Jumanne, 10 Machi 2015

MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA ATUNUKIWA SHAHADA YA HESHIMA


Siku ya jumamosi iliyopita katika ukumbi mkubwa wa Blue Pearl uliopo ndani ya Ubungo Plaza jijini Dar es salaam kulishuhudiwa tukio la Askofu na mwanzilishi wa kanisa la Ufufuo na Uzima nchini Josephat Gwajima akitunukiwa shahada ya udaktari wa heshima ph.D katika thiolojia kwa mchango wake wa uanzilishaji kanisa hilo nchini.

Shahada hiyo ya heshima ilitolewa na chuo kikuu cha Omega Global University cha nchini Afrika ya kusini ambapo pia viongozi wengine walitunikiwa shahada hiyo tukio ambalo pia lilihudhuriwa na wachungaji na watumishi kutoka makanisa mbalimbali nchini pamoja na ndugu, jamaa na marafiki wa watunukiwa.








- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/03/mchungaji-josephat-gwajima-atunukiwa.html#sthash.qjJr3GVb.dpuf

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni