Jumanne, 30 Mei 2017

YESU ANAKUJA.

 Na Mtumishi Oscar Samba.
(MWANAKONDOO Ministry)
Ni kweli ndugu yangu Ujio wa Yesu Kristo huu karibu mno na anakuja ili kuuhukumu ulimwengu hali itakayotoa maamuzi ama hatima ya maisha yako. Kama utaenda mbinguni ama Jehanamu ya Moto.

Kumbuka waendao mbinguni ni wale waliomwamini kama Bwana na mwokozi wa Maisha yao. Na kama hauja fanya hivyo ni wangu wito kumua hivyo sasa kwani ukifa hutakuwa na uamuzi katika hilo tena.
Warumi 10:9 Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.

10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.

Jumatatu, 29 Mei 2017

UHAKIKA BAADA YA KUFA.

Na Mtumishi Oscar Samba.

(MWANAKONDOO Ministry)

Ni jambo jema kuwa na uhakika wa maisha utakayo ishi ama sehemu utakayoenda mara baada ya kufa. Na uhakika huo unatokana na wewe jinsi ulivyo amua kuyaishi maisha unayoishi hivi sasa.
Maandiko yanasema wazi ya kwamba mara baada ya kufa ni hukumu, ikiwa na maana huwezi kutubu baada ya kufa ama hakuna atakayekuamulia mahali pakwenda mara baada ya kifo chako nikiwa na maana ya kwama hata ndugu zako wangekupenda na kukuombea kwa jinsi gani bado isingalikupa tiketi ya kubadilishiwa maisha ama sehemu upaswapo kwenda.

NINA MANTIKI YA KWAMBA, UWAMUZI WA UTAENDA WAPI UNAFANYIKA UNGALI HAPA DUNIANI NA SIO BAADA YA KUTOWEKA AMA KUNYAKULIWA. USIKUBALI KUDANGANYWA NA WIMBI LA UONGO WA MCHANA YA KWAMBA ETI UTAOKOKA MARA BAADA YA KUFA, AU UTATUBU UKIFA. HUO NI UWONGO WALA BIBILIA HAIJASADIFU JAMBO HILO.

Ni yangu rai kukutaka leo kuwamua mahali utakapo kwenda, Na kumbuka kuwa njia zipo mbili. 1. Kwanza ni ile ikupelekayo mbinguni na njia hiyo ni kumuamini Yesu. 2 Ni

MKIMBILIE YESU.


Na Mtumishi Oscar Samba
 (MWANAKONDOO Ministry)
Haijalishi unakumbana na jambo gani, ama unaishi maisha ya aina gani,? Jamii uliyonayo inakuheshimu ama kukudharau. Ila ujumbe ambao Mungu amenipa siku ya leo ni huu; MKIMBILIYE YEYE.

Ukifika kwa Yesu kila kinachokusumbua kitakoma, magonjwa, mateso ya kimaisha, ugumu wa kiuchumi, ndoa kusumbua, taabu za kukataliwa na kutengwa na ndugu. Ama ni tabia za ukahaba, umalaya, wizi ulevi na hata ile ambayo hakuna nayeijua na nivigumu kumwambia mtu mwingine yeyote na mimi siwezi kuitaja hapa maana kimaadili sio vyema.
Katika hayo yote wewe mwendee YESU naye atakusaidia maana amesaidia wengi ikiwemo yule mwanamke aliyeonekana najisi kwa kunuka damu za mwezi na zilimtoka kwa muda wa miaka 12.

Jumamosi, 27 Mei 2017

YESU ANAKUPENDA





Na Mtumishi Oscar Samba.
Wanadamu wanaweza kukuchukia, kukutenga, kukubagua, kukudharau na hata kukunyanyapaa ila huyu YESU hawezi kukutenda hayo badala yake ni wa Upendo daima.

 

Hajui kumchukiwa mtu, hata kama ni Kahaba, Mlevi, Mwizi, Mtukanaji, jamii inamuona kama Kichaa ama aliyechanganyikiwa na Maisha ama kurukwa na Akili.

Ijumaa, 26 Mei 2017

NJOO KWA YESU.

   Na Mtumishi Oscar Samba
Yamkini umekuwa ukisumbuka ama kuangaika kutokana na mambo kadha  wakadha kukusumbua maishani mwako ikiwemo tabia usizozipenda ama masumbufu ya kimaisha. Wangu wito ninakutaka uje kwa Yesu ili akusaidiye ama akuokowe na taabu hizo.

Huyu Yesu ninayemtaja mbele yako amewawezesha wengi kutoka katika adha kama hizo, wapo waliokuwa wezi akawaokoa, akiwemo yule mwizi pale msalabani, makahaba, akiwemo Rahabau. (Waebrania11:31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani )

 

Na wewe mkaribishe Yesu Kristo leo moyoni mwako kwa amani ili akuokowe na kisha kukutoa katika hayo maangamivu ya kudharauliwa au kutengwa pia kuwa hatarini kupata magonjwa kama UKIMWI na madhara kama yakifo ama kubaguliwa daima.

 

Yesu huyu aliyemtoa Paulo Mtume aliyeitwa Sauli kwenye tabia ya uwaji anaweza kukusaidi na wewe. Natumai hivi sasa upo tayari kuokoka ili Yesu awe Msaada wako sasa.

Kama ndio Fwatisha maneno haya kwa Imani’ Sema BWANA YESU, NINAKIRI, YAKWAMBA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NA WEWE NI MUNGU NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, INGIA SASA NDANI YANGU NA UNIOKOWE. AMENI.

Hongera kwa kuokoka natafuta kanisa la watu waliokoka ukasali hapo.

MAWASILIANO: SIMU +255 759 859 287. WEB: www.mwanakondooinjili.blogspot.com