Jumamosi, 10 Mei 2014

KAKOBE; YANIPASA NIFANYE NINI NIPATE KUOKOKA?

Neno la Uzima kutoka kwa Askofu Zachary Kakobe

Tovuti : www.bishopzacharykakobe.org

Facebook : www.facebook.com/bishopkakobeministries

Youtube : www.youtube.com/user/bishopkakobe

SOMO LA MAKANISA YA NYUMBANI

SOMO LA 111 : YANIPASA NIFANYE NINI NIPATE KUOKOKA?

NENO LA MSINGI:

MATENDO YA MITUME 16:30, 32

“Kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, YANIPASA NIFANYE NINI NIPATE KUOKOKA? Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake”.

<><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><><

W


atu waliookoka katika Kanisa la Kwanza lililokuwa linaongozwa na Mitume, walijua sana jinsi ya kumweleza mtu maana ya wokovu hata yeye naye akaokolewa. Katika Neno hili la msingi, tunaona mtu mmoja akiuliza afanye nini apate kuokoka, na hapohapo anaambiwa neno la Bwana na kuelewa analopaswa kulifanya. Watu wote tuliookoka, ni wajibu wetu kuwaambia watu wote neno la Bwana linalohusu wokovu ili yamkini wote wapate kuokolewa. Jambo la huzuni ni kwamba watu wengi waliookoka, hawawezi kumweleza mtu mwingine neno la BWANA hata akaelewa, na yeye akaokolewa. Kanisa la Mungu halipaswi kuwa hivi na kuwaacha wengi wakiangamia! Basi, ni makusudi ya somo la leo la Kanisa la Nyumbani, kujifunza hatua kwa hatua yanayotupasa kufahamu katika kumwambia mtu neno la BWANA hata na yeye aokolewe. Ikiwa wewe uliyehudhuria leo katika Kanisa la Nyumbani hujaokolewa basi unapokuwa unajifunza somo hili hujaokolewa basi ni siku yako pia kuokolewa baada ya kufahamu yote yanayokupasa kufahamu na kuyafanya.

A: NINI MAANA YA NENO “KUOKOKA” AU “KUOKOLEWA?“

Kuokoka au kuokolewa, ni kunusurishwa, kuopolewa, kusalimishwa au kuponywa kutoka katika maafa makubwa yaliyo dhahiri kabisa kukupata. Inaweza ikawa kuponywa kutoka katika hatari ya kifo adhabu kali au madhara yoyote makubwa yaliyo dhahiri. Katika hali ya kukosa matumaini ya kukwepa maafa hayo yaliyo dhahiri, inapotokea ghafla njia ya kusalimika hapo inasemekana umeokoka.

ANGALIA MIFANO KATIKA BIBLIA:

Baada ya Yusufu kuuzwa na ndugu zake na kupelekwa kuwa mtumwa huko Misri,

ilitokea njaa kubwa sana katika ulimwengu wote wa wakati huo. Watu wengi mno walikufa kwa kukosa chakula, na kulikuwa hakuna matumaini. Ndugu zake Yusufu nao walikuwa katika hatari ya kifo. Kabla ya njaa, huko Misri Yusufu kwa uwezo wa ajabu wa Mungu, aliaminiwa na kuwa Waziri Mkuu wa nchi ya Misri na akatumiwa na Mungu kuhifadhi chakula kingi ambacho hatimaye, kilitumika kuwaokoa ndugu zake katika maafa ya kufa kwa njaa.

MWANZO 45: 5 – 7:

“Basi sasa, msihuzunike, wala msiudhike nafsi, kwa kuniuza huku; maana Mungu alinipeleka mbele yenu kuhifadhi maisha ya watu. Maana miaka hii miwili njaa imekuwa katika nchi, na iko tena miaka mitano isiyo na kulima wala kuvuna. Mungu alinipeleka mbele yenu kuwahifadhia masazo katika nchi,NA KUWAOKOA NINYI KWA WOKOVU MKUU“.

Daudi akiwa katika hali ya hatari anaelezea juu ya hali ya mtu anayehitajika kuokolewa mtu ambaye yuko katika hatari ya kufa baada ya kuzama katika matope mengi na maji yakiwa yamefika nafsini mwake.

ZABURI 69:1 – 2:

“Ee Mungu, UNIOKOE, maana maji yamefika mpaka nafsini mwangu. Ninazama katika matope mengi, pasipowezekana kusimama. Nimefika penye maji ya vilindi, mkondo wa maji unanigharikisha.”

Wakati wa Nuhu, Mungu akiwa amechukizwa na dhambi za watu wa wakati ule, aliwaonya watu juu ya maafa yatakayokuja, kuwaangamiza wote wasiomtii Mungu. Watu wote wakapuuza ujumbe huo, isipokuwa Nuhu aliyetii na kuunda Safina iliyotumika kumwokoa yeye na watu wa nyumba yake kutoka katika maafa ya kufa kwa gharika kuu. Watu wote walikufa kutokana na gharika hiyo isipokuwa Nuhu na wenzake saba waliookolewa katika maafa hayo.

WAEBRANIA 11:7:

“Kwa Imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu aliunda safina, APATE KUOKOA NYUMBA YAKE”.

B: MAISHA YA BAADAYE YA MTU MWENYE DHAMBI:

Mtu yeyote mwenye dhambi lazima atapata adhabu ya milele. Adhabu yake inaitwa MAUTI YA PILI auMAUTI YA MILELE ambayo ni kutupwa motoni na kuteswa milele. Hakuna mwenye dhambi atakayekwepa adhabu. Kila mmoja atapata mshahara huu wa dhambi, mauti ya milele au kutupwa Jehanum ya moto.

MITHALI 11:19 – 21:

“——- Afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe—— Hakika, mtu mwovu hatakosa adhabu——-”.

EZEKIELI 18:4, 20:

“—-Roho itendayo dhambi itakufa————-”.

WARUMI 6:25:

“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti.”

UFUNUO 21:8:

“Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao, ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo MAUTI YA PILI.”

Hakuna mtu yeyote mwenye dhambi yaani asiyekuwa na haki mbele za Mungu atakayeokoka katika maangamizo hayo. Kwa sasa mtu mwenye dhambi anaona kwamba yuko salama na kwamba amani iko kwake, lakini ghafla uharibifu wake utamwijia.

1 WATHESALONIKE 5:3:

“Wakati wasemapo, kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla, kama vile uchungu umjiavyo mwenye mimba wala hakika hawataokolewa.”

ZABURI 119:155:

“Wokovu u mbali na wasio haki kwa maana hawajifunzi amri zako (na kuzitenda)”.

C. NI NANI MWENYE DHAMBI?

Jibu ni kwamba kila mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke, kutokana na asili ya Adamu, yuko miongoni mwa wenye dhambi. Wote wamefanya dhambi. Kwa mtu mmoja Adamu, dhambi iliingia ulimwenguni; na WATU WOTE wakahesabiwa kuwa wenye dhambi. Kutokana na kila mtu kuzaliwa akiwa na asili ya dhambi, kila mtu anatenda dhambi pia. Hivyo watu wote pamoja, na wewe, wanazaliwa katika dhambi na pia wote wanatenda dhambi.

MHUBIRI 7:20:

“Bila shaka hakuna mwanadamu mwenye haki hapa duniani, ambaye afanya mema, asifanye dhambi.”

ZABURI 53:3:

“Kila mtu amepotoka, wameoza wote pamoja, hakuna atendaye mema, La! hata mmoja.”

ISAYA 53:6:

“Sisi sote kama kondoo tumepotea, kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe———”.

WARUMI 3:23:

“Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.”

WARUMI 5:12:

“Kwa hiyo kama kwa mtu mmoja (Adamu) dhambi iliingia ulimwenguni na kwa dhambi hiyo mauti na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi”.

1 YOHANA 1:8, 10:

“Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu.”

Unaona basi! Kila mtu anakuwa mwenye dhambi kutokana na uzao wa Adamu. Kila mtu anazaliwa akiwa ana asili ya dhambi. Kama Adamu alivyofanya dhambi, wote tunazaliwa na dhambi ya asili.

KANISA LA KILUTHERI MWANZA LATOA TAMKO JUU YA BOMU KANISANI KWAO


Kanisa la Kilutheri jijini Mwanza.

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria (DMZV), limeitaka Serikali kuhakikisha inawatafuta watu waliohusika na tukio la bomu lililolipuka kanisani hapo juzi.Pia, limewataka Wakristo kuwa watulivu, wasiogope wala wasitishwe na mashambulizi hayo na kwamba wasilipize kisasi.

Akizungumza kwenye Kanisa la Imani Makongoro Misheni jana, Askofu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki Ziwa Victoria, Andrew Gulle alisema wanaamini shambulio hilo ni la kigaidi na kwamba, Serikali inapaswa kuchukua hatua ya kuwasaka wanaohusika “Kanisa tunaamini tukio hili linahusiana na ugaidi, umefika wakati Serikali ikachukua hatua za kuwasaka waliohusika ili sheria ifuate mkondo wake,” alisema Gulle.

Hata hivyo, wachambuzi wa masuala ya dini wanasema huenda tukio hilo linatokana na migogoro inayoendelea kanisani hapo kwa sababu tayari kuna baadhi ya waumini wamejitenga kwa kuanzisha kanisa lingine “Wasikwepe matatizo yao ya ndani, kuna askofu aliuawa kwa kupigwa tofali kutokana na migogoro, hivyo hata hili (tukio) litakuwa ni migogoro inayoendelea,” alisema mmoja wa waumini ambaye hakutaka kutajwa jina lake.
Askofu Gulle alikanusha kuwapo kwa migogoro kanisani hapo na kwamba, tukio hilo halihusiani na mgogoro wowote ndani ya Kanisa bali ni ugaidi.

Majeruhi aendelea vizuri

Hali ya majeruhi wa mlipuko wa bomu uliotokea kanisani hapo, Benadeta Alfred, imeelezwa kuendelea vizuri katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando alikolazwa. “Hali ya mgonjwa ni nzuri ukilinganisha na tulivyompokea kwani hata kuongea alikuwa hawezi, lakini hivi sasa anaweza kuongea japo kwa shida,” alisema Lema.

Ijumaa, 2 Mei 2014

Je, Biblia Ina Habari Sahihi Kuhusu Maisha ya Yesu?


Jibu la Biblia
Mwandishi wa Biblia, Luka, alisema hivi kuhusu masimulizi aliyoandika kuhusu maisha ya Yesu: “nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi.”—Luka 1:3.

Watu fulani wanadai kwamba masimulizi ya maisha ya Yesu yaliyoandikwa katika Vitabu vya Injili, yaani, maandishi ya watu walioishi wakati wake kama vile Mathayo, Marko, Luka, na Yohana, yalibadilishwa wakati fulani katika karne ya nne.

Hata hivyo, sehemu fulani muhimu ya Injili ya Yohana ilipatikana nchini Misri mwanzoni mwa karne ya 20. Sehemu hiyo inajulikana kamaPapyrus Rylands 457 (P52) na imehifadhiwa katika Maktaba ya John Rylands Library, huko Manchester, Uingereza. Ina kitabu cha Yohana 18:31-33, 37, 38 katika Biblia za leo.

Hii ndiyo sehemu ya zamani zaidi ya hati za Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Wasomi wengi wanaamini kwamba sehemu hiyo iliandikwa karibu mwaka wa 125 W.K., miaka 25hivi baada ya maandishi ya awali kuandikwa. Maandishi ya sehemu hii yanalingana kabisa na maandishi ya hati za baadaye.

Kwa Nini Yesu Anaitwa Mwana wa Mungu?

Jibu la Biblia
Mungu hakuwa na mke halisi ambaye walipata naye watoto. Lakini ndiye Muumba wa vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Kwa hiyo, Adamu, mwanadamu wa kwanza ambaye Mungu alimuumba, anaitwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Vilevile, Biblia inafundisha kwamba Yesu aliumbwa na Mungu. Hivyo, Yesu pia anaitwa “Mwana wa Mungu.”—Yohana 1:49.

Mungu alimuumba Yesu kabla ya kumuumba Adamu. Kumhusu Yesu, Mtume Paulo aliandika: “Yeye ndiye mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.” (Wakolosai 1:15) Maisha ya Yesu yalianza miaka mingi kabla ya kuzaliwa katika zizi huko Bethlehemu. Hata Biblia inasema kwamba “asili yake ni kutoka nyakati za kale, kutoka siku za wakati usio na kipimo.” (Mika 5:2) Kabla ya kuzaliwa akiwa mwanadamu hapa duniani Yesu, Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu, alikuwa kiumbe wa roho huko mbinguni. Yesu mwenyewe alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni.”—Yohana 6:38

FIKRA NJE YA BOKSI: BADILI CHANZO CHA TAARIFA

chanzo gosipe Kitaa
Na Fredy Msungu

UTANGULIZI
Katika maisha ya kila siku, kila mmoja kwa upande wake kuna mambo ambayo anayatarajia sana kama matokeo halisi ya kitu fulani aliwahi kupanga au kuwaza katika maisha yake.Japo kua matarajio hayo hua ni siri ya mtu binafsi lakini nina uhakika kwa asilimia nyingi sana kwamba kila mmoja wetu anamatarajio mazuri katika maisha yake.Pamoja na kua kila mmoja wetu anategemea matokeo mazuri (chanya) lakini kuna kitu cha kwanza kufanya ambacho hicho ndio huleta matokeo unayoyahitaji,Inawezekana ukawa na matarajio mazuri sana lakini kua na matarajio (imani juu ya kitu fulani)na mambo makuu na mazuri hiyo haimaanishi tayari umepata uhakika au tiketi ya kuyafikia matarajio hayona kuyafanya kua kitu harusi.Wapo watu wengi waliokua na ndoto kubwa (matarajio)lakini hawakuweza kufikia, Na hii ni kwasababu tu!Hawakutengeza mwanzo wao kuakisi matokeo ya kesho yao.Kua na wazo au tarajio zuri peke yake si ufunguo wa mafanikio kuyafikia malengo, kuna mambo ambayo kupitia kwayo hayo ndio huzaa matokeo chanya moja kati ya jambo la msingi sana kati ya hayo ni CHANZO CHA TAARIFA:
TAARIFA NI NINI?Taarifa ni ujumbe wowote unaokujia kwa njia tofauti tofauti...inaweza kua kwa :-
• Kuambiwa /kusimuliwa
• Kusikiliza
• Kusoma
• Kuona

Viko vitu vingi ambavyo vinaweza kua ni sababu ya wewe kupata taarifa, lakini hizo ni njia au vyanzo vichache ambavyo mara nyingi vimetumika sana kutoa taarifa au elimu ya kitu fulani. Kitu cha muhimu Sana hapa kujua ni kwamba taarifa ni taarifa Haijalishi ni taarifa nzuri au mbaya!Ukishaipokea kwa kupitia moja kati ya hizo njia nilizoziorodhesha basi tayari hiyo ni taarifa.Na kwa namna moja au nyingine tegemea kuathiriwa na ile taarifa ulioipokea.

LENGO LA TAARIFA NI NINI?Lengo kuu la taarifa hua ni kujuza, kuaminisha, Kuonya, kuelimisha na wakati mwingine kupotosha .Hayo yote ni malengo ya taarifa ambayo mara nyingi yanatokea kutokana na mtoaji taarifa anamlengo gani au mpokeaji wa hiyo taarifa amechagua kusikia nini au kumsikiliza nani.
Kitaalamu, kiuumbaji (kisayansi) moja kati ya kazi kubwa ya ubongo ni kupokea taarifa mbali mbali (kufikiri) Na huwezi kufikiri bilakua na kitu cha kukifikiria, Sasa hicho kitu cha kufikiri ndio hiyo taarifa ambayo inatokana na vile vyanzo nilivyoviorodhesha awali.

MUHIMU: Ninachotaka kukujuza hapa ni kwamba uwe unapenda au haupendi swala la kupokea taarifa kwako si la hiyari kwako, Ni lazima kuna taarifa ubongo wako utapokea tu! na baada ya ubongo kupokea taarifa ni lazima ubongo ufanye kazi ya kufikiri, na fikra hutokea kutokana na aina ya taarifa uliyoisikia na matokeo yeyote unayoyaona yametokea nje chanzo chake hua ni taarifa.Swala kupokea taarifa si hiyari lakini ni aina ipi ya taarifa umechagua kupokea hilo ni uchaguzi wako.

Kwa maneno machace tu hapa naweza kukujuza kwamba ......CHANZO SAHIHI CHA TAARIFA HULETA FIKRA SAHIHI....NA FIKRA SAHIHI HULETA MATOKEO SAHIHI.vivyo hivyo CHANZO KIBOVU (POTOFU) CHA TAARIFA HULETA FIKRA MBOVU NA FIKRA MBOVU HULETA MATOKEO MABOVU

JINSI TAARIFA INAVYOATHIRI MAAMUZI YAKO
Maamuzi ni chanzo kikubwa cha matokeo, Hakuna jambo lolote lilitokea bila mtu kufanya maamuzi ya kuliweka jambo katika vitendo, Wazo pekee halitoshi kuleta matokeo yanayoonekana ...maamuzi ni hatua inayosababisha tendo na tendo huleta matokeo lakini haya maamuzi yanaathiriwa sana na chanzo cha taarifa. (Warumi 10:17 Basi imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neon la kristo) Ukisoma Kwa umakini hapo utatambua kitu kikubwa sana. Ukifikia hatua ya kuamua kitu basi lazima kuna taarifa iliyokushawishi kukupelekea wewe kuamua.Imani ni matokeo tayari ambayo chanzo chake kimekuja kwa njia ya kusikia lakini chanzo cha taarifa hapa ni nini? Au kusikia kutoka kwenye chanzo gani cha taarifa? Hili ni swali kubwa ambalo unatakiwa kujiuliza.Kwa mujibu wa andiko hapo juu utaona kwamba kulisikia neno la kristo hicho ndo chanzo kikuu cha taaarifa.Sasa kama matokeo ya kuamini au imani hua ni kusikia jiadhari sana na nini unachagua kusikia kwani hicho ndicho huleta matokeo ya jambo.Unaweza ukawa unajiuliza sana kwanini mara nyingi katika safu hii nimetumia neno ‘UNACHAGUA KUSIKIA’?Kitu kikubwa ninaamini katika maisha hali yeyote ulionayo ni matokeo ya uchaguzi wako mwenyewe,kama ni umasikini au utajiri,kufaulu au kufeli,kushinda ama kushindwa hivi vitu vyote ni uchaguzi wa mtu binafsi.Hii inaweza ikakupa shida kidogo lakini nitakueleza kwanini imani yangu inanituma hivyo.

FIKRA TATA: 1
• Hakuna mtu aliezaliwa na kitu/mali /mafanikio... Inaweza ikakupa shida kuamini kwasababu kila siku unaona kuna watu mashuhuri/matajiri na wana watoto, utaniambia Fred wale si watu waliozaliwa na kuyakuta mafanikio tayari? Ni sawa lakini hebu tulia kidogo na fikiri hivi yule mtu wa kwanza kabisa ambae ndio mwenye hayo mafanikio ...Je nayeye hizo mali/mafanikio alizitoa wapi? Jibu ni rahisi sana hapa kwamba wakati wote tulikua katika hali sawa uwezo sawa na mazingira sawa kuna mtu mmoja ambae yeye aliamua kufikiri zaidi ya mipaka ya kawaida (fikra nje ya boksi) Matokeo ya kufikiri nje ya mipaka ni kufanya vitu nje ya mipaka na kufanya vitu nje ya mipaka ni kupata matokeo makubwa nje ya mipaka.Baada ya hayo yote sasa utofauti ndio unaanza kuonekana kwasababu yeye aliamua kulipa gharama na kutenda nje ya mipaka ni lazima matokeo yamtoe nje ya mipaka pia na ndio maana watu wenye uwezu wa juu na wasio na uwezo hawakai sehemu moja..Unaweza ukalahumu saaana lakini mfumo ndo umeamua hivyo aliwaza nje ya mipaka ataishi nje ya mipaka pia, Lakini wote mwanzo wetu ulikua sawa.

AMKA MAISHA NI UCHAGUZI.
KUNA UHUSIANO GANI KATI YA MALENGO/NDOTO NA TAARIFA?
Hili linaweza kua moja kati ya maswali ambayo umejiuliza sana toka ulipoanza kusoma safu hii, Kwamba mipango /ndoto ni yako wewe binafsi sasa taarifa inaingiaje hapa ama kuna uhusiano gani baina ya vitu hivi viwili?

Jibu: Ni kweli kwamba maisha ni yako wewe ndoto/mipango na maono uliyonayo ni vyako.Lakini kumbuka mpaka vitu hivyo vikatokee kuna mchakato fulani ambao ni lazima uupitie kama njia ya kuielekea hatma yako au kilele cha mafanikio yako.
Njia hizo ni:-
• Kujifunza/kupata uzoefu: Sehemu yeyote duniani kwenye sekta yeyote hakuna mtu ambaye amefanikiwa na akasema kwamba hakuna mtu yeyote mwenye mchango katika mafanikio yake, abadani si kweli.... mara zote hua kuna watu waliotutangulia (wenye uzoefu)ambao wamefanya vitu sawa na tunavyoviwaza wakafanikawa, watu hao husimama kama mifano/ushuhuda kwa vizazi vingine vijavyo ili kuyafikia malengo.Kama kumbu kumbu yako nzuri utakumbuka mwanzoni kabisa nilikuambia kwamba jitambue wewe ni nani na unataka nini ili uchague watu unaodhani wanafanana na wewe ili upate uzoefu(kujifunza toka kwao)Ili kuyafikia matokeo unayoyatarajia.Na uzoefu huo utaupata kwa njia ya kujifunza.

Kuna njia nyinginezo nyingi ambazo ni vyanzo vya taarifa, Na huu ndio uhusiano sasa kati ya ndoto yako/malengo/mipango na taarifa. Taarifa inaathiri Sana matokeo ya malengo yako kwasababu wakati wa kutendea kazi mawazo unazungukwa ka watu mbali mbali na pengine ili kufikia malengo itakuhitaji pia kuwatumia baadhi ya watu ili kutoboza upande wa pili na hii ndio sababu unatakiwa kua na chanzo sahihi cha taarifa ili usikie vitu sahihi.

UMECHAGUA FUNGU GANI LA TAARIFA?
Kama swala la kusikia! Watu wengi wanasikia.....Ila unasikia nini? Kutoka Kwa nani? Hapa ndio nataka kujenga hoja yangu Kwa upana kwasababu chochote ulichoamini mwanzo wake ulikua ni kusikia. Baada ya kusikia na kuamini maamuzi ya vitendo hufuata.Na hapa ndipo safari ya mafanikio au ya kufeli (kutofanikiwa)inaanza.Na hii inatokana umesikia taarifa gani kutoka kwenye chanzo gani uliochagua kuisikiliza na kuiamini.Ukisikia taarifa sahihi utaamua kwa jinnsi ilivyo sahihi ,Pia ukisikia kwa taarifa isiyo sahihi kutoka kwenye chanzo kisicho sahihi basi fikra na maamuzi yako pia hayatakua sahihi.Inawezekana kabisa ukaona ukuu ndani yako ukawa na mipango mikubwa tu , lakini kama utaruhusu masikio na fikra yako kupokea taarifa za kushindwa mara kwa mara, haijalishi una ndoto kubwa kiasi gani ukiruhusu taarifa za kushindwa tegemea kushindwa pia.

Kabla sijatoa mfano huu nikuweke sawa kwanza katika hili...Kwagu mimi kiwango cha utajiri wa mtu au mafanikio makubwa ya aina yeyote si kigezo kwamba Mungu ndio anatenda kazi au niamini Mungu kwasababu amefany litu fulani,Nimefika mahali pa kuelewa kua Mungu hua anabaki kua Mungu tu iwe ametenda unachotaka au hajatenda..(Mungu hapimwi kwa alichofanya anabaki kua Mungu kwasababu ndivyo alivyo) huo ni mtazamo wangu, Japo kua mimi siamini katika umasikini
Sasa mfano wangu ni huu..!Ukifanya tathinimi ya wale wachungaji ambao wao wanahubiri sana injili za aina moja unyonge (uhitaji) hebu jaribu kuangalia maisha yao na ya watu wanaowaongoza...hali zao kiuchumi (kimaisha)hua ni mbaya sana na wao hua wameridhika kabisa, Lakini si kwamba Mungu hawezi kufanya kitu au hawana Mungu hapana! Ila kwasababu ni kitu ambacho wanakisikia kwa sana,Hivyo inawajengea imani na imani inaleta matokeo ya walichokisia.Kwahiyo hili si swala la kumlaumu mtu ni swala la ufahamu tu...Baba wa upentecoste Nigeria Askofu mkuu Benson Idahosa enzi za uhai wake aliwahi kusema hivi ‘Ukihubiri sana juu ya habari ya kuzimu(moto) kuna hatari kubwa washirika wako wakaishia huko,Lakini ukihubiri sana juu ya habari za mbinguni kuna asilimia kubwa ya watu unaowaongoza kuiona mbingu(peponi)’.Kauli hii ilinigusa sana na imeakisi sana ujumbe wangu kwamba chanzo cha taarifa kikiwa kibaya mara kwa mara tegemea matokeo mabaya na pia ukijizoesha kusikiliza taarifa za ushindi tegemea ushindi pia.

Hata katika maisha yetu ya kawaida kabisa kuna watu wengi waliamua kufanya vitu kutokana na taarifa fulani waliosikia kwa wengine. Aina hii ya taarifa tunaweza kuiita ni ushuhuda. Mfano: Watu wengi katika biashara ya simu mara nyingi wanahama katika mitando yao kwenda mitandao mingine kwasababu ya kusikia taarifa(ushuhuda)toka kwa mwingine kwamba huku kuna nafuu kuliko sehemu nyingine.Kinachomfanya huyu mtu kufanya maamuzi ya kuhama ni ile taarifa (ushuhuda)aliyoipata kutoka kwa mwingine,Hivyo maamuzi yake yameathiriwa na taarifa aliyoisikia.

Mfano: 2 Watu wengi sasa wanaamua kuondoka vijijini kukimbilia mjini kutokana na taarifa wanazozipata kwamba mjini kuna maisha mazuri kuliko kijijni.Inawezekana ikawa si taarifa sahihi lakini tayari mtu kashafanya maamuzi kutokana na aina ya taarifa aliyoipata.Hata makanisani watu wanahama kutokana na taarifa wanazozipata zinazowapelekea wao kuamini kwamba kuna matokeo tofauti atakayoyapata, Haijalishi kama lengo hua linatimia au halitimii....kikubwa hapa ni kwamba kitu kilichomsababisha mtu kufanya maamuzi aliyofanya ni ile taarifa aliyoipata.


Tuendelee wiki ijayo...
Unaweza kuwasiliana na mwandishi kupitia namba 0653-318117, ama kwa barua pepe fredymsungu@gmail.com

Alhamisi, 1 Mei 2014

TAFSIRI YA NAMBA 5 KATIKA MAANDIKO


Mchungaji Peter Mitimingi, mkurugenzi wa The Voice of Hope Ministries (VHM).

Namba TANO ni namba ya neema ya maajabu ya Mungu.
Nakutakia Neema na Maajabu ya Mungu katika MWezi huu wa 5

1. Mwanzo 1:20, 21 tunasoma udhihirisho wa neema ya Mungu katika kuumba. Aliumba viumbe hai katika siku ya TANO.
2. Katika Mwanzo 15:9, Mungu aliagiza wanyama WATANO wachinjwe.
3. Isaya 9:6 inamtaja Yesu katika nafsi TANO, (Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani).
4. Yesu aliwalisha watu zaidi ya elfu TANO na mikateilikuwa MITANO.
(Mt 15:13
5. Waefeso 4:11, Kristo alitoa huduma TANO kwa Kanisa. (Mitume, Manabii, Wachungaji, Wainjilisti na Waalimu.
6. Katika Mambo ya Walawi waliamriwa kutoa sadaka za aina TANO. (Sadaka ya Ondoleo la Dhambi, Sadaka ya Asili, Sadaka ya Matendo ya Dhambi, Sadaka ya Amani).
7. Kulikuwa na wanawali wa TANO wenye busara na WATANO wapumbavu
8. (Mt 25:34)
9. Namba TANO imetajwa mara 318 katika maandiko.
10. Amri 10 zimegawanyika katika mafungu mawili, amri TANO za kwanza zinazungumzia juu ya uhusiano wetu na Mungu, na amri TANO zingine zinazungumzia juu ya uhusiano wetu sisi kwa sisi.
11. Katika agano la kale mwizi lazima alipe mara TANO ya thamani ya mifugo aliyoiba.(Kutoka 22:1)
1 “Mtu akiiba ng'ombe au kondoo, na kumchinja, au kumwuza; atalipa ng'ombe watano badala ya ng'ombe mmoja, na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja”
Nawewe kila ambacho shetani ameiba mwezi huu lazima arudishe mara tano ya thamani yake sema amen.

13. Benjamin aliheshimiwa na Yusufu kwa kupewa nafaka mara TANO zaidi ya kaka zake. (Mwanzo 43:34)
“34 Wakapelekewa sehemu za chakula kutoka mezani pake, lakini akazidisha sehemu ya Benyamini iwe kubwa mara TANO kuliko zao. Wakanywa, wakafanya furaha pamoja naye.”

14. Namba Tano inawakirisha Neema ya Mungu na hii inaonekana katika muundo wa hema ya kukutania kule jangwani. (Kutoka Sura ya 26)
• Nguzo zilikuwa dhiraa TANO mbali na mikono mitano ya juu.

• Madhabahu ya shaba ilikuwa mikono MITANO kwa mikono mitano.

• Kulikuwa na nguzo TANO mwishoni mwa Patakatifu.

• Pande za maskani zilikuwa kushinikizwa na baa TANO kila upande (Kutoka 26:26-27)
Nawe fanya mataruma ya mti wa mshita; mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa maskani, 27 na mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande wa pili wa maskani, na mataruma matano kwa ajili ya mbao za upande wa maskani ulio nyuma kuelekea magharibi.

• Mfuniko wa ndani mwa hema ulikuwa na mapazia matano ambayo yaliambatanishwa na mapazia MATANO mengine na kufanya jumla ya mapazia 10. (Kutoka 26:3)
3 Mapazia matano yataungwa pamoja, hili na hili; na mapazia MATANO mengine yataungwa pamoja, hili na hili.”

• Kulikuwa na makuhani halisi watano Haruni na watoto wake wanne (Kutoka 28:1)
“Nawe umlete Haruni ndugu yako karibu nami, na wanawe pamoja naye, miongoni mwa wana wa Israeli, ili anitumikie katika kazi ya ukuhani. Haruni, na Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari, wana wa Haruni.”

15. Kulikuwa na Matao TANO katika lile birika la Bethaida. (Yohana 5:2)
2 Na huko Yerusalemu penye mlango wa kondoo pana birika, iitwayo kwa Kiebrania Bethzatha, nayo ina matao matano

16. Kitabu cha Zaburi kimegawanyika katika sehemu huu TANO
• Zaburi 1- 41
Inahusu sikukuu ya Pasaka, mwanzo wa Israeli, na mwanzo wa mpango wa Mungu wa wokovu kuelekea Kristo.

• Zaburi 42 – 72
Inahusu juu ya ishara ya umoja wa Israel katika ardhi na inatoa picha ya uumbaji wa kanisa la Agano jipya.
• Zaburi 73 – 89
Laana juu ya uharibifu wa hekalu la Mungu na mji wa Yerusalem. Sehemu hii pia inazungumzia juu ya siku za mwisho na dhiki kuu.

• Zaburi 90 – 106
Kufurahia zaidi ya 1,000 ya utawala wa Yesu na inaonyesha Israeli walikutana tena

• Zaburi 107 – 150
Inatoa picha ya wakati ambapo Yuda (mwakilishi wa Israel) atakapokombolewa tena.

KAMA UMEBARIKIWA SEMA AMEN!

Jumatano, 30 Aprili 2014

HABARI PICHA KUTOKA MBEYA: MAZISHI YA ALIYEKUWA MKURUGENZI WA WANAWAKE WA INJILI EAGT


Picha ya marehemu Mama Benja (Junitha B. Mwamnyila)

Shujaa umekwenda, Kazi umemaliza mama kapumzike, ni baadhi ya maneno yaliyosikika na GK kwa waombolezaji waliojitokeza katika viwanja vya kanisa la EAGT Gilgal Mwanjelwa kuuaga mwili wa Mwinjilisti na Mkurugenzi wa WWI Taifa Mama Benja na kisha kwenda kuulaza kwenye nyumba ya milele maeneo ya Sabasaba.


Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio yaliyojiri kama ambavyo GK iliahidi kukuletea baada ya kupiga kambi msibani hapo, ambapo awali ilikupa picha za awali.

VIONGOZI WAKUU WA EAGT TAIFA NA WACHUNGAJI



















Mchungaji Daniel Kulola



MKE WA MAREHEMU MOSES KULOLA NAE ALIKUWEPO







WATOTO NA NDUGU WA MAREHEMU MAMA BENJA













MARAFIKI WALIKUWEPO KUFARIJI







WATU MBALIMBALI WALIJITOKEZA KUAGA
















WENGINE WALISHINDWA KUJIZUIA




















MWILI ULISHUSHWA KABURINI












MAVUMBINI TUTARUDI






Marehemu ameacha watoto wanne, ambapo uzao wake wote umekuwa watoto mapacha, mara ya kwanza akijifungua mapacha wa kike, na kisha uzao wake wa pili ukiwa mapacha tena, wa kike na wa kiume. Na katika maisha yake, Mama Benja (Benjamin likiwa jina la marehemu mume wake aliyekwisha fariki miaka mingi iliyopita) amekuwa mwinjilisti hodari na kushika nyadhifa mbalimbali kwenye kanisa la Evangelistic Assemblies of God.


Kama hukupata fursa ya kusikia maneno yake ya mwisho, basi bofya hapa, usikie alichosema marehemu ambaye alizaliwa tarehe 2 Oktoba 1951, na kufariki dunia tarehe 24 Aprili 2014. Kwa watumiaji wa simu bofya hapa kuipakua. Gospel Kitaa inawaombea wafiwa wote wapate nguvu katika kipindi hiki kigumu. BWANA ametoa, na BWANA ametwaa, jina la BWANA lihimidiwe.