Ijumaa, 26 Mei 2017

NJOO KWA YESU.

   Na Mtumishi Oscar Samba
Yamkini umekuwa ukisumbuka ama kuangaika kutokana na mambo kadha  wakadha kukusumbua maishani mwako ikiwemo tabia usizozipenda ama masumbufu ya kimaisha. Wangu wito ninakutaka uje kwa Yesu ili akusaidiye ama akuokowe na taabu hizo.

Huyu Yesu ninayemtaja mbele yako amewawezesha wengi kutoka katika adha kama hizo, wapo waliokuwa wezi akawaokoa, akiwemo yule mwizi pale msalabani, makahaba, akiwemo Rahabau. (Waebrania11:31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani )

 

Na wewe mkaribishe Yesu Kristo leo moyoni mwako kwa amani ili akuokowe na kisha kukutoa katika hayo maangamivu ya kudharauliwa au kutengwa pia kuwa hatarini kupata magonjwa kama UKIMWI na madhara kama yakifo ama kubaguliwa daima.

 

Yesu huyu aliyemtoa Paulo Mtume aliyeitwa Sauli kwenye tabia ya uwaji anaweza kukusaidi na wewe. Natumai hivi sasa upo tayari kuokoka ili Yesu awe Msaada wako sasa.

Kama ndio Fwatisha maneno haya kwa Imani’ Sema BWANA YESU, NINAKIRI, YAKWAMBA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA WEWE NI MUNGU NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, INGIA SASA NDANI YANGU NA UNIOKOWE. AMENI.

Hongera kwa kuokoka natafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

MAWASILIANO: SIMU +255 759 859 287. WEB: www.mwanakondooinjili.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni