kabla jambo kutokea,pia alijitabiria mwenyewe yatakayomtokea mbele (MARKO 8:31,LUKA 9:22,LUKA 12:50,LUKA 22:37,LIKA 24:7-26,YOHANA 3:14,YOHANA 10:17-18,YOHANA 7:33,YOHANA 13:33,YOHANA 14:28,YOHANA 17:11,YOHANA 16:5,10,16,18 ).

Yesu aliabudiwa na kusujudiwa akiwa hapa duniani,Sifa ya kuabudiwa na kusujudiwa ni ya Mungu pekee hivyo Yesu ni Mungu.(MATHAYO 4:10).
Hata malaika wote wanamsujudia Yesu (UFUNUO 22:8-9,WAEBRANIA 1;6).
Ndiyo maana Yesu alisujudiwa akiwa mtoto mchanga alipozaliwa (MATHAYO 2:11,MATHAYO 14:33<LUKA 24;52).
Hata pepo wachafu walimsujudia Yesu (MARKO 5:2,6).

YESU ALIKUWA MWANADAMU ALIPOKUWA DUNIANI


A: Alizaliwa na bikira Mariamu(mwanadamu) ( LUKA 2:3-7 ).

B: Aliongezeka kimo ( LUKA 2:40-42-52)

C: Aliona njaa kama watu wengine ( LUKA 4:2)

D: Alilala usingizi kama binadamu wengine( LUKA 8:23)

E: Alikuwa na viungo kama binadamu( LUKA 24:36-40)

F: Alikula chakula ( LUKA 24:41-43)

G: Alichoka kama mwanadamu ( LUKA 4:6; WAEBRANIA 4:15 : 2:16-18
Msalabani alikufa kama mwanadamu hakufa kama Mungu ila alitupatanisha 1TIMOTHEO 2:5
Tunaona mama yake mariamu asema mimi ni mjakazi wa BWANA YESU ( LUKA 1:38-46-47)
Tunaona pia hapa wakati wamekusanyika kwa ajili ya maombi akiwemo na Mariamu waliomba kwa jina la BWANA wala si kwa jina la mariamu(MATENDO 1:13-15,1 YOHANA 4:1-2.

4:YESU MWANA WA MUNGU

Tunaona hapa biblia inatuambia YESU KRISTO ni mwana wa Mungu (YOHANA 20:30-31) hapa Yesu mwenyewe anasema yeye ni mwana wa Mungu ( MATHAYO 26:59-64; 16:13-17 ) , neno mwana linamzungumzia Yesu mwana siyo kuwa Mungu anazaa la hasha

Yesu anaitwa mwana wa Mungu kwa sababu alizaliwa kwa uweza wa R oho Mtakatifu. Hata sisi tumezaliwa kwa mara ya pili kwa roho tunapo mwamini Yesu Kristo hivyo tunahesabika kuwa ni wana wa Mungu.(WAFILIPI 2:14-15,YOHANA 1:12).Kwahiyo Yesu anapoitwa Mwana wa Mungu maana yake ni chapa ya Mungu (HUIOS) WAEBRANIA 1:1-3.Ndiyo maana hapa Yesu anawaambia wanafunzi wake,mumeniona mimi ;mumemuona Mungu,maana yake ndiyo hiyo (HUIOS) yaani chapa ya Mungu (YOHANA 14:7-9)
Tunaona hapa Yesu alisema Yeye ni Mwana wa Mungu (YOHANA 9:35-37)
Shetani naye anajua kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (MARKO 3:11,LUKA 4:41).
Malaika nao wanasema kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (LUKA 1:30-35)
Mungu mwenyewe anasema kuwa Yesu ni Mwanangu mpendwa (MATHAYO 3:17,MATHAYO 17:5 )

KUMKIRI YESU KRISTO KUWA NI BWAMNA

Matatizo yote yanayompinga Yesu Kristo kuwa si Mwana wa Mungu,inatokana mtu yeyote anakuwa hana roho wa Mungu (1yohana 4:15) na Mungu hayuko ndani ya mioyo yao (1YOHANA 2:23,LUKA 10:16)ndiyo maana maandiko matakatifu ya Mungu yanasema asiyemwamini Mwana hana uzima wz milele,hiyo adhabu ya milele inamkalia (YOHANA 5:23,YOHANA 3:36,YOHANA 5:11-13) Kwahiyo wanaomkataa Yesu Mwana wa Mungu hawawezi kushinda dhambi.Huwezi kushinda dhambi kama huamini kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu (1YOHANA 5:4-5,YOHANA 1:12).Ndiyo maana mtu mwenye dini tu hawezi kushinda dhambi kwasababu hajampokea Yesu Mwana wa Mungu (YOHANA 1:12) Wote wanaompokea wanapewa uwezo wa kushinda dhambi.Ni rahisi kuthibitisha ukweli wa maneno haya; wewe muangalie mtu yeyeyote wa dini tu bila Yesu,hana uwezo wa kushinda dhambi.Ni watukanaji,wazinzi,wenye tama n.k ingawa sala zao ni nyingi na ndefu lakini haziwezi kuwasaidia kushinda dhambi.Ni muhimu kufahamu kuwa ni Yesu peke yake aliyeishi duniani bila kutenda dhambi (WAEBRANIA 4:15).Hakuna wokovu katika mwingine (MATENDO 4:12).Hakuna uwezekano kwa mtu ambae hajamkiri Yesu Kristo kuingia mbinguni (YOHANA 14:6).Yesu ni njia na kweli n a nuzima………………………………………………………………………..

………………………………………………………………………………………………………..

Ni sifa ipi ya kutuwezesha kuingia mbinguni? Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14). Ndani yake hakitaingia kamwe chochote kilicho kinyonge (UFUNUO WA YOHANA 21:27). Kinyonge ni kipi? Ni yule anayetenda dhambi. Huyu ni mtu asiyefaa, ni mnyonge! Je, wewe ni mtakatifu? Jibu ni la! Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini; hivyo wewe pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13; YOHANA 14:6). Je, uko tayari kutubu sasa ili upate rehema hii? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii ya toba kwa dhati kutoka moyoni; “Mungu Baba asante kwa ujumbe huu. Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi. Sistahili kuingia mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Kuanzia leo nataka niifuate njia ya Yesu Kristo. Bwana Yesu niwezeshe. Asante kwa kunisikia katika Jina la Yesu. Amen”. Mpendwa msomaji umekubaliwa kuingia mbinguni. Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu. MUNGU AKUBARIKI !!!